Mharabu ni nani katika biblia?

Mharabu ni nani katika biblia?

Kuna tofauti kati ya “Mwarabu” na “Mharabu”. Maneno haya mawili yameonekana sehemu kadhaa katika biblia na yana maana mbili tofauti.

Tukianza na “Mwarabu”.

Mwarabu au kwa wingi waarabu; ni jamii ya watu wanaoishi maeneno ya mashariki ya kati. Yaani maeneno ya  Syria,Jordani, Palestina, Saudi Arabia, Yordani, Yemen, Kuwait,  Iran, Iraq, na Uturuki. Wenyeji wa maeneo hayo ndio wanaojulikana kama waaramu.. akiwa mmoja ni mwarabu, wakiwa wengi ni waarabu.

Katika biblia watu hao wametajwa sehemu kadhaa..

Yeremia 3: 2 “Inua macho yako, ukavitazame vilele vya milima, ukaone; pa wapi mahali ambapo hawakulala nawe? Kando ya njia umeketi ili kuwangojea, KAMA VILE MWARABU JANGWANI; nawe umeitia nchi unajisi kwa ukahaba wako na uovu wako”.

Na pia unaweza kusoma Isaya 13:20, utaona mwarabu akitajwa.

Lakini pia katika biblia kuna neno “MHARABU” , Neno hili au jina hili halihusiani na watu hao wenyeji wa mashariki ya kati, bali linamaanisha “Mharibuji”. Mtu anayetumwa kuharibu kwa kuua ni  Mharabu (Mithali 18:9), lakini pia Malaika wa Mungu anayetumwa kwa lengo la kuitimiza ghadhabu ya Mungu kwa kuua, naye pia anaitwa Mharabu.

Tunaweza kuona mfano mmoja katika biblia..

1Wakorintho 10:10 “Wala msinung’unike, kama wengine wao walivyonung’unika, wakaharibiwa na mharabu”.

Mharabu anayezungumziwa hapo, ni malaika yule aliyetumwa kuwaharibu na kuwaangamiza wana wa Israeli walipokuwa wananun’unikia Mungu jangwani..ambapo Bwana Mungu aliwaonya wana wa Israeli, waende katika njia zake ili wasiangamizwe na malaika huyo..

Kutoka 23: 20 “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.

21 Jitunzeni mbele yake, mwisikize sauti yake; wala msimtie kasirani; maana, hatawasamehe makosa yenu; kwa kuwa jina langu limo ndani yake”.

Na hata leo, Mharabu wa Mungu yupo, kwaajili ya kutulinda katika safari ya wokovu, lakini tukienda kinyume na mapenzi ya Mungu, yupo mbele yetu kutupinga kama alivyowapinga wana wa Israeli na kuwaua wengi na kama alivyompinga Balaamu katika Hesabu 22.

Bwana atujalie neema yake na kutulinda.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255693036618 au +255789001312


Mada Nyinginezo:

USITAFUTE KUKANWA NA BWANA SIKU ILE.

IFAHAMU HUZUNI NA FURAHA YA MALAIKA.

VITA VYA IMANI NI VITA ENDELEVU.

MAPIGO YA VITASA SABA, NA SIKU YA BWANA.

REKEBISHA YAFUATAYO ILI MAMBO YAENDE SAWA.

Rudi nyumbani

Print this post

About the author

Admin administrator

Subscribe
Notify of
guest
0 Comments
Inline Feedbacks
View all comments