Kujuzu ni nini kama tunavyosoma katika 2Wakorintho 12:4?

by Admin | 16 June 2021 08:46 am06

Labda tuanzie kusoma kuanzia juu kidogo,

2Wakorintho 12:2 “ Namjua mtu mmoja katika Kristo, yapata sasa miaka kumi na minne, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua). Mtu huyo alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu

3 Nami namjua mtu huyo, (kwamba alikuwa katika mwili sijui; kwamba alikuwa nje ya mwili sijui; Mungu ajua

 4 ya kuwa alinyakuliwa mpaka Peponi, akasikia maneno yasiyotamkika, ambayo haijuzu mwanadamu ayanene”

Neno kujuzu maana yake ni “kutoruhusiwa”. Hivyo hapo Paulo alikuwa anaelezea maono aliyoyaona, kwamba alinyakuliwa mpaka mbingu ya tatu na kuambiwa maneno ambayo hakuruhusiwa kuyasema kwa watu.

Neno hilo pia tunalisoma katika kitabu cha Mwanzo..

Mwanzo 34: 7 “Wanawe Yakobo waliposikia hayo, wakaja kutoka nyikani; nao wakasikitika sana, wakakasirika mno, kwa sababu amefanya upumbavu katika Israeli kwa kulala na binti Yakobo, neno LISILOJUZU kutendeka”

Hata katika imani yapo mambo ambayo hayajuzu kuyafanya..Kwa mkristo aliyeokoka, haijuzu kuupenda ulimwengu, haijuzu kuishi maisha ya dhambi na anasa, haijuzu kuwa mtukanaji, haijuzu kuwa mwizi na tapeli, haijuzu kuwa mzinzi na mwasherati, haijuzu kuwa mlevi, haijuzu kujifunga nira na watu wasioamini, na mambo mengi yote yanayofanana na hayo. Zaidi sana tunapaswa tujiweke katika hali ya usafi na utakatifu na kuchukua msalaba watu na kumfuata Yesu kila siku katika maisha yetu, kwasababu biblia inasema pasipo huo utakatifu hakuna mtu atakayemwona Mungu.

Waebrania 12:14 “Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao”.

Bwana atubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

BIBLIA INAITAJA NJIA KUU YA MFALME, NJIA HII NI IPI?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

KWANINI MIMI?

MUUNGANO WA DINI NA MADHEHEBU YOTE, UMEKARIBIA.

MAWE YALIYOKWISHA KUCHONGWA MACHIMBONI.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/06/16/kujuzu-ni-nini-kama-tunavyosoma-katika-2wakorintho-124/