Hilo ni kosa mojawapo linalofanywa na watumishi wengi wa Mungu sasa, ikiwa Mungu amekupa ujumbe kwa mwanasiasa, basi utoe kulingana na maagizo ya ki-Mungu, na usiwe wakati wa wewe kila jambo la kisiasa upo, kampeni upo, jeshi la polisi upo, bungeni upo, ..n.k..vikao vya kisiasa mtaani kwako upo, mijadala ya kisiasa upo, Hayo ni mambo ambayo kwa nje unaweza ukaona upo sahihi lakini nyuma yake unajiangamiza mwenyewe.