MWANAMKE ULIYEKOMAA KI-UMRI, ITAMBUE HUDUMA YAKO.

by Admin | 10 July 2020 08:46 pm07

Ni kwanini wakati mwingine tunaona kama kuna mambo hayaendi sawa katika kanisa la Kristo, kwasababu tunafiri mambo yote yanatatuliwa na mchungaji, au mwalimu au mwinjilisti peke yake..

Kila kiungo katika mwili wa Kristo kinayo kazi yake, hivyo kimoja kisipowajibika ipasavyo ni lazima tu mapungufu yataonekana haijalishi vile vingine vitawajibika kiasi gani…

Leo hii utajiuliza ni kwanini wanawake wengi wanayo malezi mabaya ya watoto.. utakuta mwanamke anaye mtoto lakini hana heshima au maadili, au anaye mtoto lakini kichwani pamejaa miziki ya kidunia na wakati huo huo hajui hata mstari mmoja wa biblia..Unadhani hiyo inatokana na nini? Inatokana na mtu mmoja kushindwa kutimiza jukumu lake katika kanisa la Kristo.

Au utakuta mwanamke hamuheshimu mume wake, anajibizana naye kama mtoto, hajui kuwa ni agizo la Mungu kila mke amuheshimu mume wake, kama vile sisi tunavyomuheshimu Kristo na kila mume ampende mke wake, kama vile Kristo anavyotupenda sisi..Lakini yeye hilo si kitu kwake, anaona ni kawaida tu, na bado anafahamika kama mkristo, unadhani kilichomfanya awe na tabia hizo ni nini? ni kwasababu mtu Fulani hakutimiza jukumu lake katika kanisa, alimwachia mchungaji, au mtumishi Fulani afanye yeye kila kitu.

Au kwanini wanawake wengine, hawatulii katika shughuli zao, majumbani mwao, kinyume chake, ni kujizungusha mitaani, kutafuta habari za wengine, wanakosa staha, wanavaa mavazi yasiyo na heshima, nusu uchi wanakatiza barabarani, na bado ni waimba kwaya,…Unadhani hiyo inatokana na nini wakati mwingine? Ni kwasababu mtu Fulani hakutimiza jukumu lake katika mwili wa Kristo..

Paulo alimwandikia Timotheo maneno haya, akamwambia..

Tito 2:3 “Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wafundishao mema;

4 ILI WAWATIE WANAWAKE VIJANA AKILI, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao;

5 na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe”.

Unaona hapo biblia inaeleza wazi kabisa huduma ya mwanamke mzee ni ipi kanisani…Kumbuka mwanamke mzee sio lazima awe ni mzee kikongwe, lakini walau mwanamke ambaye ameshafikia umri wa makamo, ameshapitia mambo mengi hususani katika ndoa, anajua jinsi gani ya kuishi na mume katika Kristo..

Ikiwa wewe ni mmojawapo na upo katika kanisa, basi fahamu kuwa unalo jukumu zito la kuwasimamia ipasavyo wanawake vijana, ukijionyesha kwanza wewe mwenyewe kama kielelezo, kwa mwenendo wako wa utakatifu na tabia. Kisha ndio uwafundishe na kuwasimamia mabinti, na wanawake vijana jinsi ya kuishi kama mwanamke wa Kikristo..

Vinginevyo usipofanya hivyo, ujue kuwa jina la Mungu linatukanwa kwa ajili yako.

Hi ni huduma kubwa sana katika kanisa, lakini cha kushangaza ni kwamba mwanamke huyu huyu mzee na yeye anataka awe mchungaji kwasababu anaona huduma aliyopewa kama vile ni ndogo haijulikani.. Hafahamu kuwa hata katika kanisa wanawake huwa ndio wengi kuliko wanaume, hivyo kama huduma basi yeye ndio mwenye huduma kubwa ya kuwaangalia watu kuliko mwanaume, lakini hilo halitaki, anataka yeye naye asimame mimbarani, ahubiri kama askofu mkuu Fulani, au mwalimu Fulani au nabii fulani..Na matokeo yake ndio unakuta migogoro mingi ya kifamilia mara mwanaume huyu kagombana na mkewe kwasababu hamuheshimu mara Yule kapigwa na memewe n.k..mwisho wa siku jina la Mungu linatukanwa kwasababu tu kiungo Fulani kanisani kilishindwa kutimiza kusudi lake.

Ikiwa wewe ni mama, leo hii tambua jukumu lako. Na ufahamu kuwa Kristo anaiheshimu sana huduma yako kama tu anavyoliheshimu lile la mchungaji, na askofu…na kama utafanya vizuri ina thawabu kuliko hata hizo zinazoonekana ni kubwa kuliko nyingine.

Bwana akubariki.

Shalom

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

NAFASI YA MWANAMKE KATIKA KANISA

JE NI DHAMBI KUWA NA MAHUSIANO KABLA YA NDOA?

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

TUJIFUNZE JAMBO KWA WANAWAKE HAWA WAWILI:

USHAURI KWA MWANAMKE WA KIKRISTO.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/10/mwanamke-uliyekomaa-ki-umri-itambue-huduma-yako/