Swali: Kurushwa upesi kunakozungumziwa katika Danieli 9:21 ndio kupi?

by Admin | 21 December 2020 08:46 pm12

Jibu: Tusome.

Danieli 9:21 “naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza, akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni”.

Kurushwa upesi kunakozungumziwa hapo ni “kuruka kwa haraka” au kwa lugha rahisi zaidi ni “kuruka/kupaa kwa spidi”. Ndege wa angani huruka kwa upesi..Kwa mfano ni rahisi kumsogelea ndege kama njiwa, na akikuona tu, mara ghafla utamwona kapiga mbawa na kupotelea kwenye ukingo wa anga. Hiyo ndiyo maana ya kuruka kwa upesi.

Na Biblia inasema hapo Danieli alimwona Malaika Gabrieli akirushwa kwa upesi na Mungu..  Maana yake alikuwa anamwona katika maono, akija kwa kasi, na akiondoka kwa kasi.

Kumbuka wapo malaika wenye mbawa na wasio na mbawa (maana yake wasioruka)..Gabrieli ni miongoni mwa malaika wenye mbawa, na wa kupeleka ujumbe kwa watu.

Ni kawaida kile kitu kinachopeleka ujumbe kwa haraka sana ni bora kuliko kile kinachopeleka kwa taratibu. Hivyo Gabrieli ni malaika mwenye sifa ya kupeleka ujumbe kwa haraka sana

Malaika Gabrieli ameonekana katika agano la kale na vile vile katika agano jipya. Katika agano la kale, ndio hichi kipindi cha Nabii Danieli alipotumwa ampe ujumbe juu ya mambo yanayokuja.

Na katika Agano jipya alionekana kipindi cha Kuhani Zakaria, Baba yake Yohana Mbatizaji, alipotumwa na Mungu ampe ujumbe kuhusu kuzaliwa kwa Yohana Mbatizaji ambaye atatangulia kumtengenezea Bwana njia (Soma Luka 1:19). Na pia kipindi kifupi baadaya akaja kuonekana tena kwa Bikira Mariamu kumpa ujumbe wa kubeba mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu (Unaweza kusoma Luka 1:26).

Na hata leo Malaika Gabrieli anatumwa kwa watu wengi duniani walio waaminifu kwa Mungu kuwapa jumbe mbalimbali.

Kama utapenda kujua zaidi kuhusu Malaika unaweza kufungua hapa >> Malaika

Je umempokea Kristo?. Yesu anarudi.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

Je! Kuna malaika wangapi mbinguni?

MALAIKA WAPELELEZI WA HUKUMU WANAPITA SASA.

Je! mbinguni kuna malaika wa kike?. Na je! tukifika mbinguni tutafanana wote?

Kwanini Mungu anasema “Afanyaye malaika zake kuwa pepo”?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/12/21/swali-kurushwa-upesi-kunakozungumziwa-katika-danieli-921-ndio-kupi/