JINSI MUNGU ATAKAVYOTOA THAWABU ZAKE, NA VIGEZO ATAKAVYOTUMIA. (Sehemu ya 1)

by Admin | 18 December 2021 08:46 pm12

Bwana Yesu asifiwe, katika Makala hizi, tutazama vigezo ambavyo Mungu atavitumia kutoa thawabu zake, tutakapofika kule ng’ambo, Hii itatusaidia kuzidisha hamasa zetu katika kumtumikia Mungu, kama vile mtume Paulo, alivyoliona hilo, mpaka akasema..

Wafilipi 3:14 “nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu”.

 Tutapitia baada ya vifungu, ambavyo vitatupa picha jinsi thawabu hizo Mungu atakavyozigawa; Kigezo cha thawabu ya kwanza tunakisoma katika Mathayo 20:1-16

  1. Wapo watu watafanya kazi kidogo, lakini watalipwa sawasawa na wale waliofanya kazi nyingi.

Unaweza ukasema ni kwanini Mungu afanye hivyo? Embu tupitie Habari hii, tutapata majibu yote.

Mathayo 20 : 1-16

“1 Kwa maana ufalme wa mbinguni umefanana na mtu mwenye nyumba aliyetoka alfajiri kwenda kuajiri wakulima awapeleke katika shamba lake la mizabibu.

2 Naye alipokwisha kupatana na wakulima kuwapa kutwa dinari, aliwapeleka katika shamba lake la mizabibu.

3 Akatoka mnamo saa tatu, akaona wengine wamesimama sokoni wasiokuwa na kazi;

4 na hao nao akawaambia, Enendeni nanyi katika shamba langu la mizabibu, na iliyo haki nitawapa. Wakaenda.

5 Akatoka tena mnamo saa sita na saa kenda, akafanya vile vile.

6 Hata kama saa kumi na moja akatoka, akakuta wengine wamesimama, akawaambia, Mbona mmesimama hapa mchana kutwa bila kazi?

7 Wakamwambia, Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri. Akawaambia, enendeni nanyi katika shamba la mizabibu.

8 Kulipokuchwa, yule bwana wa shamba akamwambia msimamizi wake, Waite wakulima, uwalipe ujira wao, ukianzia wa mwisho hata wa kwanza.

9 Na walipokuja wale wa saa kumi na moja, walipokea kila mtu dinari.

10 Na wale wa kwanza walipokuja, walidhani kwamba watapokea zaidi; na hao pia wakapokea kila mtu dinari.

11 Basi wakiisha kuipokea, wakamnung’unikia mwenye nyumba,

12 wakisema, Hao wa mwisho wametenda kazi saa moja tu, nawe umewasawazisha na sisi tuliostahimili taabu na hari za mchana kutwa.

13 Naye akamjibu mmoja wao, akamwambia, Rafiki, sikudhulumu; hukupatana nami kwa dinari?

14 Chukua iliyo yako, uende zako; napenda kumpa huyu wa mwisho sawa na wewe.

15 Si halali yangu kutumia vilivyo vyangu kama nipendavyo? Au jicho lako limekuwa ovu kwa sababu ya mimi kuwa mwema?

16 Vivyo hivyo wa mwisho watakuwa wa kwanza, na wa kwanza watakuwa wa mwisho”.

Lakini ni wakina nani hawa, ambao, watakuja kulipwa sawasawa na wale waliotaabika katika kazi ya Mungu kwa muda mrefu.

Ukitazama, utaona, wale wa mwisho, hawakuwa wanashughulika mahali popote hapo kabla.. Bali mwenye shamba alipowafuata na kuwauliza kwanini mmesimama hapa mchana kutwa wakasema “Kwa sababu hakuna mtu aliyetuajiri”.. Hii ikiwa na maana kama wangebahatika kufuatwa na mwenye shamba tangu asubuhi nao pia wangefanya kazi kubwa tu kama wale wengine, lakini hakutokea mtu wa kuwaajiri mpaka jioni.

Ikifunua kuwa, kuna watu mpaka sasa bado hawajafikiwa na neema ya wokovu, na pengine umri umeenda, labda tuseme mpagani Fulani mwabudu ng’ombe, lakini akiwa na miaka 80, ndio anahubiriwa injili na kuokoka kwa kumaanisha, na baada ya hapo anakuwa tayari kumtumikia Mungu kwa moyo wake wote, pengine akamtumikia Mungu kwa uaminifu kwa mwaka 1 tu akafa.

Au mwingine, neema imemkuta katika ujana wake, labda miaka 20 tu, lakini akatumika miaka 2 tu, alipofikisha miaka 22 akafariki.

Sasa watu kama hawa, kama walitumika kwa uaminifu kwa muda huo mfupi tu. Usishangae kuwakuta kule ng’ambo wamepewa thawabu sawa mitume. Ni kwanini? Ni kwasababu wakati neema inawafikia, na muda wao wa kutumika ulipokuja, waliandikiwa muda mchache sana. Hivyo kama wangekutwa tangu zamani ni wazi kuwa wangemtumikia Mungu kwa uaminifu.

Lakini,ikiwa wewe leo hii unaisikia neema, unaichezea, leo upo na Kristo, kesho upo na shetani, yaani hueleweki, usitazamie, Kristo atakupa thawabu yoyote, ikiwa utakufa leo katika hali kama hiyo, yaani umezaliwa katika familia ya kikristo, unajua kabisa misingi ya kiimani kwamba, pasipo wokovu huwezi kwenda popote, usitazamie, utalingana na yule mpagani au mtu wa dini nyingine ambaye kaokoa hivi karibuni, halafu akafa.

Bwana alisema wamwisho watakuwa wa kwanza, na kwanza watakuwa wamwisho. Ithamini neema uliyopewa , hizi ni siku za mwisho.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

KWANINI MTINI KATIKATI YA MIZABIBU?

NI NANI ATAKAYEUCHUKUA MSALABA WA YESU?

AINA TATU ZA WAKRISTO.

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/12/18/jinsi-mungu-atakavyotoa-thawabu/