Nini maana ya “Amali” na “Ijara” katika biblia?

by Admin | 9 July 2021 08:46 am07

Jibu: Shalom.

Neno “Amali” maana yake ni “kazi ngumu” hususani ile inayohusisha mwili, kama vile kazi ya kibarua cha kulima au kukata mti.

Katika biblia neno hilo limeonekana mara nne..

Mhubiri 4: 4 “Tena nikafikiri AMALI ZOTE, na kila kazi ya ustadi, ya kwamba inatoka katika mtu kupingana na mwenzake. Hayo nayo ni ubatili na kujilisha upepo”.

Mistari mingine inayoainisha neno hilo ni pamoja na Mhubiri 4:8, Mhubiri 5:19,  na Mhubiri 8:15.

Neno “Ijara” maana yake ni “mshahara anaolipwa mtu kwa siku”. kumbuka mshahara anaolipwa mtu kwa mwezi hauitwi Ijara, Ijara ni mshahara wa siku tu, mara nyingi unawahusu vibarua.

Walawi 19:13 “Usimdhulumu jirani yako, wala kumnyang’anya mali yake; IJARA YAKE aliyeajiriwa isikae kwako usiku kucha hata asubuhi”.

Isaya 3:11 “Ole wake mtu mbaya; shari itakuwa kwake, kwa maana atapewa IJARA ya mikono yake”

Isaya 40: 10 “Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake”.

Mistari mingine inayoanisha neno hilo ni 2Nyakati 15:7, Mhubiri 4:9, Mhubiri 9:5, Isaya 5:23, Mika 1:7, Zekaria 8:10, na 2Wakorintho 5:10.

Hivyo hakuna Amali isiyo na Ijara. Vile vile kazi ya Mungu ina ujira wake, kama Bwana alivyosema katika kitabu cha Ufunuo..

Ufunuo 22:12 “Tazama, naja upesi, na ujira wangu u pamoja nami, kumlipa kila mtu kama kazi yake ilivyo.

13 Mimi ni Alfa na Omega, mwanzo na mwisho, wa kwanza na wa mwisho.

14 Heri wazifuao nguo zao, wawe na amri kuuendea huo mti wa uzima, na kuingia mjini kwa milango yake”.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

NAMNA YA KUITAMBUA SAUTI YA MUNGU INAPOZUNGUMZA NA WEWE

AHADI YA ROHO ILIYOSALIA SASA KWA KIPINDI CHETU.

JE UNAIFANYA KAZI YA MUNGU?

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/07/09/nini-maana-ya-amali-na-ijara-katika-biblia/