Nini maana ya neno ‘Kuabiri’ kama linavyotumika katika  biblia?

by Admin | 26 December 2020 08:46 am12

Kuabiri maana yake ni kupanga safari, husasani ile ya majini, Neno hilo ndilo lililozaa neno abiria, ikiwa na maana  wale wanaosafiri.

Utalisoma sana sana katika zile ziara za mtume Paulo, na ile safari yake ya kuelekea Rumi kama mfungwa.

Vifuatavyo ni vifungu ambavyo utakutana na neno hilo.

Matendo 20:13 “Lakini sisi tukatangulia kwenda merikebuni,TUKAABIRI kwenda Aso, tukikusudia kumpakia Paulo huko; kwa maana ndivyo alivyoagiza, yeye mwenyewe aliazimu kwenda kwa miguu”.

Hapo mtume Paulo anamaanisha walipotangulia kwenda merikebuni walipanga safari ya majini ya kwenda Aso.

Matendo 21:1 “Ikawa tulipokwisha kujitenga nao na KUABIRI, tukafika Kosi kwa tanga moja, na siku ya pili yake tukafika Rodo na kutoka huko tukafika Patara”,

Hapo Paulo anamaanisha , walipokwisha kujitenga nao wakapanga safari majini ya kuelekea Kosi.

Vifungu vingine ni hivi;

Matendo 27:1 “Basi ilipoamriwa TUABIRI hata Italia, wakamtia Paulo na wafungwa wengine katika mikono ya akida mmoja, jina lake Yulio, wa kikosi cha Augusto.

2 Tukapanda katika merikebu ya Adramitio iliyokuwa tayari kusafiri mpaka miji ya pwani za Asia, tukatweka; Aristarko, Mmakedonia wa Thesalonike, akiwa pamoja nasi”.

Matendo 28:10 “nao wakatuheshimu kwa heshima nyingi; BASI TULIPOABIRI wakatupakilia vitu vile tulivyokuwa na haja navyo.

11 Baada ya miezi mitatu tukasafiri katika merikebu ya Iskanderia iliyokuwa imekaa pale kisiwani wakati wa baridi; na alama yake ni Ndugu Pacha”.

Shalom.

Tazama maana ya maneno mengine ya biblia chini.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Mtu mwenye “kitango” ni mtu wa namna gani kibiblia?

Mruba ni mdudu gani kwenye biblia?(Mithali 30:15)

Pambaja ni nini katika Biblia kama tunavyosoma katika kitabu cha Wimbo ulio bora 1:2?

“Shinikizo” ni nini kibiblia, Na maana yake rohoni ni ipi?

Shekina ni nini? Na Je! Utukufu wa shekina unamaana gani?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/12/26/nini-maana-ya-neno-kuabiri-kama-linavyotumika-katika-biblia/