Shilo ni wapi?

by Admin | 22 October 2021 08:46 am10

Shilo ni nini?

Katika biblia Shilo ulikuwa mji mtakatifu, ambapo Kabla ya Mungu kupachagua Yerusalemu kama mji atakaoweka jina lake milele, hapo kabla wana wa Israeli walikuwa wanakusanyiko huko Shilo, kama sehemu takatifu ya kufanyia ibada na kutolea dhabihu.

Na hata sanduku la agano mara tu baada ya wana wa Israeli kuingia nchi ya ahadi, mji uliotueuliwa kwaajili ya kuliweka sanduku hilo la agano la Mungu..ulikuwa ndio huo wa mji wa Shilo, ambapo sanduku hilo lilikaa mjini huko bila kutoka kwa miaka mingi mpaka  Wafilisti walipokuja kulichukua kutoka huko sababu ya makosa ya wana wa Israeli (1Samweli 10-11).

Huko Shilo pia ndiko Nabii Samweli alikolelewa maisha yake yote (1Samweli 1:24 )

Mji huu wa Shilo ulikuwa unapatikana kaskazini mji mwa mji wa Betheli, karibu na Samaria.

Unaweza kusoma zaidi kuhusu mji huo kupitia mistari ifuatayo > Yoshua 18:8-10, Yoshua 19:51, Yoshua 21:2, Waamuzi 18:31, Waamuzi 21:19, 1Samweli 1:9, Zaburi 78:60.

Lakini swali ni je! Hii Shilo mpaka leo ni sehemu takatifu?.

Jibu ni la!

Shilo ya Leo sio tena huko Israeli, bali ni katika Neno la Mungu.

Katika Kweli ya Neno la Mungu na katika Roho Mtakatifu..tunamwabudu Baba..kama Bwana Yesu alivyosema..

Yohana 4:21

“Yesu akamwambia, Mama, unisadiki, saa inakuja ambayo hamtamwabudu Baba katika mlima huu, wala kule Yerusalemu.

22 Ninyi mnaabudu msichokijua; sisi tunaabudu tukijuacho; kwa kuwa wokovu watoka kwa Wayahudi.

23 Lakini saa inakuja, nayo sasa ipo, ambayo waabuduo halisi watamwabudu Baba katika roho na kweli. Kwa maana Baba awatafuta watu kama hao wamwabudu”

Je umempokea Roho Mtakatifu, je unaliishi Neno?.

Bwana akubariki.

Maran atha.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Nini maana ya Dirii, Chepeo na Utayari?

Raheli aliwalilia vipi watoto wake?

Nini maana ya “Ulipo mzoga, ndipo watakapokutanika tai?

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/10/22/shilo-ni-wapi/