FUNDISHO, NI KUSEMA NENO USILOLIJUA

Ubora wa Kuhubiri au kufundisha haupimwi kwa elimu kubwa ya biblia, au mifano mizuri, au utashi fulani wa kupangilia maneno. Hapana, bali ni uwezo wa kupenya katika mioyo ya watu.

Haimaanishi kuwa na elimu ya biblia haichangii ubora wa fundisho au hubiri..inachangia sana lakini hiyo ni kama gamba la juu sana..ambalo linaweza lisitoe pia matokeo yoyote.

Pale fundisho linapoweza kuingia ndani ya moyo wa mtu, kupambanua, kuchoma, kulainisha, kupindua-pindua, kukarabati, kuponya hadi kumfanya mtu kuwa na mwitikio wa dhahiri wa nje. Hilo ndio linaitwa fundisho au hubiri kibiblia.

Sasa tendo hilo mpaka kufikiwa, si jambo rahisi hata kidogo, hakuna utashi wa kibinadamu unaweza kufanya hivyo.

Kwasababu hakuna anayejua ndani ya mtu mwingine kuna nini?

Lakini lililo gumu zaidi ni kuwa hata yeye mwenyewe hajijui vema, kama anahitaji matengenezo katika eneo fulani la moyo wake. Anaweza akawa ana hofu akadhani huwenda chanzo cha hofu hiyo ni ule ugonjwa uliomshika, kumbe chanzo ni kingine kabisa.

Kwasababu mwanadamu mwenyewe moyo wake ni fumbo kubwa.

Yeremia 17:9

[9]Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Umeona jinsi ilivyo ngumu sana. Ikiwa yeye mwenyewe hajijui, wewe mtu wa tatu utayajulia wapi yaliyomo moyoni mwake? Lakini Mungu anataka uyahubiri yahusuyo moyo wake.

Usifikiri unapomwona mtu, labda ana huzuni, au furaha au ana tabia za ulevi, wizi, , ukadhani anahitaji fundisho linaloendana na hiyo tabia unayoiona kwa nje.

Unaweza ukakosa shabaha kwa maili nyingi sana, ukifikiri tu hivyo.

Utamwona analia, pengine ni mgonjwa, amefiwa, amepoteza kila kitu kama ilivyokuwa kwa Ayubu na wewe unamfuata na fundisho la faraja, ukadhani kuwa ndio uponyaji wake utakapotokea.

Kumbe Mungu anajua anataka makemeo, na makaripio ili aponywe.

Wakati mwingine utasimama kwenye mkusanyiko wa watu wengi labda mia. Huko huko wapo wanaohitaji faraja, wanaohitaji unabii, wanaohitaji maonyo, wanaohitaji maarifa, wanaohitaji kufunguliwa. Sasa wewe unasimama na fundisho lako lenye mlengo mmoja wa makemeo, unadhani wote watahudumiwa na hilo. Kama ukikosa namna ya ki-ungu, unaweza ukawa unazungumza maneno yako.

Na lengo la Mungu ni watu wote wahudumiwe na Neno.

Hapo ndio linakuja suala la hakuna mbobezi wa fundisho au hubiri. Inahitaji hekima nyingine itokayo juu, ya kuhubiri usichokuwa na ufahamu nacho, au ujuzi nacho.

Siku ile ya Pentekoste, kilichotendeka mpaka ikapelekea watu wale kuchomwa mioyo, na hatimaye kuamini kwa idadi ile kubwa ya watu.

Haikuwa kwasababu walipaza sauti sana, au walihubiri kwa ujasiri sana, au maneno yao yalikuwa na elimu kubwa ya theolojia..

Hapana angalia utaona yalikuwa ni maneno ya kawaida kabisa… lakini yaliyoundwa na Roho Mtakatifu kwa namna ambayo yalipenya katika moyo wa kila mmoja.

Utaona, hatua ya kwanza walinena kwa lugha ambazo hata wao wenyewe hawakuzijua, lugha hizo zilikuwa zinawahubiria wengine.. zinanena mambo yao ya sirini, zinawakemea, zinawafariji, zinawaponya, zinawashuhudia Kristo.

Mpaka baadaye wanamaliza kunena tayari injili imeshahubiriwa wasijue ni kitu gani kimehubiriwa.

Petro aliposimama kumalizia maneno yake, wote wamenywea wanasubiri tu kupewa maelekezo ni nini cha kufanya baada ya pale..

Matendo ya Mitume 2:37

[37]Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

Hao ni watu wasio na elimu yoyote, walikuwapo waandishi, na mafarisayo wenye elimu lakini hakuna matokeo yoyote ya mafundisho yao.

Hata leo hii mimi na wewe.. Tujue kuwa kuhubiri na kufundisha hakutegemei sana ujuzi, au utashi, bali kunategemea zaidi Roho Mtakatifu.

Kwanini Roho Mtakatifu?

Kwasababu yeye ndiye anayeweza kuzama ndani ya mioyo ya watu na kujua shida zao, na kuwaponya.

Ni nini tunapaswa kufanya, ili fundisho likazame moyoni, lisitoke kwa makisio yetu?

Jambo kuu ni Kuwa na maandalizi ya kutosha.

Maandalizi hayo yapo kwa namna mbili.

1) Kumwandalia Roho Mtakatifu njia ya kuanzia..Ndio hapo unahitaji kwanza kusoma na kuandaa somo / fundisho. Kumbuka Ni lazama utenge muda kuandaa fundisho ambalo utalihubiri. Andika, na ujue pa kuanzia, bila kuwa na maandalizi hayo, unasema nitaenda tu kuzungumza. Ujue tayari umeizuia njia ya Roho Mtakatifu kufundisha.

2) Lakini hilo peke yake halitoshi, hatua nyingine ni kuomba maingilio ya Roho Mtakatifu yawe makubwa. Hapo ndipo unatenga muda mrefu wa kuomba, ili Roho Mtakatifu akatembee kwenye vyumba vya ndani kabisa ambavyo wewe hujui, wakati utakaposimama na kufundisha, kushuhudia.

Sasa ukimaliza hapo. Jiandae kwenda kusema ulichokusudia.. kumbuka mhubiri anayetumia dakika kumi kufundisha lakini amekuwa na maandalizi ya masaa matano kwenye kusoma na maombi. Ana nguvu zaidi ya yule atakayefundisha masaa matano, halafu alijiandaa kwa dakika tano.

Mwisho Ukienda kufundisha na kuona mazungumzo yako yanasogea nje ya mada, au taarifa nyingine zinakuja kichwani mwako tofauti na zile ulizoziandika kwenye daftari ujue ni kazi za Roho Mtakatifu usizizuie.

Baadaye utakuja kusikia tu shuhuda, na hata kama hazitasemwa, ujue Neno lako halijakwenda bure.

Tukiwa wahubiri na waalimu wa namna hii. Roho nyingi za watu zitaokolewa.

Kuhubiri ni kusema tusichokijua, cha wengine.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 2 (AMRI YA UPENDO)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari hizi tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

PENDO LA MUNGU.

Bwana YESU alitufundisha kuwa Amri ya kwanza ni “Kumpenda Bwana na ya pili ni kuwapenda majirani kama nafsi zetu”.

Mathayo 22:36 “Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?

37 Akamwambia, MPENDE BWANA MUNGU WAKO KWA MOYO WAKO WOTE, NA KWA ROHO YAKO YOTE, NA KWA AKILI ZAKO ZOTE.

38 Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.

39 Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, MPENDE JIRANI YAKO KAMA NAFSI YAKO.

40 Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii”.

Na tena alisema…

Yohana 14:21 Yeye aliye na amri zangu, na kuzishika, yeye ndiye anipendaye; naye anipendaye atapendwa na Baba yangu; nami nitampenda na kujidhihirisha kwake.

 

   1. OMBA ONGEZEKO LA UPENDO WA MUNGU NDANI YAKO (Tumia dakika 30)

i. Kwa moyo wako wote.

  • Hapa utaomba Bwana akujalie kumtafuta kwa hiari bila shuruti, kwasababu hiyo ndio maana ya kumpenda kwa moyo wako wote.

     ii. Kwa roho yako yote

– Hapa utamwomba Bwana kuwa upendo wako ukatoke rohoni, katika kumtafuta kwasababu Neno linasema waabudua watamwabudu baba katika roho na kweli.

               iii.    Kwa akili zako zote.

                           – Hapa utaomba Bwana akuwezeshe kumtumikia yeye kwa ujuzi aliokupa, (ule wa asili na ule wa kujifunza) kama ni msomi basi kupitia elimu yako hiyo umtumikie MUNGU, na kuyafanya mapenzi yake.

          iv. Kwa Nguvu zako zote.

      – Nguvu zinaweza kuwa za mwili kama wewe ni kijana, lakini pia zinaweza kuwa za kifedha, katika maeneo hayo yote mwombe BWANA akusaidie uweze kumpenda MUNGU na kufanya mapenzi yake, Utoe muda wako au mali zako katika kumtumikia MUNGU.

            2. OMBA UPENDO KWA JIRANI. (Tumia dakika 30)

Neno la MUNGU linatufundisha kuwa “Tujaponena kwa lugha zote na kufanya ishara zote kama hatuna Upendo sisi sio kitu”

      1Wakorintho 13:1 “Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao”.

Na tena inasema…

Waebrania 13:1 “Upendano wa ndugu na udumu”.

    i. Omba Upendo kwa ndugu wa kiroho (Wachungaji na washirika wenzako)

  • Hapa utaomba Bwana akakukumbushe mema waliyokutendea.
  • Utaomba Bwana akuondolee chuki na kutokusamehe.
  • Utaomba Bwana akuoneshe kasoro zako ili pendo kati yako na wapendwa wenzako lidumu.
  • UOmbea kanisa na wakristo wenzako wakajawe na Upendo wa kiMungu.
  • Omba Bwana akaachie roho ya kusameheana.

     ii.   Omba Upendo kwa ndugu wa kimwili (Wana familia)

  • Hapa mwombe Bwana akuongezee upendo kwa wazazi, na ndugu wengine wadogo kwa wakubwa.
  • Waombee wana familia yako wajawe na upendo kama wewe unavyojiombea..

        3. KEMEA KILA ROHO INAYOJIINUA KUPOOZA UPENDO WA MUNGU, NA WA KINDUGU

Kemea kwa jina la YESU KRISTO kila pando la chuki kanisani kwako, katikati yako na wakristo wenzako, katikati yenu kama familia.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 1 (MAPENZI YA  MUNGU)

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

MAPENZI YA MUNGU.

Bwana YESU alisema si kila aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika ufalme, bali yule afanyaye mapenzi ya Baba wa mbinguni.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa basi kama kigezo cha kuingia mbinguni ni “KUFANYA MAPENZI YA MUNGU”, hivyo tukimwomba MUNGU atusaidie kuyajua na kuyafanya mapenzi yake tutakuwa tunaomba jambo sahihi kabisa.

      1. OMBA KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Tumia dakika 30)

Katika Eneo la kiroho.

  • Hapa utaomba Bwana akufunulie uyajue mapenzi yake katika kazi yake ya huduma, na wapi unapaswa utumike na utumikeje, pia kama bado haujaifahamu karama yako, mwombe Bwana akufunulie.

Katika Eneo la kimaisha.

  • Hapa utamwomba Bwana akufunulie kuyajua mapenzi yake katika kazi unazozifanya au elimu, ni kipi sahihi unapaswa ukifanye ukiwa hapo kazini, ni watu gani sahihi unapaswa ushirikiane nao ili usifanye kinyume jambo nje na mapenzi ya MUNGU pia kama unatafuta kazi, basi omba MUNGU akakufunulie kazi sahihi na kukuongoza hapo.

Katika Eneo la kifamilia.

  • Hapa omba Bwana akakuoneshe mapenzi yake kuishi na mke, mume, na watoto, au wazazi pia ombea wanafamilia yako wote wakayajue mapenzi ya MUNGU na kuyafanya.

 

  2. OMBA KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU. (Tumia dakika 30)

Utauliza katika kuyatenda mapenzi ya MUNGU kuna haja ya kuomba?. Jibu ni Ndio! Kwasababu pasipo yeye kutusaidia sisi hatuwezi kufanya lolote. (Soma Yohana 15:5).

Katika Eneo la kifikra

  • Hapa utaomba Bwana akakusaidie fikra zako, Bwana akakupe uwezo wa kufikiri yanayompendeza yeye kila wakati akilini mwako (Waefeso 5:10).

Katika eneo la Viungo

  • Hapa mwombe Bwana akusaidie viungo vyako kama mikono, miguu, macho, masikio viwe vyepesi katika kufanya mapenzi ya MUNGU, baada ya kuyajua mapenzi ya MUNGU, ikiwa na maana kwamba miguu yako iwe tayari kukimbilia kuyafanya mapenzi ya MUNGU, mikono yako iwe tayari na mwepesi kufanya mapenzi ya MUNGU, macho yako yawe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU.

 

     3. KEMEA KILA ROHO INAYOKUZUIA WEWE KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Zipo roho za adui zinazozua kuyafanya mapenzi ya MUNGU, roho hizi zinazuia fikra zako za ndani zisifikiri, wala kupenda kuyafanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kushuhudia habari za wokovu, ndani ya fikra zako woga unaingia au aibu au kukosa ujasiri, tumia muda kuzikemea.

Pia zinazuia viungo vyako visiwe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kuhubiri au kwenda kufanya kazi yoyote iliyo halali na ghafla udhaifu wa mwili utaingia kama uchovu, uvivu, au ugonjwa. Hivyo chukua muda kukemea roho hizo na Bwana atakufungua.

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.

Bwana akubariki usikose sehemu ya Pili ya Mwongozo huu wa Neno na Maombi, kwa msaada zaidi wasiliana nasi kwa namba tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

NENO NA MAOMBI~ Sehemu ya 1 (MAPENZI YA  MUNGU)

 

Jina la Bwana YESU libarikiwe, karibu katika kujifunza Neno na Maombi. Kusoma Neno bila Maombi, au kuomba bila Neno ni sawa na kitamba cha bendera kisicho na mlingoti, kupitia mfululizo huu wa tafakari tutapata mwongozo sahihi wa kuomba kupitia maandiko ya kwenye Biblia.

MAPENZI YA MUNGU.

Bwana YESU alisema si kila aniambiaye Bwana Bwana atakayeingia katika ufalme, bali yule afanyaye mapenzi ya Baba wa mbinguni.

Mathayo 7:21 “Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.

22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi?

23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu”.

Sasa basi kama kigezo cha kuingia mbinguni ni “KUFANYA MAPENZI YA MUNGU”, hivyo tukimwomba MUNGU atusaidie kuyajua na kuyafanya mapenzi yake tutakuwa tunaomba jambo sahihi kabisa.

  1. OMBA KUYAJUA MAPENZI YA MUNGU KWAKO (Tumia dakika 30)

 

  1. Katika Eneo la kiroho.
  • Hapa utaomba Bwana akufunulie uyajue mapenzi yake katika kazi yake ya huduma, na wapi unapaswa utumike na utumikeje, pia kama bado haujaifahamu karama yako, mwombe Bwana akufunulie.
  1. Katika Eneo la kimaisha.

– Hapa utamwomba Bwana akufunulie kuyajua mapenzi yake katika kazi unazozifanya au elimu, ni kipi sahihi unapaswa ukifanye ukiwa hapo kazini, ni watu gani sahihi unapaswa ushirikiane nao ili usifanye kinyume jambo nje na mapenzi ya MUNGU pia kama unatafuta kazi, basi omba MUNGU akakufunulie kazi sahihi na kukuongoza hapo.

               iii.        Katika eneo la kifamilia.

                           – Hapa omba Bwana akakuoneshe mapenzi yake kuishi na mke, mume, na watoto, au wazazi pia ombea wanafamilia yako wote wakayajue mapenzi ya MUNGU na kuyafanya.

 

  1. OMBA KUYATENDA MAPENZI YA MUNGU. (Tumia dakika 30)

Utauliza katika kuyatenda mapenzi ya MUNGU kuna haja ya kuomba?. Jibu ni Ndio! Kwasababu pasipo yeye kutusaidia sisi hatuwezi kufanya lolote. (Soma Yohana 15:5).

  1. Katika Eneo la kifikra
  • Hapa utaomba Bwana akakusaidie fikra zako, Bwana akakupe uwezo wa kufikiri yanayompendeza yeye kila wakati akilini mwako (Waefeso 5:10).

 

  1. Katika eneo la Viungo
  • Hapa mwombe Bwana akusaidie viungo vyako kama mikono, miguu, macho, masikio viwe vyepesi katika kufanya mapenzi ya MUNGU, baada ya kuyajua mapenzi ya MUNGU, ikiwa na maana kwamba miguu yako iwe tayari kukimbilia kuyafanya mapenzi ya MUNGU, mikono yako iwe tayari na mwepesi kufanya mapenzi ya MUNGU, macho yako yawe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU.

 

  1. KEMEA KILA ROHO INAYOKUZUIA WEWE KUYAFANYA MAPENZI YA MUNGU.

Zipo roho za adui zinazozua kuyafanya mapenzi ya MUNGU, roho hizi zinazuia fikra zako za ndani zisifikiri, wala kupenda kuyafanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kushuhudia habari za wokovu, ndani ya fikra zako woga unaingia au aibu au kukosa ujasiri, tumia muda kuzikemea.

 

Pia zinazuia viungo vyako visiwe tayari kufanya mapenzi ya MUNGU, ndio hapo utatamani kwenda kuhubiri au kwenda kufanya kazi yoyote iliyo halali na ghafla udhaifu wa mwili utaingia kama uchovu, uvivu, au ugonjwa. Hivyo chukua muda kukemea roho hizo na Bwana atakufungua.

 

1Petro 4:2 “Tangu sasa msiendelee kuishi katika tamaa za wanadamu, bali katika mapenzi ya Mungu, wakati wenu uliobaki wa kukaa hapa duniani.

3 Maana wakati wa maisha yetu uliopita watosha kwa kutenda mapenzi ya Mataifa; kuenenda katika ufisadi, na tamaa, na ulevi, na karamu za ulafi, na vileo, na ibada ya sanamu isiyo halali;

4 mambo ambayo wao huona kuwa ni ajabu ya ninyi kutokwenda mbio pamoja nao katika ufisadi ule ule usio na kiasi, wakiwatukana”.

 

Bwana akubariki usikose sehemu ya Pili ya Mwongozo huu wa Neno na Maombi, kwa msaada zaidi wasiliana nasi kwa namba tajwa hapa chini.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

ITAFAKARI SANA MAUTI YA BWANA.

 
Je unajua Mauti inaweza kuzaa uzima?.
Unajiuliza “mauti inawezaje kuzaa uzima, na ili hali yenyewe haina uzima”.
 
Jibu ni ndio inawezekana kabisa kwani Mauti ya Bwana YESU ilizaa uzima.
 
Tofauti na inavyotafsiriwa na baadhi kuwa kifo cha Bwana YESU kilikuwa ni “msiba” , lakini ukweli ni kwamba kufa kwa Bwana YESU hakukuwa msiba wala simanzi kwetu na wala Bwana YESU, hajawahi kuitwa marehemu wala hayati.
 
Bali kifo chake kilikuwa ni shangwe na mpango kamili wa MUNGU, katika hatua za kumkomboa mwanadamu aliye dhambini.
 
Kivipi?
 
Unakumbuka kifo cha Elisha kilivyoleta uzima kwa yule mmoabi aliyekufa?…
 
Tusome…
 
2 Wafalme 13:20 “Elisha akafa, nao wakamzika. Basi vikosi vya Wamoabi wakaingia katika nchi mwanzo wa mwaka.
 
21 Ikawa, walipokuwa wakimzika mtu, angalia, waliona kikosi; wakamtupa yule mtu kaburini mwa Elisha; mara yule maiti alipoigusa mifupa ya Elisha, alifufuka, akasimama kwa miguu”
 
Umewahi kujiuliza inawezekanikaje maiti kuifufua maiti yenzake?.Lakini jambo hilo liliwezekana kwa mifupa ya Elisha. (Mauti ilizaa uzima).
 
Sasa kama kupitia Mauti ya nabii Elisha Mungu alishawahi kutenda muujiza mkubwa kiasi kile wa kufufua maiti vipi Mauti ya Bwana YESU?.
 
Ni wazi kuwa Mauti ya Bwana ina muujiza mkubwa kuliko huo wa Elisha, kwani Elisha alimfufua mmoja tu, bali Bwana YESU atawafufua maelfu watakaomwamini.
 
Je unataka kufufuliwa baada ya kifo?
Kama unatamani kutokea na kuishi tena baada ya maisha haya kupita, chagua leo njia njia ya uzima ya kumwamini Bwana YESU na kutubu dhambi kwa kumaanisha kuacha kabisa makosa.
 
Kumbukumbu la Torati 30:15 “Angalia, nimekuwekea leo mbele yako uzima na mema, na mauti na mabaya”.
 
Hakuna “shortcut” ya kwenda kumwona MUNGU, njia ni moja tu iliyonyooka na ni nyembamba, nayo ni YESU KRISTO.
 
Mathayo 16:24 “Wakati huo Yesu aliwaambia wanafunzi wake, Mtu ye yote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe, ajitwike msalaba wake, anifuate.
 
25 Kwa kuwa mtu atakaye kuiokoa nafsi yake, ataipoteza; na mtu atakayepoteza nafsi yake kwa ajili yangu, ataiona.
 
26 Kwani atafaidiwa nini mtu akiupata ulimwengu wote, na kupata hasara ya nafsi yake? Au mtu atatoa nini badala ya nafsi yake? 
 
27 Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba yake pamoja na malaika zake; ndipo atakapomlipa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake” .
 
Kama bado haujampokea YESU (haujaokoka), wasiliana nasi kupitia namba tajwa hapo chini, tutakupa mwongozo utakaokufaa, lakini kama tayari umeshampa YESU maisha yako, basi nakuombea uendelee mbele kwa bidii na Roho Mtakatifu akuongezee Neema.
 
Shalom.
 
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWANAMKE ALIYEONGOZWA NYIKANI.

Ulishawahi kutafakari kwanini yule mwanamke aliyemzaa yule mtoto wa kiume, kupewa uwezo wa kukimbilia nyikani, kama njia ya kuepushwa na joka lile?

Kwanini asichuliwe mashambani, au mjini, au milimani, kinyume chake iwe nyikani.

Ufunuo 12:13-14

[13]Na joka yule alipoona ya kuwa ametupwa katika nchi, alimwudhi mwanamke yule aliyemzaa mtoto mwanamume.

[14]Mwanamke yule akapewa mabawa mawili ya tai yule mkubwa, ili aruke, aende zake nyikani hata mahali pake, hapo alishwapo kwa wakati na nyakati na nusu ya wakati, mbali na nyoka huyo.

Nyikani ni mahali ambapo hapana uzuri wowote, hapana mahitaji yoyote ya msingi, mahali pasipovutia, kwasasa tunaweza kusema ni nyakati za ukame, ambazo huoni, jambo lolote, huoni hatua yoyote dhahiri,ijapokuwa unajitahidi sana..huoni mafanikio yoyote, huoni mazingira rafiki..

Wakati mwingine ni kipindi cha kupungukiwa kwa muda mrefu, upo pale pale.

Tunapofikia hatua hii, mara nyingi tunamlilia Mungu atuondoe huko, tunahuzunika, tunanyong’onyea, tunasinyaa kiroho, tunamlilia Mungu kwa juhudi nyingi atuvushe..

Ni kweli kabisa jangwa si zuri, lakini wakati mwingine Bwana hulitumia kutuepusha na yule mwovu. Njia pekee iliyompasa huyu mwanamke kuepushwa na joka lile, ilikuwa ni kukimbilia jangwani, na si vinginevyo.

Hivyo ujikutapo katika nyakati mbalimbali ngumu, maadamu upo ndani ya Kristo na unaendelea vema katika imani, fahamu pia huko ulipo Mungu anakuandaa na unatimiza kusudi la Mungu.

Tuwapo katika mazingira yoyote, suluhisho si kulalamika bali ni kuomba, kushukuru na kuitafuta hekima.

Bwana akubariki.

Shalom

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

KIJAKAZI ALIYEJUA UPONYAJI ULIPO.

Hauhitaji nafasi kubwa kuzijua siri za Mungu.

Naamani alikuwa ni mtu mkuu, jemedari wa vita, lakini alikaa na ukoma uliomtesa kwa muda mrefu, bila ufumbuzi wowote wala tumaini lolote la kupona.

Katika ushujaa wake, na cheo chake hakuwahi kujua siri za uponyaji zipo wapi, isipokuwa kijakazi wake ambaye hajatajwa hata jina lake, aliuona uzima wa Bwana wake, mahali ulipo, mbali sana na taifa lake, kwa mtu wa Mungu aliyeitwa Elisha.

Kijakazi huyu ndiye aliyefungua njia ya Naamani  kupokea uponyaji wake mkamilifu

2 Wafalme 5:1-4

[1]Basi Naamani, jemadari wa jeshi la mfalme wa Shamu, alikuwa mtu mkubwa mbele ya bwana wake, na mwenye kuheshimiwa, kwa sababu kwa mkono wake BWANA alikuwa amewapa Washami kushinda; tena alikuwa mtu hodari wa vita; lakini alikuwa mwenye ukoma. 

[2]Na Washami walikuwa wametoka vikosi, wakachukua mfungwa mmoja kijana mwanamke kutoka nchi ya Israeli; naye akamhudumia mkewe Naamani. 

[3]Akamwambia bibi yake, Laiti bwana wangu angekuwa pamoja na yule nabii aliyeko Samaria! Maana angemponya ukoma wake. 

[4]Mtu mmoja akaingia, akamwambia bwana wake, akasema, Yule kijana mwanamke aliyetoka nchi ya Israeli asema hivi na hivi. 

Huhitaji kuwa mtu fulani, wala huhitaji kuwa hodari duniani, kuwa msomi sana, jasiri sana, kuzidhihirisha nguvu za Mungu, au kuwahudumia watu wake, au kuwaponya na kuwafundisha,  unahitaji tu, unyenyekevu ambao unadhihirishwa kwa kumcha Bwana. Kisha yeye mwenyewe Mungu kwa hekima yake ataitengeneza njia yake anayoijua mwenyewe kuwasaidia wengine kupitia wewe.

Ndio maana Neno la Mungu linasema;

1 Wakorintho 1:26-29

[26]Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa; 

[27]bali Mungu aliyachagua mambo mapumbavu ya dunia awaaibishe wenye hekima; tena Mungu alivichagua vitu dhaifu vya dunia ili aviaibishe vyenye nguvu; 

[28]tena Mungu alivichagua vitu vinyonge vya dunia na vilivyodharauliwa, naam, vitu ambavyo haviko, ili avibatilishe vile vilivyoko; 

[29]mwenye mwili awaye yote asije akajisifu mbele za Mungu. 

Wekeza zaidi kwenye kumcha Mungu, zaidi ya juhudi za kibinadamu kwasababu hekima yake ni mbali sana na mavumbuzi ya wanadamu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

NJAA KUU IKAINGIA KATIKA ILE NCHI.

Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze Biblia.
Je unaikumbuka ile habari ya mwana mpotevu?..
Luka 15:13 “Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
14 Alipokuwa amekwisha tumia vyote, NJAA KUU ILIINGIA NCHI ILE, YEYE NAYE AKAANZA KUHITAJI.
15 Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe”.
16 Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, WALA HAPANA MTU ALIYEMPA KITU”.
Kilichomfanya huyu kijana “ateseke sana” wala si kwasababu ya “kutumia vyote alivyokuwa navyo”..kwasababu hata baada ya kiutumia vyote alikuwa na matumaini kwamba mambo yangeweza kuwa vizuri hata kwa kufanya kazi ya kuajiriwa na kupata chochote kitu.
Lakini kilichomtesa sana hata kufikia hatua ya kuzingatia kurudi kwa baba ni “njaa kuu iliyoingia katika ile nchi”.
Maana yake ni kwamba ile nchi labda mvua ilikata, kukawa hakuna chakula cha kutosha au labda mji ulizungukwa pande zote kama kipindi kile cha njaa ya Samaria.
2 Wafalme 6:25 “Njaa ikawa kuu huko Samaria; na tazama, wakauhusuru, hata kichwa cha punda kikapata kuuzwa kwa vipande themanini vya fedha, na kibaba cha mavi ya njiwa kwa vipande vitano vya fedha”.
Hii njaa ya Samaria ilisababisha Mavi (kinyesi) cha njiwa kuuzwa kwa fedha nyingi sana..
Nashawishika kuamini kuwa kijana yule aliyetamani kula maganda ya nguruwe, alikuwa kwenye nchi yenye njaa inayoikaribia hiyo nchi ya Samaria.
Sasa kikawaida njaa ikashaingia kwenye nchi hata fedha inakuwa haina thamani tena, ni tabu kuu.
Ndivyo ilivyo kwa watu wenye kukimbia mbali na hifadhi ya MUNGU, wenye kuukimbilia ulimwengu na kumwacha Baba wa mbinguni wakiamini kuwa ulimwenguni kuna raha.
Pasipo kujua kuwa matatizo yatakuwa katika mahali wanapokaa, au katika vitu wanavyovitegemea.
Utajitumainia leo na kazi yako, lakini utafika wakati njaa kuu itaingia katika hilo shirika, katika hiyo taasisi, katika hilo kampuni utafanya nini?.
Unawategemea wanadamu na moyoni umemwacha Bwana, utafika wakati njaa kuu itaingia katikati ya hao watu unaowategemea.
Utafika wakati shida kuu zitaingia hapo shuleni unapopatumainia, hapo chuoni au taasisini ulipo, njaa itakayofanya fedha isiwe na thamani hata kama unayo tele.
Utafika wakati njaa kuu itaingia katika nchi ambapo hata fedha yako haitakuwa na thamani.
Leo hii jifunze kwa mwana huyu aliyepotea ambaye mwishoni alizingatia kurudi kwa baba yake.
Luka 15:17 “Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa.
18 Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako;
19 sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako.
20 Akaondoka, akaenda kwa babaye. Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana”.
Zingatia leo hii kurudi kwa Baba yako wa mbinguni, kabla ya njaa kuu kuingia mahali ulipo au katika kile unachokitegemea.
Na unarudi kwa baba kwa njia ya kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO.
Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

YAFAHAMU NA YATENDE MAPENZI YA MUNGU.

NAMNA GANI NITAPOKEA NGUVU ZA BWANA YESU?.

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

HEKIMA YA KIMUNGU, INAINGIAJE MIOYONI MWETU?

NINI TUNAJIFUNZA KWA MWANA MPOTEVU NA NDUGUYE?

ACHA UASHERATI.

 Dhambi pekee inayotajwa kwenye Biblia yenye laana ya umaskini na  inayofilisi  ni “Uasherati”.

Luka 15:13 “Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; AKATAPANYA MALI ZAKE HUKO KWA MAISHA YA UASHERATI”.

Ukitaka kufilisika kuwa mwasherati… kila utakachokipata kitapukutika na hutajua kimeishaje.

Labda unawaza kwamba mali zitaisha tu kwa “kuonga” (kwa kuwapa makahaba). Ndio hiyo namna ya kwanza ya kufilisika, Lakini nataka nikuambie hata usipoonga pesa yoyote, ukawa unafanya uasherati bila kugharimika….nataka nikuambie kuwa bado tu utaanguka kiuchumi, utaombea na kila aina ya watumishi na kutoa kila aina ya sadaka na hautafunguliwa.

Kwasababu uasherati “unaondoa akili”

Mithali 6:32 “Mtu aziniye na mwanamke hana akili kabisa; Afanya jambo litakalomwangamiza nafsi yake”.

Uasherati unaondoa akili ya “maendeleo”…kwahiyo hata pasipo kuonga mwanamke bado tu utafilisika, ndio maana hata wanawake wanaofanya uasherati maisha yao yanafanana tu na wanaume waasherati, wote wanasumbuka, kwasababu hata pesa wanazopewa na wanaume hazijawahi kuwasiadia chochote kwasababu tayari kile kitendo kimewatolea akili.

Haujawahi kusikia popote kahaba kapata pesa za kutosha sasa ameacha kazi hiyo na kupitia mtaji wa ukahaba wake sasa anajishughulisha na jambo jingine, wote utaona hata wapate fedha nyingi bado watarudi katika hiyo kazi.

Dhambi ya uasherati inatajwa kama ubaya mkubwa..

Mwanzo 39:9 “Hakuna mkuu katika nyumba hii kuliko mimi, wala hakunizuilia kitu cho chote ila wewe, kwa kuwa wewe u mkewe. Nifanyeje ubaya huu mkubwa nikamkose Mungu?”.

Ndugu ukitaka kufunguliwa kimaisha acha uasherati kabisa, jitenge na huyo binti unayemwita “girl friend”..kama unataka kuishi naye funga naye ndoa takatifu na halali inayojulikana na sio ufanye uasherati.

Binti, achana na huyo kijana unayemwita “boyfriend”..ukitaka kuishi naye funga naye ndoa halali ya kibiblia, lakini maisha ya uasherati unayoendelea nayo yanakuondolea akili za asili na zile zile za neema.

Matokeo ya mwisho ya  uasherati ni hukumu ya MUNGU.

1 Wakorintho 6:9 “Au hamjui ya kuwa wadhalimu hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike; WAASHERATI HAWATAURITHI UFALME WA MUNGU, wala waabudu sanamu, wala wazinzi, wala wafiraji, wala walawiti”.

Hii ndio hasara kubwa inayotokana na uasherati, (kuukosa uzima wa milele).

Ni heri ukose mali zote za duniani kuliko uukose uzima wa milele, kwani dunia inaita na mambo yake yote.

Lakini pamoja na hayo, kwanini uteseke duniani na bado uteseke baada ya kifo?.

Amua leo kumpa YESU KRISTO maisha yako, akusafishe dhambi zako na kukutakasa.

Huo uasherati ambao unaona ni mgumu kuuacha, ni kwasababu haujaokoka sawasawa, wewe fanya maamuzi thabiti ya kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, na ondoa vichocheo vyote vya uasherati katika maisha yako kama mavazi ya kizinzi ( ya kubana maungo, na mitindo yote ya kidunia).

Pia jitenge na makundi ya watu wenye mizaha, na acha mahusiano hayo yasiyo rasmi, futa namba zote za watu unaozungumza nao mambo ya kihuni, na kiri mbele yao kwamba umeokoka, uone kama Roho Mtakatifu hatakutengeneza, na uasherati wote utakufa ndani yako itabaki historia tu.

Lakini ukitubu na kuendelea kuishi maisha yale yale ya siku zote, nakuambia hitaona matokeo yoyote zaidi sana ndio utazama zaidi katika dhambi.

Ikiwa utahitaji kuokoka utaweza kuwasiliana nasi kwa namba zilizopo hapa chini na utasaidika kwa Neema ya MUNGU.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255789001312 au +255693036618

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Nini maana ya kutokuwa chini ya sheria?

Swali: Biblia inasema “Tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria”(Wagalatia 5:18) maana yake nini andiko hili?


Jibu: Tuanzie ule mstari wa 16 ili tuelewe vizuri..

Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

17 Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

18 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria”.

Awali ya yote ni vizuri kujua roho inayozungumziwa hapo ni roho gani?.. si roho ya mtu, bali roho ya MUNGU (Yaani Roho mtakatifu) ndio maana imeanza kwa herufu kubwa… maana yake “Tukiongozwa na Roho Mtakatifu hatupo chini ya sheria”

 Sasa anaposema “tukiongozwa na Roho hatupo chini ya sheria” haimaanishi kuwa tunapookoka basi tuna ruhusa ya kufanya kila kitu, au kutenda jambo lolote, au kuvaa vyovyote au kuishi vyovyote, na kwamba tupo juu ya sheria.

La! Hiyo sio tafsiri yake.. ili tuelewe vizuri maana au tafsiri halisi ya andiko hilo, hebu takafakari mfano huu.

Mwalimu wa Hisabati anawaambia wanafunzi wake kuwa “Mkitumia kikokoteo (yaani calculator) hamtateseka na kanuni/sheria za mahesabu”.. maana yake ni kwamba mtafanya mahesabu yale yale lakini katika urahisi, lakini si kukwepa mahesabu… ikiwa na maana kuwa ile calculator inarahisisha kufanya mahesabu bila mwanafunzi kutumia kanuni.

Ni ivyo hivyo katika hilo andiko anaposema “Mkiongozwa na Roho hampo chini ya sheria”… maana yake sheria za kumcha MUNGU ambazo kwa udhaifu wa mwili ni ngumu, kama vile zile sheria za hisabati, kwa kupitia Roho Mtakatifu zinakuwa nyepesi.

Maana yake kama Biblia imesema “Usizini” au “Usiseme uongo”… kutimiza sheria hiyo ya kukaa bila kudanganya au bila kufanya zinaa ya nje au moyoni ni ngumu.. lakini kwa msaada wa Roho Mtakatifu inawezekana kutimiza sheria hiyo kirahisi,

Ndio maana hapo kwenye mstari wa 16 anasema “Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.

Na hapa ndipo tunapoona umuhimu mkubwa wa kujazwa Roho Mtakatifu kama Biblia inavyotufundisha..

Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho”.

Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli hawaoni shida kuishi maisha matakatifu yasiyo na dhambi, wengine wote wanaweza kuwashangaa wanawezaje kuishi bila wizi, matusi, rushwa, zinaa, ulevi na bado wanayafurahia hayo maisha, pasipo kujua siri kuwa ni Roho Mtakatifu aliye ndani yao, anawasaidia udhaifu wao.

Na ili tujae Roho Mtakatifu ni lazima tufahamu kanuni ya kumpata Roho Mtakatifu, kama tu ili tupate kikokoteo wepesi (calculator) itakachotusaidia kutatua mahesabu magumu kwa haraka na wepesi ni lazima tujue jinsi ya kuipata au mahali pa kuipata na gharama zake.

Sasa tunampataje Roho Mtakatifu ili tuwezi kuishi pasipo sheria??

Tunampata kwa kanuni ifuatayo..

Matendo 2:37 “Walipoyasikia haya wakachomwa mioyo yao, wakamwambia Petro na mitume wengine, Tutendeje, ndugu zetu?

38 Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu”.

Kwa njia ya kutubu dhambi kwa kumaanisha kuiacha!, na kubatizwa kwa Maji mengi kwa jina la Bwana YESU, yule Roho ataingia ndani ya kuwezesha uwezo huo mkubwa wa kuishi kwa utakatifu bila mapambano makubwa moyoni.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho Mengine

ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

Ahadi Ya Roho Mtakatifu.

KUWA NA  MAFUTA YOTE YA ROHO MTAKATIFU NDANI YAKO.

ZIFAHAMU KARAMA 9 ZA ROHO MTAKATIFU NA UTENDAJI KAZI WAKE.

KAZI ZA ROHO MTAKATIFU