Kwanini Paulo, alihukumu wakati hukumu hairuhusiwi?

by Admin | 18 August 2021 08:46 pm08

SWALI: Tukisoma katika Kitabu cha 1 Wakorintho Sura ile ya Tano, Tunaona Mtume Paulo Akizungumzia Habari Ya kutengwa Kwa Watu wenye kulichafua kanisa la Mungu,… sasa tukija katika Mstari wa 3, alisema hivi..

“ Kwa maana kweli, nisipokuwapo kwa mwili, lakini nikiwapo kwa roho, mimi mwenyewe nimekwisha KUMHUKUMU yeye aliyetenda jambo hilo, kana kwamba nikiwapo”.

Swali langu ni hili, Katika Huo mstari wa Tatu, naona Mtume Paulo anasema kwamba, mtu wa namna ile, Yaani aliye mzinzi, mlevi N.K.. yeye Amekwisha Kumuhukumu,… Sasa na Tukisoma katika kitabu cha Mathayo, 7:1, Bwana Yesu alituonya Kwamba tusihukumu, kwa maana tukihukumu mtu nasi tutahukimiwa….Sasa hapa imekaaje kaaje?


JIBU: Hukumu Mtume Paulo aliyomaanisha hapo si kuhukumu ile inayozungumziwa katika Mathayo 7..Kwamba msihukumu msije mkahukumiwa,.. Ile inayozungumziwa inakuja pale mtu anapotoa maneno yanatoa hatma ya maisha ya mtu mwingine, kana kwamba ni Mungu , kwamfano,kumwambia mwenzako wewe ni wa motoni tu, hata iweje huwezi kuokoka.  Hapo umeshahukumu. Au unapowaona wenye dhambi, kama vile mashoga, na unaanza kusema wale makafiri Mungu hawezi kuwakubali milele, dhambi zao hazifutiki,..Hapo tayari umeshahukumu.

Lakini mtume alichokimaanisha hapo sio hicho, bali alimaanisha hukumu ya ADHABU. Yaani kuadhibiwa kwa huyo mtu.

Na jambo kama hilo Mungu ameliruhusu wakati mwingine katika kanisa kufanyika.. Kwamfano katika habari hiyo ukiendelea kusoma mistari inayofuata utaona, mtume Paulo alisikia wakorintho wamejihusisha na zinaa mbaya, iliyokithiri ambayo haipo hata kwa watu wenye dhambi, yaani mtu anazini na mama yake halafu bado yupo katika kanisa. Sasa kwa kosa kama hilo Paulo akawaambia wakorintho, hata kabla hajafika tayari ameshamuhukumia adhabu mtu kama huyo. Na adhabu yenyewe ni kumkabidhisha shetani amuue, mwili aungamie ili roho ipone siku ile ya hukumu.

Hata sasa, matendo kama haya, yanaendelea katika kanisa la Kristo, leo hii limekuwa ni jambo la kawaida kusikia wachungaji wanazini na washirika wao, wengine wanavuka mipaka hadi na watoto wadogo, utasikia askofu anazini na muumini pamoja na mama yake, jambo ambalo huwezi kuliona hata kwa watu wenye dhambi. Na wenyewe wanaona ni sawa kwasababu hakuna mtu wa kuwakabidhisha kwa shetani.

Paulo anasema, ni heri ukabidhiwe kwa shetani uuawe, walau hasira ya Mungu utapoa juu yako, na siku  ile ya hukumu unusurike, kuliko kuendelea kuishi, katika hali hiyo hiyo mpaka kufa kwako, kwani adhabu yako itakuwa kubwa sana siku ile.

Luka 12:47 “Na mtumwa yule aliyejua mapenzi ya bwana wake, asijiweke tayari, wala kuyatenda mapenzi yake, atapigwa sana”.

Hivyo hiyo inatukumbusha  tuwe makini sana, katika ukristo wetu, vilevile  na katika wito wetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya msiwe waalimu wengi (Yakobo 1:3)?

Tofauti ya kazi ya Damu ya Yesu na Jina la Yesu ni ipi?

Tofauti kati ya mtume na mwanafunzi ni ipi kibiblia?

KAMA SI YESU, HABARI YETU INGEKUWA IMEISHA ZAMANI SANA.

Mungu anaposema “nitaliweka jina langu” ana maana gani?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/08/18/kwanini-paulo-alihukumu-wakati-hukumu-hairuhusiwi/