Uchaji ni nini kama tunavyosoma katika 1Timotheo 2:10?

by Admin | 1 December 2020 08:46 pm12

Tusome..

1Timotheo 2:10 “bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”

Uchaji ni kitendo cha “kumcha Mungu”. Ni sawa na neno “Ulaji wa chakula” ni neno linalotokana na kitendo cha “kula chakla” Na vivyo hivyo uchaji, ni kitecho cha kumcha Mungu.

Lakini tukirudi kwenye mstari huo, tukianzia juu kidogo kina jambo lingine la kujifunza..Tusome,

1Timotheo 2.9 “Vivyo hivyo wanawake na wajipambe kwa mavazi ya kujisitiri, pamoja na adabu nzuri, na moyo wa kiasi; si kwa kusuka nywele, wala kwa dhahabu na lulu, wala kwa nguo za thamani;

10  bali kwa matendo mema, kama iwapasavyo wanawake wanaoukiri uchaji wa Mungu”

Mstari huo unawahusu wanawake, yaani vigezo vya wanawake wanaoukiri Uchaji wa Mungu, kwamba wanapaswa wawe watu wa kujisitiri, maana yake ni kuwa mwanamke ambaye hajisitiri, haijalishi anafanya kazi gani ya kanisa, au anamwimbia Mungu..Bado Hamchi Mungu..Huyo ni wa kidunia, ni mfano wa Yezebeli.

Kumbuka hili binti wa Mungu, Mwanamke hapaswi kuvaa hereni, mikufu, hapaswi kuvaa suruali (iwe pana au nyembamba), hapaswi kuchonga nyusi, hapaswi kusuka rasta, hapaswi kupaka rangi kucha, wala kupaka rangi mdomoni na mambo mengine yanayofanana na hayo. Na sababu pekee ni kwamba Miili yetu ni hekalu la Roho Mtakatifu, na sisi sio mali yetu wenyewe, ni mali ya mwingine hivyo hatuna uhuru asilimia zote wa kufanya yale tunayotaka.

Kadhalika mwanamke asiye na adabu na moyo wa kiasi, huyo pia Hamchi Mungu haijalishi anahudhuria kanisani mara ngapi, au anaimba kwaya. Huyo ni wa shetani.

Hivyo mwanamke/mama/dada kama huukiri Uchaji wa Mungu kwa kufanya hayo yaliyoorodheshwa hapo juu. Huu ni wakati wako wa kukata shauri la kuokoka. Kwasababu bado ulikuwa hujaokoka kama ulikuwa unavaa vimini. Basi tubu leo na kumpokea Yesu, na ukabatizwe ufanyike kiumbe kipya, na Roho Mtakatifu atakuja juu yako kukutengeneza kama anavyotaka Mungu.

Marana atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312


Mada Nyinginezo:

Mlango uitwao “Mzuri” Unaozungumziwa katika Matendo 3:2 ndio upi?

UFUNUO: Mlango wa 1

NITAONGEZAJE NGUVU ZANGU ZA ROHONI?

OLE WAO WANAOJITAHIDI KUMFICHA BWANA MASHAURI YAO.

USHIRIKINA NA MADHARA YAKE.

Je tunapaswa tushiriki Meza ya Bwana mara ngapi?

MAMBO 5 AMBAYO KILA MKRISTO ANAPASWA KUFAHAMU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/12/01/uchaji-ni-nini-kama-tunavyosoma-katika-1timotheo-210/