Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali ni chukizo kwa BWANA.

by Admin | 4 December 2022 08:46 pm12

SWALI: Nini maana ya huu mstari?

Mithali 20:10

[10]Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA.

JIBU: Ni mstari unaolenga ubadhilifu katika biashara au maisha…kwamfano labda mtu ni muuzaji wa mchele..na kwenye duka  lake anakuwa na mawe mawili ya mizani…moja la haki na lingine lenye uzito wa chini kidogo..hivyo akija mtu kumuuzia anampimia kwa lile jiwe la uzani wa chini, ili yeye abakiwe na kingi..

Au mwingine ni muuzaji wa mkaa, lile kopo la kipimo analibonda bonda ili lisichukue mkaa mwingi…sasa haya yote ni machukizo kwa Bwana..ndio hapo maandiko yanasema.. “Vipimo mbalimbali, na pishi mbalimbali, Vyote viwili ni chukizo kwa BWANA”.

Udanganyifu katika biashara ni tatizo sugu, na lipo katika nyanja mbalimbali pia kwamfano …utakuta mtu anauza maziwa ya ng’ombe, sasa ili apate faida kubwa zaidi anatia maji ili yawe mengi, kisha anauza…hayo ni machukizo..

Mwingine ni mama ntilie, ananunua sahani ndogo, au vikombe vidogo ili auze chai kidogo kwa bei ileile ya sikuzote apate faida kubwa.

Vilevile kuonyesha upendeleo kwa wengine ni machukizo kwa Mungu, kwasababu hivyo navyo ni vipimo mbalimbali. Labda ni muhuguzi, ambaye anawaongoza watu katika foleni ya kumwona daktari, anapokuja mtu wake wa karibu au mwenye pesa, anampitisha mlango wa nyuma, hamweki kwenye foleni.

Hivyo Bwana anatutaka tuwe watu wa usawa na wa haki. Kwasababu na yeye pia ni Mungu wa haki

shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Majina mbalimbali ya Mungu na maana zake.

VIPIMO MBALIMBALI VYA KIBIBLIA.

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Tofauti kati ya kuhukumu na kulaumu ni ipi?

Kuhimidi ni nini?(Zaburi 31:21)

JINSI EDENI ILIVYOKUWA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/12/04/vipimo-mbalimbali-na-pishi-mbalimbali-ni-chukizo-kwa-bwana/