Matuoni ni nini katika biblia?

Matuoni ni nini katika biblia?

Matuoni limetokana na neno “kituo”. Hivyo popote lilipoonekana katika biblia lilimaanisha kituo, au vituo au kambi. Na matuo hayo au kambi hizo zinaweza kuwa ni kambi za kazi, au za vita, au za makazi au za shughuli nyingine yoyote maalumu.

Kwamfano tunaweza kuona sehemu chache neno hilo lilipoonekana katika biblia..

2Wafalme 3: 24 “Hata walipokuja matuoni kwa Israeli, Waisraeli wakainuka wakawapiga Wamoabi, hata wakakimbia mbele yao; wakaendelea wakiwapiga-piga Wamoabi hata kwao”.

Hapo neno hilo limetumika kama “kambi ya vita”.. hivyo ni sawa na kusema “Hata walipokuja kambini mwa Israeli, Waisraeli wakainuka wakawapiga Wamoabi, hata wakakimbia mbele yao”

Pia tunaweza kulisoma katika..

2Nyakati 32:21 “Naye Bwana akatuma malaika aliyewakatia mbali mashujaa wote, na majemadari, na maakida,MATUONI mwa mfalme wa Ashuru. Basi akarudia nchi yake mwenye haya ya uso. Naye alipoingia nyumbani mwa mungu wake, wale waliotoka viunoni mwake mwenyewe wakamwangamiza humo kwa upanga”.

Mistari mingine yenye neno hilo ni Zaburi 106:16, 2 Nyakati 22:1, Amosi 4:10 na Zekaria 14:5.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

UFUNUO: Mlango wa 19

JINSI SHETANI ANAVYOZUIA MAJIBU YA MAOMBI YETU.

CHUKIZO LA UHARIBIFU

UMEPATA UHAKIKA WA KUTOKUINGIA HUKUMUNI KATIKA SIKU ILE?

Ni uthibitisho upi unaoonyesha kuwa kuna MBINGUNI na KUZIMU?

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments