Baradhuli/Mabaradhuli ni nini au ni nani kwenye biblia?

by Admin | 13 September 2020 08:46 pm09

Baradhuli ni nani/ ni nini kama lilivyotumika kwenye biblia?


Kibiblia Baradhuli ni mtu asiyefaa, mpumbavu sana, aliyevuka mipaka

Ipo mistari kadha wa kadha inayoeleza tabia za watu wabaradhuli. Kwa mfano:

  1. Watu wanaoabudu miungu mingine kwa makusudi mbali na Mungu wa Israeli, muumba wa mbingu na nchi, hao ni mabaradhuli kibiblia.

Wanaokwenda kwa waganga wa kienyeji angali wanajua kabisa wanachokifanya ni kinyuma na mapenzi ya Mungu, wanaofanya uchawi, wanaofanya matambiko n.k. Hao ni mabaradhuli kibiblia.

Kumbukumbuku 13:12 Ukisikia yasemwa habari ya miji yako mmojawapo, akupayo Bwana, Mungu wako, ukae humo, ukiambiwa,

13 Kumetoka katikati yako MABARADHULI kadha wa kadha, wamewapotoa wenyeji wa mji wao, wakisema, Twendeni tukaabudu miungu mingine msiyoijua;

14 ndipo nawe uulize na kutafuta, ukiuliza kwa bidii; nawe angalia, ikiwa kweli, na jambo lile halina shaka, kwamba machukizo mfano wa haya yafanyika katikati yako;

15 hakika yako uwapige wenyeji wa mji ule kwa makali ya upanga, kwa kuwaangamiza kabisa, pamoja na vitu vyote vilivyomo, na wanyama walio humo, kwa makali ya upanga.

  1. Mabaradhuli pia ni watu wanaomwaga damu isiyo na hatia.

Ukisoma kitabu cha Waamuzi utaona Gideoni alikuwa na watoto sabini na wawili, lakini baada ya Gideoni kufa, mtoto wake mmoja aliingiwa na tamaa kutawala sehemu ya Gideoni hivyo akaamua kuwaua ndugu zake wote waliosalia ili yeye afanywe muamuzi badala yake, Ndipo biblia inatuambia alikwenda kuwaajiri watu Mabaradhuli ili kutekeleza adhma yake hiyo ya uuaji,..Hao watu wakashirikiana naye kuwaua ndugu zake wote siku moja juu ya jiwe. (Waamuzi 9:1-5).

  1. Mabaradhuli ni watu wanaofanya vitendo vya ubakaji na ulawiti.

Ukisoma tena kitabu cha Waamuzi 19  utamwona Yule mlawi ambaye alikuwa na suria wake, aliyekwenda kufanya ukahaba, kitendo ambacho kilimpelekea amrudishe nyumbani kwa baba yake, hivyo akakaa kule kwa muda wa miezi 4, ndipo baadaye akaghahiri akaamua amfuate surua wake amrudishe kwake, sasa alipokuwa njiani mji mmoja wa ugenini, alikaribishwa na mzee mmoja wa mji ule. Lakini usiku mambo yalibadilika kwani wale watu wa mji ule wa Benyamini, waliizingira nyumba wakataka wapewe hao wageni walale nao..Kama tunavyoijua habari Yule mlawi akaona ni heri amtoe suria wake wamfanye waliyotaka kumfanya..Wakafanya hivyo mpaka asubuhi baadaye Yule Suria akafa..

Waamuzi 19:22 “Hapo walipokuwa wakifurahisha mioyo yao, tazama, watu wa mji huo, watu MABARADHULI wakaizingira hiyo nyumba pande zote, wakagonga mlango; wakasema na huyo mwenye nyumba, huyo mzee, na kumwambia, Mlete nje mtu yule aliyefika nyumbani kwako, ili tupate kumjua”.

Soma sura yote ya 19,20 na 21, upate picha kamili, na nini kiliendelea baada ya pale..

  1. Mabaradhuli pia ni watu waasi.

Watu wanaoshikamana na viongozi waasi, au waliokosa heshima katika jamii.

2Nyakati 13:7, Waamuzi 11:3.

Je mpaka sasa mabaradhuli wapo?

Unapaswa ujiulize je! tabia mojawapo ya hizo unazo?

Kumbuka kuwa waovu wote, sehemu yao ni katika lile ziwa la moto. Ikiwa wewe ni muuaji, wewe ni baradhuli, ikiwa wewe ni mchawi(unakwenda kwa waganga) wewe ni baradhuli, n.k.

Ufunuo 21:8 “Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili”.

Lakini tumaini lipo kwa Yesu tu peke yake. Yeye peke yake ndiye anayeweza kuyageuza maisha yako na kukusaheme kabisa kabisa. Na kukufanya kuwa mwana wake.

Je! unahitaji kuokoka leo?

Unahitaji Yesu ayabadilishe maisha yako leo?

Unahitaji kupokea Roho Mtakatifu?

Biblia inasema..

Isaya 1:18 “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

19 Kama mkikubali na kutii mtakula mema ya nchi”;

Kama ndivyo basi fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Bwana akubariki.

Mada Nyinginezo:

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

Arabuni maana yake ni nini?

LAKINI USIKU WA MANANE, PAKAWA NA KELELE.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

MKUMBUKE MKE WA LUTU.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/09/13/baradhuli-mabaradhuli-ni-nini-au-ni-nani-kwenye-biblia/