WAFIRAJI KWENYE BIBLIA.

by Admin | 18 July 2020 08:46 pm07

Je! biblia inasema nini juu ya wafiraji?


Ufiraji ni Neno  linalojumisha kitecho chochote cha kumwingilia mwanadamu mwanzako  kimapenzi kinyuma na maumbile.

Na ni dhambi biblia imesema hivyo na kwamba watu wote wanaofanya vitendo kama hivyo hawawezi kuurithi uzima wa milele.

1Wakoritho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; waasherati hawataurithi ufalme wa Mungu, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala WAFIRAJI, WALA WALAWITI,

10 wala wevi, wala watamanio, wala walevi, wala watukanaji, wala wanyang’anyi”.

Watu wengi wanajidanganya na kudhani kuwa wakiwaingilia wake zao, maadamu tayari wapo nao katika ndoa, sio dhambi..Ndugu usidanganyike, tendo lolote la kumwingilia mtu mwingine kinyume na maumbile haijalishi ni rafiki, au jirani, au kahaba, au mke, hiyo tayari ni ufiraji.

Na wafiraji wote watahukumiwa.

Kilichosababisha Sodoma na Gomora viangamizwe, kilikuwa ni kitendo hichi cha ufiraji,

Yuda 1:7 “Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.
8 Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu”.

Hivyo kama wewe ni mmojawapo tubu haraka sana, kwa kuacha kitendo hicho. Mgeukie Yesu Kristo ayaokoe maisha yako. Ikimbie hukumu ya Mungu. Ziwa la moto lipo kweli.

Jiepushe na utazamaji wa picha na video chafu za ngono zinazozagaa mitandaoni, watu wengi wanaingiliwa na hizi roho kwa kuzitazama tu. Utakuta hapo mwanzo, hakuwa hivyo lakini siku alipooanza kuzitazama tu, anaona kama, shinikizo fulani la nguvu linatoka ndani kumuhimiza kufanya hivyo.

Kama na wewe ni mmoja wapo basi, nakushauri, kaa mbali sana na mambo hayo, shetani anafahamu kuwa wakati wake ni mfupi aliobakiwa nao. Hivyo itazame sana mienendo yako.

Mada Nyinginezo:

JINSI SODOMA NA GOMORA ILIVYOKUWA INAVUTIA SANA..

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

SI KILA KIPENDEZACHO KINATOKA KWA BWANA.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/18/wafiraji-kwenye-biblia/