Kuchelea ni nini?(2Wakorintho 11:3)

by Admin | 12 October 2020 08:46 pm10

Nini maana ya neno kuchelea kama tunavyolisoma katika biblia?


Kuchelea ni hofu au wasiwasi, husanani ule unaotokana na kuzuka kwa madhara Fulani.

Kwa mfano tusome mstari huu;

2Wakorintho 11:2 Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi.

3 Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikira zenu, mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo.

Hapo ni Paulo anaonyesha wasiwasi wake, kwa kanisa la Kristo kudanganywa na ibilisi haraka, na kuuacha unyofu wa moyo. Na ndio maana ukiendelea kusoma mistari inayofuata utaona Paulo, akiwatahadharisha, wasipokee injili nyingine, au Yesu mwingine au roho mwingine ambao wao hawakumuhubiri kwao..Ili wawe salama na uongo wa ibilisi.

2Wakorintho 12:20 “Maana nachelea, nisije nikawakuta si kama vile nitakavyo kuwakuta, nikaonekana kwenu si kama vile mtakavyo; nisije nikakuta labda fitina na wivu, na ghadhabu, na ugomvi, na masingizio, na manong’onezo, na majivuno, na ghasia”;

Vifungu vingine vinavyozungumzia Neno hili, ni kama vifuatavyo;

Matendo 23:9 “Pakawa na makelele mengi. Waandishi wengine wa upande wa Mafarisayo wakasimama, wakateta, wakisema, Hatuoni uovu wo wote katika mtu huyu; bali ikiwa roho au malaika amesema naye, ni nini?

10 Ugomvi mkubwa ulipotokea, yule jemadari akachelea Paulo asije akararuliwa nao, akaamuru askari washuke na kumwondoa kwa nguvu mikononi mwao, na kumleta ndani ya ngome”.

(Hapo ni jemedari alikuwa anaonyesha hofu yake ya kuuliwa kwa Paulo katikati ya baraza lile)

Soma tena;

Matendo 27:29 “Wakachelea tusije tukapwelewa mahali penye miamba, wakatupa nanga nne za tezi, wakaomba kuche”.

Soma pia Wagalatia 4:11.

Bwana akubariki.

Tazama pia maana ya maneno mengine chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

Kutahayari ni nini katika biblia?(2Timotheo 2:15)

Mlima Gerizimu na Ebali ni ipi, na umuhimu wao rohoni ni upi?

Amin, nawaambia, Kizazi hiki hakitapita, hata hayo yote yatakapotimia..!!

Daawa ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Mavyaa ni nani kibiblia?(Mika 7:6)

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/10/12/kuchelea-ni-nini2wakorintho-113/