Tarishi au Matarishi ni akina nani  kwenye biblia?

by Admin | 14 January 2021 08:46 pm01

Tarishi ni mtu aliyeajiriwa kwa kazi ya kusafirisha na kuwasilisha barua au nyaraka mahali pengine. Katika biblia watu ambao walikuwa wanatumwa kusambaza barua za wafalme kwa watu wa mji, au viongozi  waliitwa Matarishi.

Kwa mfano katika habari hii, utaona enzi zile za wafalme kulikuwa na  Mfalme aliyeitwa Hezekia ambaye alikusudia kurejesha tena sikukuu zilikuwa zimesahauliwa katika Israeli kwa miaka mingi, Hivyo ili adhma yake iweze kufanikiwa  ilimbidi awaandae hawa wajumbe (matarishi) ili wamsaidie kulipeleka hili agizo lake kwa watu wote waliokuwa Israeli wapande Yerusalemu kwenda kumfanyia Mungu sikukuu ya pasaka..

2Nyakati 30:5 “Basi wakafanya amri kupiga mbiu kati ya Israeli yote, toka Beer-sheba mpaka Dani, ya kwamba watu waje wamfanyie pasaka Bwana, Mungu wa Israeli, huko Yerusalemu; maana tangu siku nyingi hawakuifanya kama vile ilivyoandikwa.

6 Wakaenda MATARISHI wenye nyaraka za mfalme na wakuu wake, kati ya Israeli yote na Yuda, na kwa amri ya mfalme, kusema, Enyi wana wa Israeli, mrudieni Bwana, Mungu wa Ibrahimu, na Isaka, na Israeli, apate kuwarudia waliosalia wenu waliookoka mikononi mwa wafalme wa Ashuru”.

Utaona tena, kipindi kile, cha Mfalme Ahasuero, Amri ilipotolewa na Mfalme kuwa wayahudi wote wanapaswa wauliwe ndani ya siku moja, utaona agizo hilo lilisambazwa katika miji yote kwa mikono ya  hawa matarishi.

Esta 3:13 “BARUA ZIKAPELEKWA KWA MIKONO YA MATARISHI mpaka majimbo yote ya mfalme kuwaangamiza Wayahudi wote, na kuwaua, na kuwafisha, vijana kwa wazee, watoto wachanga na wanawake pia, siku moja, yaani, siku ya kumi na tatu ya mwezi wa kumi na mbili ndio mwezi wa Adari; na kuyachukua mali yao kuwa nyara”.

Neno hilo utalisoma pia katika vifungu hivi..

Esta 8:10 “Akaandika kwa jina la mfalme Ahasuero, na kutia muhuri kwa pete ya mfalme, akazipeleka barua kwa MATARISHI, wamepanda farasi, wamepanda wanyama wepesi sana waliotumika kwa huduma ya mfalme, ndio waliozalishwa katika zizi la mfalme”.

Ayubu 9:25 “Basi siku zangu zina mbio kuliko TARISHI; Zakimbia, wala hazioni mema”.

Yeremia 51:31 “TARISHI mmoja atapiga mbio kumlaki mwingine, Na mjumbe mmoja atapiga mbio kumlaki mwenziwe, Ili kumpasha habari mfalme wa Babeli, Ya kuwa mji wake umetwaliwa kila upande”.

Soma pia 2Nyakati 30:10, Esta 8:14

Lakini swali la kujiuliza na sisi je  ni matarishi wa habari gani? Je Ni habari za Kristo, au habari za watu mitaani?. Sote tunawajibu wa kuwa matarishi wa Kristo, tuwe wepesi kwenda kuwahubiria wengine habari njema za msalaba, ili waokolewe, kuliko habari nyingine zozote. Bwana anatazamia, vinywa vyetu, mikono yetu, maisha yetu,  vyote vitumike katika kuutangaza ufalme.

Je, mimi na wewe tunafanya hivyo?. Majibu tunayo mioyoni mwetu,

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Pomboo ni nini katika biblia?(Kutoka 25:5, Ezekieli 16:10)

Mharabu ni nani katika biblia?

Matuoni ni nini katika biblia?

USIPIGE MATEKE MCHOKOO!

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/01/14/tarishi-au-matarishi-ni-akina-nani-kwenye-biblia/