NENO LA MUNGU NI NINI?.

by Admin | 24 July 2020 08:46 pm07

Neno la Mungu ni nini?


Neno la Mungu ni ujumbe kutoka kwa Mungu, au mkusanyiko wa jumbe kutoka kwake. Ukisoma katika maandiko utaona mara nyingi manabii walikuwa wanasema maneno haya “Neno la Bwana linakanijia kusema”..Soma (Yeremia 1:11, Yeremia 13:3, 1Nyakati 22:8)

Wakiwa na maana ujumbe wa Mungu umenifikia kuwaambia. Hivyo biblia kwa ujumla inajulikana kama  Neno la Mungu.

Lakini pia Neno la Mungu ni jina la YESU KRISTO.

Ukisoma..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.

2 Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu.

3 Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika cho chote kilichofanyika.

4 Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima, nao ule uzima ulikuwa nuru ya watu….

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

Neno la Mungu ni nini?

Kwanini YESU aitwe Neno?

Anaitwa Neno Kwasababu yeye ndiye kinywa chote cha Mungu,(Yohana 8:38), Yeye ndio wazo lote la Mungu, yeye ndiye utimilifu wote wa Mungu kwa jinsi ya mwili (Wakolosai 2:9)..Yeye ndiye aliyepewa hukumu yote na Mungu, na yeye ndiye aliyepewa milki ya vitu vyote..

Hivyo chochote afanyacho, chochote asemacho, ni sauti ya Mungu kweli, na ujumbe wa Mungu kweli kweli kwetu..

Na ndio maana utamsoma katika Ufunuo akijitambulisha kwa jina hilo.

Ufunuo 19:12 “Na macho yake yalikuwa kama mwali wa moto, na juu ya kichwa chake vilemba vingi; naye ana jina lililoandikwa, asilolijua mtu ila yeye mwenyewe.

13 Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.

14 Na majeshi yaliyo mbinguni wakamfuata, wamepanda farasi weupe na kuvikwa kitani nzuri, nyeupe, safi”.

Hivyo ukiyashika maneno ya Yesu, basi umelishika Neno la Mungu, ukiyashika maagizo ya Yesu basi umeyashika maagizo yake…Naamini umeshafahamu sasa Neno la Mungu ni nini!

Bwana akubariki.

Je! Unatambua kuwa tunaishi katika siku za mwisho? Je! Una habari kuwa hili ndio kanisa la mwisho lijulikanalo kama Laodikia, na kwamba hatutakuwa na kanisa lingine zaidi ya hili,.Pengine kizazi chetu zitashuhudia tukio la ujio wa pili wa Kristo? Dalili zote zinaonyesha, Kama ni hivyo Je! Umejiwekaje tayari?..Bado upo kwenye dhambi?

Ikiwa utahitaji kumpa Yesu maisha yako leo basi uamuzi utakaoufanya ni wa busara sana, hivyo fungua hapa kwa ajili ya sala ya toba..>>>

Maran Atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia masomo haya kwa njia ya email yako au Whatsapp tutumie ujumbe kwenye box la maoni chini au piga namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

JINA LA MUNGU NI LIPI?

NITAFUNGUAJE MILANGO ILIYOFUNGWA MBELE YANGU?

USITOKE NJE YA HIFADHI YA MUNGU.

HUYU SI YULE SEREMALA, MWANA WA MARIAMU?

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/07/24/neno-la-mungu-ni-nini/