Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.

by Admin | 10 June 2020 08:46 am06

SWALI: Huu mstari una maana gani? Mhubiri 3:16-17 “Zaidi ya hayo,nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu.17 Nikasema moyoni mwangu,Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki, kwa kuwa kuna wakati huko kwa kila kusudi na kwa kila kazi”.


JIBU: Hizi ni hekima zilizoandikwa na mfalme Sulemani ambae alimwomba Mungu ampe hekima badala ya Mali (Jambo la kwanza na la muhimu sana ambalo na sisi pia tunapaswa tuanze kumwomba Mungu)..

Hapo katika mstari huo anasema kwa hekima ya Roho “nikaona tena chini ya jua ya kwamba,Mahali pa hukumu upo uovu,Na mahali pa haki upo udhalimu”….Zingatia hapo anaanza na neno “NIKAONA CHINI YA JUA!”..Maana yake sio mbinguni, bali ni duniani. Ikiwa na maana kuwa mbinguni mahali pa haki hapana udhalimu, vilevile Hukumu za mbinguni Mungu alipo hazina uovu,

Ayubu 34:12 “Naam, hakika, Mungu hatatenda mabaya, Wala Mwenyezi hatapotosha hukumu”.

Lakini kinyume chake hukumu za duniani (chini ya jua) ndizo zenye uovu, na haki za duniani ndio zina udhalimu…Kama Mhubiri anavyosema hapo juu.

Na hiyo ni kweli kabisa..je! huoni leo, hata mahakamani (mahali ambapo pangepaswa kutolewa hukumu ya haki)..wapo mahakimu wanaopotosha hukumu?..wanaopokea rushwa na kumnyima haki yule anayestahili haki, na kumpatia yule asiyestahili?..na wapo wengi wanaopewa kesi ambazo sio zao kwasababu tu ya rushwa..n.k

Kwahiyo ni kweli kabisa chini ya jua na si mbinguni…hukumu nyingi zinapotoshwa!..Mahali ambapo ni pa hukumu kuna uovu na mahali pa haki kuna udhalimu…mahali ambapo mtu anapaswa apate haki, ananyimwa haki yake.

Na ndio maana katika mstari wa mwisho kabisa amesema.. “Mungu atawahukumu wenye haki na wasio haki”. Maana yake ni kwamba Wale wanaosimamia haki duniani kama mahakimu watasimama katika kiti cha hukumu pia kutoa hesabu ya uhakimu wao, kadhalika na wasio haki(maana yake waovu wote) pia watasimama mbele ya kiti cha hukumu) siku ile ya mwisho, na kila mtu atahukumiwa kulingana na matendo yake.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Maana ya ‘Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake’

Nini maana ya mstari huu: (Mtu ambarikiye mwenzake kwa sauti kuu asubuhi na mapema; Itahesabiwa kuwa ni laana kwake.Mithali 27:14 )?

Maana ya huu mstari ni ipi? Mithali 14:4 ‘Zizi ni safi ambapo hapana ngombe;bali nguvu za ngombe zaleta faida nyingi’.

JE KUPONYWA NI UTHIBITISHO WA MUNGU KUWA NA WEWE?

Wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu ni wakina nani?

BWANA AKAMWAMBIA SHETANI, BWANA NA AKUKEMEE EWE SHETANI;

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/06/10/mahali-pa-hukumu-upo-uovuna-mahali-pa-haki-upo-udhalimu/