Nini maana ya “Mwenye hekima huvuta roho za watu”

by Admin | 1 April 2021 08:46 am04

SWALI: Biblia ina maana gani inaposema “Mwenye hekima huvuta roho za watu”?


JIBU: Tusome.

Mthali 11:30 “Mazao ya mwenye haki ni mti wa uzima; Na mwenye hekima huvuta roho za watu”

Zipo hekima nyingi, lakini hekima inayozungumziwa katika biblia ni hekima ya rohoni, ambayo ndiyo kuu kuliko hekima zote, ndio hekima aliyonayo Mungu mwenyewe. Sasa hapo aliposema mwenye hekima huvuta roho za watu, anamaanisha kuwa yeye anayewavuta watu kwa Mungu au watu wamjue Mungu, huyo anatambulika kama mtu mwenye hekima sana.

Hekima hii ilianza kuonekana kwa Bwana wetu Yesu Kristo, Kama tunavyojua yeye aliacha enzi na nguvu na mamlaka huko mbinguni akashuka hapa duniani kwa lengo moja tu,  na kuturejeshea sisi ule uhusiano tuliokuwa tumeupoteza na Mungu, na ndio maana akawa radhi kuhubiri injili na kama hiyo haitoshi kuutoa uhai wake kwa ajili yetu.

Vivyo hivyo na sisi pia, tukisema tumeokoka, ni lazima tuwavute na wengine kwa Mungu, ili na wao pia waokoke kama sisi, Hapo ndipo tutatambulika na mbingu  kuwa tuna hekima, lakini kama hatuonyesha bidii ya namna hiyo, haijalishi tutasema sisi ni wa rohoni kiasi gani, bado tutakuwa hatuna hekima, kwa mujibu wa maandiko.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Jiunge na kundi letu la mafundisho ya Biblia whatsapp kwa kubofya hapa > Group-whatsapp

Mada Nyinginezo:

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/04/01/nini-maana-ya-mwenye-hekima-huvuta-roho-za-watu/