KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili.

by Admin | 6 August 2020 08:46 am08

Historia ya nyimbo KUMTEGEMEA MWOKOZI Lyrics/Swahili~ Tis So Sweet to Trust in Jesus.


Wimbo huu uliandikwa na mwanamke mkristo wa kiingereza aliyeitwa, Louisa M. Stead, Mnamo mwaka 1882, Ni wimbo unaoeleza furaha mtu anayoweza kuipata katika kumtegemea Kristo, Lakini nyuma ya uandishi wa wimbo huu, imelala historia nzito ya Maisha aliyopitia Louisa M stead,

Ilikiwa ni siku moja Louisa na mumewe Pamoja na mtoto wao wa kike aliyeitwa Lily, walipanga safari ya kwenda matembezi, wakiwa ufukweni mwa kisiwa kimoja ghafla walisikia  sauti kama ya mtu inapiga kilele za kuzama, kwenda kukimbia kuangalia wakamwona kijana mmoja, hilo lilimfanya mume wa Louisa, ajaribu kwenda kumwokoa, lakini katika jitihada zake za kufanya hivyo kwa bahati mbaya wote wawili wakazama, wakafa (kijana Pamoja na mume wake), mbele ya macho ya Louisa na binti yake.

Maisha yao baada ya hapo yalianza kuporomoka, Maisha yakawa magumu, Lakini wakagundua kuwa Mungu hakuwaacha katika hali zao, aliwatimizia mahitaji yao, hapo ndipo Louisa na binti yake walijifunza kumtegemea Mungu, na ndipo akauandika wimbo huu;

Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa;
Kukubali Neno lake,
Nina raha moyoni.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa,
Kuamini damu yake,
Nimeoshwa kamili.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Kumtegemea Mwokozi,
Kwangu tamu kabisa;
Kwake daima Napata,
Uzima na amani.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.
 
Nafurahi kwa sababu,
Nimekutegemea
Yesu,Mpendwa na Rafiki,
Uwe nami dawamu.
 
Yesu,Yesu namwamini,
Nimemwona thabiti;
Yesu,Yesu,yu thamani,
Ahadi zake kweli.

*****

Baadaye Louisa na binti yake wakasafiri kwenda Afrika kusini kwa kazi ya umishionari.

Lakini ni nini tunajifunza katika wimbo huu na uandishi wake?

Mimi na wewe tunaweza tukawa hatujapitia katika hali ngumu kama aliyopitia yeye, lakini yeye aliyeyapitia amemwona Mungu akimpigania, mpaka anaimba na kusema, “Nimemwona thabiti”..Hiyo ni kuonyesha kuwa hata wewe ukimwamini Yesu na kumtegemea, ..Utamwona thabiti/hakika akiwa na wewe katika maisha yako haijalishi leo unapitia mahali pagumu kiasi gani.

Imba wimbo huu ukikumbuka matendo yote makuu aliyokutendea nyuma. Na hakika utausikia uwepo wake nafsi mwako.

Bwana akubariki.

Tazama chini historia za nyimbo nyingine za Tenzi.

Tafadhali share na wengine.

Mada Nyinginezo:

NI SALAMA ROHONI MWANGU Lyrics

MWAMBA WENYE IMARA

USINIPITE MWOKOZI Lyrics

BWANA MUNGU NASHANGAA KABISA lyrics

CHA KUTUMAINI SINA lyrics

UWEPO WA BWANA HATA KATIKATI YA MATESO.

UNATAKA KUBARIKIWA? BASI USIKWEPE GHARAMA ZAKE.

NINI KINATOKEA BAADA YA KIFO?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/06/kumtegemea-mwokozi-lyrics-swahili/