Mkatale ni nini katika biblia? (Matendo 16:24)

by Admin | 16 September 2020 08:46 am09

Mkatale ni nini?


Mkatale ni pingu ya kufungia mtu, inaweza ikawa ya chuma, au mbao nene. Na huwa inafungwa sana sana miguuni, lakini pia shingoni au mikononi,.. Tazama picha juu.

Vifungu vinavyolitaja Neno hilo katika biblia ni kama vifuatavyo;

Matendo 16:24 “Naye akiisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani, akawafunga MIGUU KWA MKATALE.

25 Lakini panapo usiku wa manane Paulo na Sila walikuwa wakimwomba Mungu na kumwimbia nyimbo za kumsifu, na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza.

26 Ghafula pakawa tetemeko kuu la nchi, hata misingi ya gereza ikatikisika, na mara hiyo milango ikafunguka, vifungo vya wote vikalegezwa”.

 

Ayubu 13:25 “Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo? Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?

26 Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu, Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;

27 Waitia MIGUU YANGU KATIKA MKATALE, na kuyaaua mapito yangu yote; Wajiandikia alama kuzizunguka nyayo za miguu yangu”;

 

Yeremia 20:2 “Ndipo Pashuri akampiga Yeremia, nabii, AKAMTIA KATIKA MKATALE, uliokuwa pale penye lango la juu la Benyamini, lililokuwa katika nyumba ya Bwana. 3 Hata ikawa, asubuhi, Pashuri huyo akamtoa Yeremia katika MKATALE. Ndipo Yeremia akamwambia, Bwana hakukuita jina lako Pashuri, bali Magor-misabibu”.

Soma pia  Ayubu 33:11, 2Nyakati 16:10, Yeremia 29:26.


 

mkatale ni nini

Hata sasa shetani anawatia watu katika mikatale yake ya mauti. Lakini Yesu Kristo peke yake ndiye anayeweza kuwatoa humo.  Swali ni Je! Mimi na wewe Yesu ameshatuweka huru?.  Kumbuka hakuna uhuru wowote nje ya Kristo, haijalishi unajiona upo salama kiasi gani, wewe bado upo kwenye mikatale mibaya ya shetani. Na lengo lake ni ufe katika hali hiyo uishie kuzimu.

Hivyo kama hujaokoka, mgeukie Kristo mapema ayaokoe maisha yako, ndani ya hichi kipindi kifupi tulichobakiwa nacho hapa duniani.

Zaburi 107:13 “Wakamlilia Bwana katika dhiki zao, Akawaponya na shida zao.

14 Aliwatoa katika giza na uvuli wa mauti, Akayavunja mafungo yao.

15 Na wamshukuru Bwana kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.

16 Maana AMEIVUNJA MILANGO YA SHABA, AMEYAKATA MAPINGO YA CHUMA”.

Bwana akubariki.

Tazama ufananuzi wa maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

KAMA MMOJA TU NDIO HIVI! SI ZAIDI 153?

KILA MMOJA WENU AJUE KUUWEZA MWILI WAKE.

Nyamafu ni nini?

MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.

 

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/09/16/mkatale-ni-nini-katika-biblia-matendo-1624/