Mretemu ni mti gani?

by Admin | 21 September 2022 08:46 pm09

Swali: Ule mretemu ambao Nabii Eliya alijilaza chini yake ulikuwa ni aina gani ya mti, na je una muujiza wowote kiroho? (1Wafalme 19:4).

Jibu: Mretemu ni aina ya mti ujulikanao sasa kama “MTARAKWA”. Zipo jamii nyingi za mitarakwa kulingana na mahali na mahali. Mtarakwa unaomea katika bara la Afrika ni tofauti kimwonekano na ule unaomea katika bara la Ulaya, (kutokana na hali ya hewa). Lakini yote inamatawi yanayofanana na tabia zinazofanana, kinachoitofautisha ni unene na urefu.

Mti wa Mtarakwa (au Mretemu) ni mti unaovumilia ukame sana, na kamwe matawi yake hayapotezi rangi yake ya ukijani, hata kama yatapitia ukame mkali.

Ndio maana utaona kipindi Eliya anamkimbia Yezebeli, tayari dunia nzima ilikuwa ni jangwa kwasababu mvua haikunyesha kwa miaka mitatu na nusu, na Eliya anauona mretemu na kukaa chini ya uvuli wake, sasa kikawaida mti uliokauka na ukame hauwezi kuwa na uvuli.

1 Wafalme 19:4 “Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi CHINI YA MRETEMU. Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha; sasa, Ee BWANA, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu.

5 Naye akajinyosha akalala chini ya MRETEMU; na tazama, malaika akamgusa, akamwambia, Inuka, ule”

Kutokana na sifa hiyo, na jinsi malaika alivyomtembelea Eliya alipokuwa chini ya huo mretemu(au mtarakwa), basi inaaminika kuwa mti huo, una miujiza fulani kiroho.

Vile vile miti hii ya Miteremu/mitarakwa inatumika katika tamaduni nyingi kama miti ya Krismas (Chrismass tree).

Asili ya mti huo kutumika kama alama ya Krismasi ni hadithi ya inayoaminika na baadhi ya watu kuwa kipindi Herode anataka kumwua mtoto Yesu, pale alipotoa amri ya kuuawa kwa watoto wote walio chini ya umri wa miaka miwili, inaaminika kuwa askari wa Herode walipomkaribia Yusufu na Mariamu ili wamwue mtoto, walikuwa karibu na huu mti wa Mteremu, na ghafla ukawafungukia matawi yake yakawaficha, askari walipokuja hawakumwona Yusufu, Mariamu pamoja na mtoto.

Hiyo ndio maana mpaka leo, watu wanautumia mti huo kama alama au nembo  ya Krismas.

Lakini swali ni je!. Ni kweli mtu huo umebeba miujiza yoyote kiroho?.

Jibu ni la!. Mti wa Mretemu/Mtarakwa hauna muujiza wowote kiroho, ni mti tu kama miti mingine, sifa yake ya kuvumilia ukame ndiyo inayowachanganya wengi, lakini kiuhalisia ni mti tu kama miti mingine.

Na zaidi sana, si kweli kwamba mti huo ulimsaidia Mariamu na Yusufu kuwalinda dhidi ya Mauaji ya Bwana Yesu.. Hizi ni hadithi za kutunga, ambazo zimetungwa kwa uerevu wa akili za watu, uliovuviwa na shetani mwenyewe.

Kwasababu Yusufu tayari alikuwa ameshaondoka Bethlehemu kabla ya Herode kuanza mauaji. Hivyo kusema kwamba mti uliwasaidia huo ni uongo wa shetani.

Na si tu mti huu ni wa kawaida, bali hata miti mingine yote haina miujiza yoyote kiroho, kitu pekee ambacho kinaweza kutuletea miujiza chanya katika maisha yetu ni KUISHI MAISHA MAKAMILIFU na kitu pekee kinachoweza kutuharibia maisha yetu ya hapa na yajayo ni MAISHA YA DHAMBI..Na si miti wala kitu kingine chochote.

Hivyo kwa hitimisho, ni kuwa Mretemu ni mti wa kawaida, na hauna muujiza wowote kiroho.

Kama hujaokoka, kumbuka hizi ni siku za mwisho, na Yesu yupo mlangoni kurudi. Mwamini leo, akuoshe dhambi zako, na kukupa kipawa cha Roho wake Mtakatifu.

Maran atha!

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mwaloni ni nini? Na je unafunua nini rohoni?

Mti wa MLOZI alioonyeshwa nabii Yeremia 1:12 tafsiri yake ni nini?

Mti wa Mshita ni mti wa namna gani?

Uasherati wa Kiroho maana yake nini?

ALITOKA HUKO, AKAENDA MAHALI KARIBU NA JANGWA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/09/21/mretemu-ni-mti-gani/