AHADI ZA MUNGU.

by Admin | 18 July 2020 08:46 pm07

Ahadi za Mungu ni za kweli kabisa,.. Lakini tatizo kubwa linalotukabili  sisi wanadamu ni kutokujua njia Mungu anazozitumia kutimiza ahadi zake.

Na hiyo inawafanya watu wengi waishie kukata tamaa pale anapoona mbona ahadi za Mungu zimechelewa, pengine nimemkosea Mungu, au Hanisikii..

Fahamu kuwa wakati wa Mungu kutimiza ahadi zake, sio lazima uwe ule wakati ulioupanga wewe Tena mara nyingi huwa anauchagua ule wakati ambao haufahau, wakati ambao mambo yote yanaokana yameharibika, mipango imevurugika, umeshachelewa, hapo ndipo Mungu anasimama ili kutimiza ahadi zake kwako.

Na hakupewa tu mtoto basi, bali na mwili wake pia ulirudishwa na kuwa kama wa kijana, yeye pamoja na mke wake Sara.

Lakini Ibrahimu katika kipindi chote hicho hapo katikati hakumkosea Mungu imani na ndio maana akaitwa baba wa Imani, tunasoma hilo katika..

Warumi 4:18 “Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa, ili apate kuwa baba wa mataifa mengi, kama ilivyonenwa, Ndivyo utakavyokuwa uzao wako.

19 Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani, alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa, (akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia), na hali ya kufa ya tumbo lake Sara.

20 Lakini akiiona ahadi ya Mungu hakusita kwa kutokuamini, bali alitiwa nguvu kwa imani, akimtukuza Mungu;

21 huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.

22 Kwa hiyo ilihesabiwa kwake kuwa ni haki”.  

Na hazikutimia akiwa nyumbani mwa Potifa hapana, bali zilitimia akiwa gerezani, mahali ambapo hapana tumaini lolote, la kuishi. Kwa kipindi karibu cha miaka 2 akiwa kule gerezani, siku moja isiyokuwa na jina Mungu alimtembelea na kumwinua, akatoka na kufanywa kuwa Waziri mkuu na makamu wa Raisi wa taifa kubwa lililokuwa lina nguvu kuliko yote ulimwenguni wakati ule (Misri).

Hivyo zipo ahadi za Mungu nyingi katika biblia ambazo tukianza kuzichambua hapa moja baada ya nyingine hatuwezi kumaliza zote..

Ahadi za Mungu kwa mkristo:

Hiyo ni kutupa tu hamasa mimi na wewe ambao pengine umesubiria ahadi za Mungu kwa muda mrefu sasa na bado hujaona matokeo yoyote. Unachopaswa kufanya ni kusubiri ndugu yangu, huku ukiendelea kumtumikia Mungu kwa moyo ule ule wa kwanza.

Unaweza ukawa ni mtumishi wa Mungu, na umejaribu kuacha kila kitu ili tu uifanye kazi yake..Nataka nikuambie endelea hivyo hivyo, upo wakati utafika ile hadi yake ya kuwa UTAPATA MARA MIA, itatimia juu yako, haijalishi ni miaka miwili tokea sasa, au 5 au 10 au 20, lakini fahamu kuwa ukiendelea kung’ang’ania njia yako bila kuiacha, utavuna ulichopanda.

Mungu atakulipa tu, mema, ukiwa hapa hapa duniani, na vyote ulivyovipoteza utarejeshewa vyote mara mia. (Marko 10:28-30) Hivyo endelea kumtumikia MUNGU.

Vilevile Bwana aliposema, usisimbukie maisha ule nini, unywe nini, avae nini, bali utafute kwanza ufalme wake na haki yake na hayo mengine utazidishiwa. Basi fahamu kuwa ukijikita kuutafuta kwanza uso wa Mungu, na kutaka kumjua yeye, ni ahadi yake kuwa  hatakuacha ufe njaa, bali atahakikisha kuwa anakuhudumia ili uendelee kuishi,..Kwasababu unautafuta ufalme wake..Hiyo ni kweli kabisa hawezi kudanganya.. Ahadi za Mungu ni thabiti.

Vivyo hivyo na ahadi nyingine yoyote aliyowahi kukuahidia , endelea tu kuingoja, wakati wake utafika tu,. Kikubwa usiuache wokovu wako na utakatifu wako kama wewe umeokoka.

Lakini kama hujaokoka, basi hakuna ahadi yoyote ya Mungu inayoweza kutimia juu yako. Hivyo unachopaswa kufanya ni kumpa Kristo maisha yako ili ayaokoe, kwani hizi ni siku za  mwisho na Unyakuo upo karibu,..Moja ya hizi siku mabadiliko makubwa sana yatatokea duniani. Na dhiki kuu itaanza, hivyo mgeukie muumba wako kabla ya hizo za hatari hazijakufikia kwa ghafla.

Bwana akubariki.

Ahadi za Mungu ni Yakini.

Mada Nyinginezo:

KWA KUVUMILIA AKAIPATA ILE AHADI.

TABIA YA KIPEKEE USIYOIJUA KUHUSU NENO LA MUNGU.

UNYAKUO.

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

FAHAMU JINSI KRISTO ANAVYOPONYA WATU ROHO.

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/18/ahadi-za-mungu/