Makuruhi ni nini, kama tunavyosoma katika biblia?

by Admin | 5 June 2021 08:46 pm06

Makuruhi; Ni neno linalomaanisha “kuchukiza kuliko pitiliza”, Kwa mfano mtu akisema mabeberu ni makuruhi kwa waafrika. Anamaanisha kuwa mabeberu ni watu wanaochukiza sana/ au ni harufu mbaya sana kwa waafrika, hawapendwi hata kidogo. Na hiyo yote ni kwasababu ya maumivu ambayo pengine walishawahi kuyapata kutoka kwao enzi za utumwa.

Vivyo hivyo neno hili katika biblia utalisoma katika mstari huu;

1Samweli 13:4 “Waisraeli wote wakasikia habari ya kwamba Sauli ameipiga hiyo ngome ya Wafilisti, na ya kwamba Waisraeli wamepata kuwa MAKURUHI kwa Wafilisti. Basi hao watu wakakusanyika pamoja kumfuata Sauli huko Gilgali.

5 Nao Wafilisti wakakusanyana ili wapigane na Waisraeli, magari thelathini elfu, na wapanda farasi sita elfu, na watu kama mchanga ulio ufuoni mwa bahari kwa wingi wao; wakapanda juu, wakapiga kambi yao katika Mikmashi, upande wa mashariki wa Beth-aveni”.

Habari hiyo ni baadaya ya Israeli kuwaivamia kambi mojawapo ya wafilisti na kuipiga, na kisha kujigamba baada ya hapo, Hivyo wafilisti walivyosikia hivyo ikawabidi wawachukie Israeli kupitiliza, mpaka ikawabidi wafilisti wote waungane na idadi yao ikawa kama mchanga wa bahari ili waifutilie Israeli mbali, hiyo yote ni  kwasababu tayari wameshafanyika kuwa makuruhi kwao.

Lakini kama tunavyoijua habari ni kuwa, walikuja kuuliwa wote, na waisraeli kwa msaada wa Mungu.

Jambo kama hili linajirudia leo hii, Vita kati ya Israeli na Palestina.  Wapalestina (ambao ndio wafilisti wa kipindi kile), sasa wanawachukia wayahudi kupitiliza, Israeli imekuwa harufu mbaya kwao, na hiyo yote ni kutimiza maandiko. Ili baadaye Mungu aje kujichukulia utukufu kutoka katika vita ambavyo vitakavyopiganwa siku za hivi karibuni pale Israeli ( Soma Ezekieli 38 &39).

Na sio tu ni makuruhi kwa  wapalestina peke yao. Hapana bali wataendelea kuwa hivyo, mpaka kwa dunia nzima. Ili kutimiza unabii wa vita ile kuu ya Har Magedoni ambayo itapiganwa pale Israeli, siku za mwisho. Vita hiyo itakuwa kati ya Israeli na mataifa yote duniani.

Zekaria 12:3 “Tena itakuwa siku hiyo, nitafanya Yerusalemu kuwa jiwe la kuwalemea watu wa kabila zote; wote watakaojitwika jiwe hilo watapata jeraha nyingi; na mataifa yote ya dunia watakusanyika pamoja juu yake”.

Kwa urefu wa vita hiyo na mambo hayo yatakayotokea fungua link hii > https://wingulamashahidi.org/2018/07/17/siku-ya-bwana-inayotisha-yaja/

Hivyo ndugu, unapoona migogoro inayoendelea Israeli leo hii, usidhani ni ishara nzuri kwako wewe mwenye dhambi. Hiyo ni ishara ya Israeli kurudiwa na Mungu. Na moja ya hizi siku tutaona mabadiliko ya ghafla katika hii dunia. Na mabadiliko hayo yakishatokea tujue kuwa Unyakuo utakuwa umeshapita wakati huo, kanisa lipo mbinguni kwenye karamu ya mwana-kondoo.

1Wathesalonike 5:3 “Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa”.

Jiulize, mabadiliko hayo yakitokea leo, wewe utakuwa wapi?

Majibu yote yapo moyoni mwako.

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

JE NI KWELI SAMAKI NGUVA YUPO?

NAYE AKASIMAMA JUU YA MCHANGA WA BAHARI.

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/06/05/makuruhi-ni-nini-kama-tunavyosoma-katika-biblia/