Kama Mungu ndiye kaumba kila kitu, je ni yeye huyo huyo ndiye aliyeumba dhambi pia?

by Admin | 7 July 2021 08:46 am07

Jibu: Ni vizuri kufahamu kuwa kuna vitu vimeumbwa na Mungu na kuna vitu vimeumbwa na viumbe wa Mungu.

Kwa mfano Mungu hajaumba gari, wala treni, wala pikipiki. Gari tunaloendesha limeumbwa na wanadamu, vile vile hajaumba ndege, wala kiti, mambo hayo yote ni sisi wanadamu ndiyo tuliyoyatengeneza… tumeichukua malighafi hii iliyoumbwa na Mungu, tukaichanganya na malighafi ile, tukatengeneza gari. N.k

Vile vile Mungu hajaumba chapati tunazokula wala maandazi, wala pilau.. alichokiumba ni malighafi hizo, yaani unga, mafuta, chumvi na maji.. Kwa utashi wetu sisi wanadamu, ndio tukachukua malighafi hizo na kuzichanganya pamoja na kuzichoma ndipo vikatokea vyakula hivyo tunavyokula kama maandazi au chapati au chakula kingine chochote.

Kadhalika Mungu hajaumba dhambi, wala matatizo wala shida.. Mambo hayo ni sisi tumeyatengeneza wenyewe, kupitia malighafi au vitu ambavyo Mungu kaviumba. Tunapochukua ukweli na kuuchanganya na vitu vingine na kuugeuza hapo ndipo unapozaliwa uongo!.. Ndio DHAMBI YENYEWE!!

Kitendo cha kukutana kimwili si kibaya lakini kinapofanyika wakati usio sahihi, au na mtu asiyesahihi kinageuka kuwa uzinzi au uasherati, Hivyo uasherati ni kitu sahihi kilichochanganywa na muda usio sahihi na mtu asiyesahihi. Kwahiyo Mungu hajaumba uasherati, bali ni watu ndio walioumba uasherati.

Hivyo dhambi zote zimeumbwa na wanadamu pamoja na shetani na malaika zake. Na si Mungu aliyeziumba kwasababu yeye ni mtakatifu, na wala hachangamani na uchafu. Ndio maana anaichukia dhambi.. Kwasababu ingekuwa ni yeye kaiumba asingeichukia.. Mtu hawezi kuchukia kitu alichokitengeneza yeye mwenyewe..

Na kila siku dhambi zinaendelea kuumbwa na wanadamu.. Ndio maana biblia inasema siku za mwisho maasi yataongezeka, maana yake kila siku maovu mapya yanazaliwa..Ndio maana katika kilele cha maovu haya Bwana lazima aiangamize hii dunia.

Hivyo hatuna budi kukaa mbali na dhambi, kwasababu Mungu wetu ni mtakatifu na wala hachangamani na dhambi.

Mathayo 5:48 “Basi ninyi mtakuwa wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu”.

Na hatuwezi kuishinda dhambi tukiwa nje ya agano la mwanae mpendwa Yesu. Tunaishinda dhambi na kuacha kuiumba kwa kuungama dhambi zetu zote, kwa kumaanisha kutozitenda tena, na kisha kwenda kubatizwa ubatizo sahihi na kupokea Roho Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya “Bwana Yesu ni mzaliwa wa kwanza wa waliokufa?”(Ufunuo 1:5)

SISI NI WINDO BORA SANA, LA DHAMBI.

Tofauti kati ya uchafu wa mwilini na rohoni ni  ipi?

Maswali na Majibu

JE! NI DHAMBI KUIMBA WIMBO WA TAIFA?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/07/07/kama-mungu-ndiye-kaumba-kila-kitu-je-ni-yeye-huyo-huyo-ndiye-aliyeumba-dhambi-pia/