Mkomamanga ni nini? Na katika biblia unawakilisha nini?

by Admin | 9 October 2020 08:46 pm10

Mkomamanga ni nini?


Komamanga ni tunda lenye mbegu ndogo ndogo nyingi ndani yake, ambalo linaliwa kwa kumumunywa mumunywa mbegu zake mpaka utamu wote uishe, au kwa kukamuliwa juisi, ni tunda lenye ladha nzuri sana, na kisayansi linavirutubisho vingi sana mwilini, kama hukuwahi kulifahamu tunda hili tazama picha juu.

Katika biblia tunda hili linawakilisha mfanikio, au uzuri wa aidha taifa, au kitu au mtu.

Kwamfano ukisoma mstari huu;

Kumbukumbu 8:6 “Nawe uzishike amri za Bwana, Mungu wako, upate kwenda katika njia zake, na kumcha.

7 Kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yuakuingiza katika nchi nzuri, nchi yenye vijito vya maji, na chemchemi, na visima, vibubujikavyo katika mabonde na milima;

8 nchi ya ngano na shayiri, na mizabibu, na mitini, na mikomamanga; nchi ya mizeituni yenye mafuta, na asali”;

Utaona Mungu akilitaja tunda hili pamoja na mizabibu, na mitini, kuonyesha uzuri wa nchi ya ahadi ambayo Mungu aliwaambia wana wa Israeli wataiingia, kuonyesha ni jinsi gani nchi hiyo itakavyokuwa nzuri na yenye mafanikio makubwa..

Na ndio maana utaona hata sehemu nyingine, walipoasi, Mungu alitumia miti hii hii ya matunda kama mfano kuonyesha, alivyowafunguia milango ya Baraka na mafanikio katika mambo yao maovu, soma.

Hagai 1:18 “Tafakarini, nawaomba; tangu siku hii ya leo na siku zijazo; tangu siku ya ishirini na nne ya mwezi wa kenda, naam, tangu siku hiyo ulipowekwa msingi wa hekalu la Bwana tafakarini haya.

19 Je! Mbegu ingali ghalani? Naam, huo mzabibu, wala mtini, wala mkomamanga, wala mzeituni, haikuzaa kitu; tangu siku hii ya leo nitawabariki”.

Soma tena;

Yoeli 1:12 “Mzabibu umesinyaa, mtini nao umevia; Nao mkomamanga na mtende na mtofaa; Naam, miti yote ya mashamba imekauka; Maana furaha imekauka katika wanadamu”.

Pia tunda hili, linawakilisha mafanikio ya kazi za mtu.

Wimbo 6:11 “Nalishukia bustani ya milozi, Ili kuyatazama machipuko ya bondeni; Nione kama mzabibu umechanua, Kama mikomamanga imetoa maua”.

Wimbo 8:1 Laiti ungekuwa kama ndugu yangu, Aliyeyanyonya matiti ya mamangu! Kama ningekukuta huko nje, Ningekubusu, asinidharau mtu.

2 Ningekuongoza nyumbani mwa mamangu, Naye angenifundisha; Ningekunywesha divai iliyokolea,Divai mpya ya mkomamanga wangu.

Soma pia 1Samweli 14:2,

Hivyo kwa ujumla, tunda hili, limetumika kuwakilisha hali ya mafanikio ya taifa, mtu au kitu.

Lakini pamoja hayo ipo nchi ya mikomamanga halisi, kuliko ile ya Kaanani, ambayo wana wa Israeli waliingia lakini bado waliugua, walikufa, waliteseka n.k. , Nchi hiyo si nyingine  zaidi ya Yerusalemu mpya. Huko hakuna shida, wala njaa, wala magonjwa, wala vifo, wala ajali, wala dhiki, lakini  swali ni je! wewe na mimi tunayo nafasi humo?

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

MADHABAHU NI NINI?

JIHADHARI NA UONGO WA SHETANI UNAOKARIBIANA NA UKWELI.

MWEZI WA ABIBU/NISANI NI MWEZI GANI?

FANYIKA SIPORA WA KRISTO, UNYAKUO UPO KARIBU.

Wafilisti ni watu gani.

UNYAKUO.

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/10/09/mkomamanga-ni-nini-na-katika-biblia-unawakilisha-nini/