BWANA, UNATUACHAJE?

BWANA, UNATUACHAJE?

Kuna  kauli ambayo tunayo sana kwenye vinywa vyetu…Hususani pale boss au kiongozi wetu anapomalizana nasi katika mpango fulani na kutuaga..tunasema “bwana unaniachaje”?

Maana yake, baada ya kukaa chini yake muda mrefu, au kumtumikia, kuna namna anapaswa akuandalie mazingira ya kukufanya uendeleze lile jambo lake, au lako mwenyewe.. ndio hapo utaona wanawaachia watumwa wao aidha viinua mgongo, mitaji, au fedha za matumizi. 

Hili linaonekana ni jambo zuri kufanywa na bwana au kiongozi yeyote mwenye busara. 

Lakini kwa Yesu mambo yalikuwa tofauti, kwenye kauli yake ya mwisho alipokuwa anapaa.. Mitume hawakuachwa na lolote, na zaidi wanaambiwa wakashuhudie habari zake kutoka pale Yerusalemu walipo, waende uyahudi, Samaria na mpaka mwisho wa nchi.

Ukitafakari kwa ukaribu jambo hilo linahitaji rasilimali nyingi za kifedha, kiuchumi n.k. lakini hawakuachiwa hata senti kumi.

Ukiwa na mawazo kuwa kiongozi wako wa kiroho akuandalie rasilimali za kujikimu kimaisha, ndio ukamtumikie Bwana vizuri, ndugu utavunjika moyo..kwasababu yeye mwenyewe alipoitwa hakuandaliwa rasilimali, Na hilo halikuanzia kwake, lilianzia kwa mitume, hadi kwa wote waliofuata baadaye yao. Tena ungekuwepo nyakati za mitume ungevunjika moyo mara kumi zaidi.

Kumbuka Yesu anaonekana kama  “Bwana mgumu” kwa baadhi ya watumwa. Usipokuwa makini unaweza kumwona pia hivyo.

Kivipi?

Mkumbuke yule aliyepewa talanta moja aliona ameachwa bila màandalizi mazuri kimtaji…akabakia tu kulalamika na kusema huyu Bwana wangu ni mgumu sana.… hii talanta moja aliyoniachia  nitafanyia nini, Hata chakula cha siku moja tu hainitoshi, Bado anataka nimletee vingi, anataka kuvuna asipopanda… Ninakwenda kumwekea pesa yake. Nikafanye mambo yangu akirudi nimpe sitaki lawama.

Hakujua uamuzi huyo ni kosa kubwa..

Luka 19:20-26

[20]Akaja mwingine akasema, Bwana, hili ndilo fungu lako, ambalo nililiweka akiba katika leso. 

[21]Kwa maana nilikuogopa kwa kuwa u mtu mgumu; waondoa usichoweka, wavuna usichopanda. 

[22]Akamwambia, Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe. Ulinijua kuwa ni mtu mgumu, niondoaye nisichoweka, na kuvuna nisichopanda; 

[23]basi, mbona hukuiweka fedha yangu kwa watoao riba, ili nijapo niipate pamoja na faida yake? 

[24]Akawaambia waliosimama karibu, Mnyang’anyeni hilo fungu, mkampe yule mwenye mafungu kumi. 

[25]Wakamwambia, Bwana, anayo mafungu kumi. 

[26]Nawaambia, Kila aliye na kitu atapewa, bali yule asiye na kitu atanyang’anywa hata alicho nacho. 

Ukiona unasubiri ufanyiwe na Yesu kwanza kitu fulani ndipo uwe na hamasa ya kuifanya kazi. 

Kuwa makini. ROHO MTAKATIFU TAYARI YUPO NDANI YAKO UMESHAPEWA. Hakuna kingine zaidi ya hiko.  Simama kwenye huduma yako, Timiza utume wako.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

About the author

Nuru ya Upendo administrator

Leave a Reply