Tirshatha ni nini? (Ezra 2:63)

by Admin | 14 August 2023 08:46 am08

Neno hili utalipata katika vifungu hivi kwenye biblia.

Ezra 2:63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.

Nehemia 8:9 Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha, na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, Siku hii ni takatifu kwa Bwana, Mungu wenu; msiomboleze wala msilie. Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati

Nehemia 10: 1 Basi hawa ndio waliotia muhuri; Nehemia, ndiye Tirshatha, mwana wa Hakalia, na Sedekia;

Soma pia Nehemia 7:65

Tirshatha ni neno la kiajemi, ambalo linamaanisha mtawala aliyeteuliwa kuongoza uyahudi chini ya ufalme wa uajemi. Kwa jina lingine ni gavana/ liwali, Katika vifungu hivyo vinamwonyesha Nehemia alikuwa kama Tirshatha/Mtawala. Soma pia (Nehemia 5:18).

Lakini pia Zerubabeli, alipewa nafasi hii kama tunavyosoma hapo kwenye Ezra 2:63, Hivyo wote hawa walisimama kama wakuu wa majimbo hayo wayaangalie, na kusimamia kazi zote walizoagizwa na mfalme.

Bwana akubariki.

Tazama pia maana ya maneno mengine ya kibiblia chini.

Je! Umeokoka? Je, unatambua kuwa Kristo anakaribia kurudi? Umejiandaaje? Tubu dhambi zako ukabatizwe upokee Roho Mtakatifu uwe salama zizini mwa Bwana. Muda ni mfupi sana tuliobakiwa nao, huu si wakati wa kubembelezewa wokovu, ni wewe mwenyewe kuona na kugeuka upesi. Ikiwa upo tayari kuyakabidhi maisha yako kwa Bwana basi fungua hapa ili upate mwongozo wa sala ya toba >>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Shalom.

Tafadhali shea na wengine ujumbe huu;

Pia Kwa maombezi/ Ushauri/ Maswali/ Whatsapp:
Tuandikie katika BOXI la Maoni hapo chini au
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

Mada Nyinginezo:

Maana Ya Maneno Katika Biblia.

Ayari ni nini kama tunavyosoma katika biblia?

Jabari ni nini, kama linavyotumika kwenye biblia?

Kisima cha joka na lango la jaa ni nini?(Nehemia 2:13)

HAPAKUWA NA NAFASI YA KUPITA KWA YULE MNYAMA ALIYEKUWA CHINI YANGU.

NI MAONO YAPI HAYO UNAYOSUBIRIA?

FUMBO ZA SHETANI.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2023/08/14/tirshatha-ni-nini/