PASAKA NI NINI? NA JE TUNARUHUSIWA KUSHEHEREKEA?

by Admin | 31 March 2020 08:46 pm03

Pasaka ni nini kibiblia?, na je tunaruhusiwa kusheherekea pasaka sisi wakristo kama wayahudi?

Pasaka ni neno la Kiswahili ambalo limetokana na neno la kigiriki “pascha” ambalo tafsiri yake kwa lugha ya kiingereza ni “passover” kwa Kiswahili  ni “pita juu”. Hivyo pasaka kwa Kiswahili tunaweza kusema tafsiri yake ni “pita juu au vuka upite”.

Asili ya Neno hili ni siku ile wana wa Israeli walipokuwa wanatolewa kutoka Misri, usiku ule ambao ndio walikuwa wanatoka Misri, Bwana Mungu aliwaagiza wasitoke nyumba zao kwamba mpaka watakapomchinja yule Mwanakondoo na damu yake kuipaka katika miimo miwili ya Milango…ili wakati yule malaika ambaye alitumwa kuwaangamiza wazaliwa wa kwanza wote wa wanadamu na wanyama waliokuwepo katika Misri nzima..atakapopita katika kila nyuma na kuiona damu hiyo ya mwanakondoo kwenye miimo ya mlango basi hataingia katika nyumba hiyo kumharibu mzaliwa wa kwanza wa nyumba hiyo “ATAVUKA JUU, AU ATAPITA JUU” Kuendelea na nyumba nyingine…na atakapofika katika nyumba nyingine na kukuta damu juu ya miimo ya mlango kama nyumba ya kwanza vile vile ATAPITA JUU na kuendelea mpaka atakapokuta nyumba ambazo hazina damu hiyo, ndipo ataingia na kuangamiza.

Kutoka 12:12 “Maana nitapita kati ya nchi ya Misri usiku huo, nami nitawapiga wazaliwa wa kwanza wote katika nchi ya Misri, wa mwanadamu na wa mnyama; nami nitafanya hukumu juu ya miungu yote ya Misri; Mimi ndimi Bwana.

13 Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, NITAPITA JUU YENU, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu, nitakapoipiga nchi ya Misri”.

Hivyo hicho kitendo cha kuvuka na KUPITA JUU ndicho kinachoitwa Passover, kwa kigiriki Pascha, kwa Kiswahili PASAKA.

pasaka ni nini

Sasa katika Agano jipya damu ya mwanakondoo yule ndio inayofanananishwa na damu ya Bwana wetu Yesu Kristo, Sisi tuliokuwa dhambini tulipotolewa dhambini(yaani Misri yetu) na tunapoelekea nchi yetu ya ahadi mbinguni…Damu ya Yesu ndiyo iliyotuokoa la laana ya Mungu dhidi ya watu wote walio katika dhambi..Na damu ya Yesu ni ishara ya Agano kwamba kwa kupitia damu yake tunalindwa na hukumu ya Mungu..Hukumu ya Mungu inapoachiliwa au itakapoachiliwa tutakuwa tumefunikwa chini ya damu ya Yesu na Malaika yule wa hukumu ATAPITA JUU YETU, na tutanusurika na hukumu ya Mungu.

Swali ni Je tunaruhusiwa kusheherekea pasaka kama watu wengine?

Tafsiri ya kusheherekea kibiblia ni tofauti na tafsiri ya kusheherekea kama inavyotafsiriwa na ulimwengu. Tafsiri ya sherehe kwa ulimwengu ni kula, na kunywa na kulewa, na kwenda kujiburudisha, kujifurahisha, kufanya uasherati, kujisisimua na kufanya anasa na kufanya kila aina ya mambo ya kimwili.

Lakini kibiblia tafsiri ya kusheherekea sio hiyo…Hata wayahudi wahakushehereka Pasaka kwa hivyo…Kibiblia, kusheherekea ni kujiweka katika ibada, na ibada sio kwenda kanisani tu..bali kujinyenyekeza na kujishusha chini ya uwepo wa Mungu, kwa kuomba, kusali, na kuzidi kujitakasa mbele zake huku tukikumbuka kuwa kwa tukio kama hili lililowahi kutokea miaka mingi iliyopita Bwana alitupa wokovu kwa kupitia damu yake pale Kalvari. Hivyo ni wakati wa kumwekea Bwana nadhiri,  wakati wa kuishiriki meza ya Bwana katika vigezo vya kimaandiko, ni wakati wa kusamehe Zaidi (sio kwamba sasa hatupaswi kusamehe mpaka siku ya pasaka ifike, hapana! tunasamehe kila siku, siku hiyo ikifika ni kumalizia tu kuvisafisha vile vidogo ambavyo tulikuwa hatujavimalizia), kwasababu utakatifu sio tu siku ya pasaka hapana bali kila siku!, siku hiyo ni kumalizia tu kuvisafisha vile vichache ambavyo vilikuwa vimesalia. Hivyo hiyo ndiyo tafsiri ya sherehe. Tukisheherekea kwa namna hiyo kuna amani fulani na furaha ya ajabu ambayo Mungu anaimimina ndani yetu..

Lakini tukishehereka kidunia kwamba ndio siku ya kutafuta kwenda disko, ndio siku ya kwenda kulewa, ndio siku ya kuvaa nguo za nusu-uchi na kutembea nazo barabarani, kwamba ndio siku ya kwenda kwenye dansi,  n.k..Tutakuwa tumejitafutia laana badala ya Baraka..Tutakuwa tumeshirikiana na shetani asilimia mia kuudhihaki na kuuzalilisha msalaba wa Kristo, na damu yake ya thamani. Hivyo tutakuwa tumejiharibia wenyewe. Lakini tukishehereka kibiblia tutapata baraka.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

(Pasaka ni nini)

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo

Je! kuna sikukuu za pasaka mbili? (Hesabu 9:11)

Easter ni nini?..Na je tunaruhusiwa kuisheherekea?

Ijumaa kuu ni nini? Na kwanini iitwe kuu?

KWA MIOYO YAO WAKAREJEA MISRI.

Je! Karamu za ‘Idi’ ndio zipo hizo tunazozisoma katika Hosea (12:9)

Ni muda gani Bwana Yesu alisulibiwa. Je! Ni saa 3 au saa 6?

HAPANA MFUPA WAKE UTAKAOVUNJWA.

JE! UTATOA HESABU YA NINI KATIKA SIKU ILE?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/03/31/pasaka-ni-nini-na-je-tunaruhusiwa-kusheherekea-pasaka/