Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake.

by Admin | 16 October 2022 08:46 pm10

Mithali 17:12 “Afadhali mtu akutwe na dubu aliyenyang’anywa watoto wake, Kuliko na mpumbavu katika upumbavu wake”.

Mpumbavu kibiblia ni mtu yeyote ambaye amekataa sheria ya Mungu na Maarifa. Yaani kwa ufupi mtu asiyetaka kumjua Mungu wake ni mpumbavu. Mtu wa namna hii hatabiriki, kwasababu shetani ndiye anayekuwa bwana na kiongozi wa Maisha yake, sio Yesu..

Kwamfano Mithali 10:23 inasema..

“Kwa mpumbavu kutenda maovu ni kama mchezo; Bali mtu mwenye ufahamu ana hekima”.

Sasa hapo biblia inaposema ni heri ukutane na dubu aliyenyang’wanya Watoto..inatupa picha jinsi gani mpumbavu alivyo hatari kuliko hata mnyama mkali dubu. Kwa kawaida dubu si mnyama mpole, na tena ukali wake unazidi pale anapokuwa na Watoto, lakini ukali huo unavuka mipaka pale anaponyang’anywa Watoto wake,Utakumbuka kile kisa cha Elisha kuwalaani wale vijana..biblia inasema arobaini na wawili kati yao waliraruliwa na dubu wawili tu jike.

Kutupa picha jinsi gani walivyohatari Wanyama hawa.. Lakini biblia inasema heri  ukutane nao kuliko mpumbavu. Mfano wa wapumbavu katika biblia ni Herode, ambaye kwa wivu wake aliwaua watoto wote, waliokuwa Yerusalemu kipindi cha kuzaliwa kwa Bwana Yesu, kama hiyo haitoshi alimuua na Yohana mbatizaji, Pamoja na Yakobo mtume wake Bwana.

Wapumbavu ndio wale wale waandishi na mafarisayo, ambao walikuwa wanazunguka huku na huko , na kuwafanya watu kuwa waongofu wapya wa dini zao, na mwisho kuwafanya  wana wa jehanamu mara mbili kuliko wao.(Mathayo 23:15).

Wapumbavu ndio manabii wa uongo walio sasa, ambao wanawatumainisha watu kuwa Mungu anawapenda wakiwa na mali au mafanikio, lakini hawakemei dhambi, na matokeo yake wengi wanakufa na kujikuta kuzimu, kwasababu walidanganywa na hila zao.

Vilevile Mpumbavu ndio mpinga-kristo atakaye kuja, ambaye ataundanganya ulimwengu mzima waipokee chapa yake, na hiyo itapelekea jopo kubwa sana la watu kufuatana naye kuzimu..Sasa biblia inasema ni heri ukutane na dubu aliyenyang’anywa Watoto wake, ambaye atakurarua tu mwili wako , baada ya hapo hawezi kukuathiri zaidi, lakini hawa, wanakurarua hadi na  roho yako, kwa kukupeleka kuzimu.

Ndio maana Bwana alisema tujiepushe naosana..

Mathayo 7:15 “Jihadharini na manabii wa uongo, watu wanaowajia wamevaa mavazi ya kondoo, walakini kwa ndani ni mbwa-mwitu wakali.

16 Mtawatambua kwa matunda yao. Je! Watu huchuma zabibu katika miiba, au tini katika mibaruti?

17 Vivyo hivyo kila mti mwema huzaa matunda mazuri; na mti mwovu huzaa matunda mabaya.

18 Mti mwema hauwezi kuzaa matunda mabaya, wala mti mwovu kuzaa matunda mazuri.

19 Kila mti usiozaa tunda zuri hukatwa ukatupwa motoni.

20 Ndiposa kwa matunda yao mtawatambua.

21 Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Soma NENO, dumu katika hilo, ndio salama yako nyakati hizi.. kwasababu tunaishi katika kipindi cha hatari sana. Ukiwa mvivu, utakwenda na maji yao.(Mathayo 24:24)

Bwana atusaidie..

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mpumbavu ni nani katika biblia? (Zaburi 14:1, Mithali 10:14)

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

NINI MAANA YA SISI KUWA WATOTO WA MUNGU?

MAISHA ULIYOPITIA NYUMA NI USHUHUDA TOSHA WA WEWE KUMTUMIKIA MUNGU.

Nini maana ya kilichotarajiwa kikikawia kuja moyo huugua (Mithali 13:12)?.

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/10/16/afadhali-mtu-akutwe-na-dubu-aliyenyanganywa-watoto-wake/