Pesa za bindoni ni nini?(Marko 6:8)

by Admin | 17 November 2020 08:46 pm11

Bwana Yesu aliposema pesa za bindoni alimaanisha pesa za mfukoni.. mfuko unaozungumziwa ni ule wa kuvaa kiunononi ambayo ndio ilitumika zamani. tazama picha.

Marko 6:7 “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu;

8 akawakataza wasichukue kitu cha njiani isipokuwa fimbo tu; wala mkate, wala mkoba, wala pesa za bindoni”;

Ni kwanini Bwana Yesu alisema hivyo?

Ieleweke kuwa Bwana Yesu hakumaanisha kuwa injili haihitaji fedha, wala mahitaji hapana, injili inahitaji fedha, tena sana ili isonge mbele.…Lakini hapo alikuwa halengi kazi ya injili   bali  aliwalenga wale wapeleka injili. Kwamba hao ndio wanapaswa wasifikiri kuwa inahitajika maandalizi mengi au makubwa ili wao wamtumikie Mungu.

Bwana aliwatuma wao kama wao, na mambo mengine yote aliwapa huko mbele ya safari. Na ndio maana sehemu nyingine aliwauliza hapo nilipowatuma hamna kitu  Je!  Mlipungukiwa na chochote? Wakasema hapana.

Luka 22:35 “Akawauliza, Je! Hapo nilipowatuma hamna mfuko, wala mkoba, wala viatu, mlipungukiwa na kitu? Wakasema, La!

Hiyo ni kuonyesha kuwa mahitaji ya muhimu aliwapatia. Huko walipoenda.  Hata na sisi, tunapaswa tujue kuwa tunapotaka kumtumikia Mungu tusifikirie sana hali zetu, labda tutaanzia wapi,au  tuna nini, au hatuna nini, hilo wazi tuliondoe, Ni kweli wazo hilo ni gumu kulipokea lakini ndio maagizo ya Bwana.. tunapaswa tuyaamini, na kwamba yeye mwenyewe atatupatia.

Shalom

Mada Nyinginezo:

Fitina maana yake nini kwenye biblia?

Kijicho ni nini? (Marko 7:22)

MZAZI, JALI MAISHA YA KIROHO YA MTOTO WAKO.

Kwanini wale dubu waliowauwa vijana wa Elisha walikuwa wa kike?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/11/17/pesa-za-bindoni-ni-ninimarko-68/