Yakobo alikuwa na watoto wangapi?

by Admin | 12 August 2020 08:46 pm08

Yakobo alikuwa na watoto wangapi?


Yakobo, mjukuu wa Ibrahimu, alipewa neema na Mungu ya kuwa na Watoto 13, Kati ya hao 12 ni wa kiume na 1 wa kike aliyejulikana kama Dina.

Yakobo alikuwa na wake wawili, Na hao wake zake kila mmoja alikuwa na kijakazi wake mmoja, ambao baadaye walikuja kufanyikiwa kuwa masuria wa Yakobo.

Mke wa kwanza aliitwa Lea, Na mke wa pili aliitwa Raheli. Kijakazi wa Lea aliitwa  Zilpa Na kijakazi wa Raheli aliitwa, Bilha.

Wafuatano ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Lea.

  1. Rubeni
  2. Simeoni
  3. Lawi
  4. Yuda
  5. Isakari
  6. Zabuloni
  7. Dina(wa kike)

Wafuatao ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Raheli.

  1. Yusufu
  2. Benyamini

Wafuatao ni Watoto wa Yakobo waliozaliwa na Zilpa (Suria)

  1. Gadi
  2. Asheri

Wafuatao ni Watoto  waliozaliwa na Bilha (Suria)

  1. Dani
  2. Naftali

Habari yote ya uzao wao utaipata katika kitabu cha Mwanzo, kuanzia sura ya 29 na kuendelea.

Mwanzo 29:31 “Bwana akaona ya kwamba Lea hakupendwa, naye akafungua tumbo lake; bali Raheli alikuwa hazai.

32 Lea akapata mimba akazaa mwana, akampa jina lake, Reubeni, maana alisema, Kwa kuwa Bwana ameona teso langu; sasa mume wangu atanipenda.

33 Akapata mimba tena akazaa mwana, akasema, Kwa kuwa Bwana amesikia ya kwamba mimi sikupendwa, amenipa na huyu; akamwita jina lake Simeoni.

34 Akapata mimba tena, akazaa mwana, akasema, Basi wakati huu mume wangu ataungana nami, kwa sababu nimemzalia wana watatu. Kwa hiyo akamwita jina lake Lawi.

35 Akapata mimba tena, akazaa mwana. Akasema, Mara hii nitamsifu Bwana; kwa hiyo akamwita jina lake Yuda; akaacha kuzaa…………..”

Bwana akubariki.

Angalia Habari za watakatifu wengine wa kale chini.

Pia kama utapenda mafundisho ya biblia yawe yanakufikia kila mara kwa njia ya whatsapp basi utatumie ujumbe kwa namba hii : +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Nuhu alikuwa na watoto wangapi?

Israeli ipo bara gani?

Mariamu Magdalene ni nani. Na hilo jina amelitolea wapi?

Bwana aliposema kuwa yeye ni “Mungu wa miungu” alikuwa na maana gani?..je! yeye ni Mungu wa sanamu?

VIFO VYA MITUME WA YESU/ JINSI MITUME WALIVYOKUFA.

Nimrodi ni nani?

Yeshuruni ni nani katika biblia?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/12/yakobo-alikuwa-na-watoto-wangapi/