Bwana Yesu alikuwa kabila gani?

by Admin | 8 November 2021 08:46 pm11

Je! Bwana Yesu alikuwa kabila gani, miongoni mwa kabila 12 za Israeli?.


Jinsi biblia inavyotafsiri makabila ni tofauti na ulimwengu sasa unavyotafsiri.

Kibiblia Kabila ni jamii ya watu wanaotoka katika mzizi wa familia moja, maana yake asili ya kizazi chao ni baba mmoja.

Kwamfano katika biblia tunaona Taifa moja la Israeli likiwa na kabila 12.

Lakini makabila hayo yote, asili yao ni mtu mmoja anayeitwa Yakobo, ambaye ndio lake Israeli. Huyu Israeli alioa wake wanne na kuzaa watoto 12.. hivyo majina ya hao watoto 12, ndio yakawa makabila 12.

Hivyo mwisraeli yoyote, ni lazima awe miongoni mwa hayo makabila 12.

Sasa tukirudi kwenye swali, Bwana Yesu alikuwa kabila gani?.

Jibu ni kwamba Bwana Yesu hakuwa miongoni mwa kabila za Israeli, kwasababu yeye hakuzaliwa na Baba wa kimwili.

Mimba aliyoipata Mariamu, ilikuwa ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu (Luka 1:35).

Hivyo Bwana hakuwa miongoni mwa kabila la Israeli, bali alikuwa ni uzao wa kimbinguni.

Lakini sasa, Yusufu ambaye ndiye aliyemposa Mariamu..(ambaye ndiye kama baba aliyekuwa mlezi wa Bwana Yesu katika utoto).

ndiye aliyekuwa wa kabila la YUDA. Hivyo kupitia yeye, ili ahadi ya Mungu ya kumketisha mmoja katika kiti chake cha enzi itimie..ndipo akampitisha Mfalme Yesu, katika mnyororo huo wa kabila hilo la Daudi, yaani Yuda.

Lakini Bwana yenyewe hakuwa wa kabila la Yuda.Bali kwasababu ya Yusufu, ndio akaitwa wa kabila la Yuda.

Ufunuo wa Yohana 5:5 “Na mmojawapo wa wale wazee akaniambia, Usilie; tazama, Simba aliye wa kabila ya Yuda, Shina la Daudi, yeye ameshinda apate kukifungua kile kitabu, na zile muhuri zake saba”.

Huyo ni Yesu, anayezungumziwa hapo?.

Swali ni je! Umemwamini na kumpokea maishani mwako?..kama bado unasubiri nini?..

Hakuna wokovu kwa mwingine yeyote, isipokuwa kwa Yesu, mwamini leo na kisha tubu dhambi zako zote kwake, na ukabatizwe katika ubatizo sahihi wa maji tele na kwa jina la Yesu, upate ondoleo la dhambi zako (Matendo 2:38).

Na Roho Mtakatifu atayabadilisha maisha yako, na kukuongoza.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

Kwanini Bwana Yesu alitokea katika ukoo wa Yuda?

FUNGUO WALIZOKUWA NAZO MABINTI WATANO WA SELOFEHADI!

Je ni kweli Yuda hakuwa na dhambi kwa kumsaliti Bwana, kwasababu tayari ilikuwa imeshatabiriwa?

Nini maana ya “Siku moja nyuani mwa Bwana ni bora kuliko siku elfu”?

 Je kualikwa kwenye sherehe za watu ambao si wakristo ni dhambi?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/11/08/bwana-yesu-alikuwa-kabila-gani/