BADO TUTAHITAJI TU KUSAIDIANA.

by Admin | 4 July 2021 08:46 pm07

Siku moja nikiwa njiani nilikutana na mama mmoja mwenye mtoto, akaniomba shilingi elfu moja apande gari aelekee nyumbani kwake chanika, basi kwa kuwa hiyo pesa nilikuwa nayo nikampa, lakini baadaye kidogo, nilipanda gari, nikasahau kuwa sikuwa na hela nyingine yoyote ya cash mfukoni, tukiwa safarini kondakta, akaniomba nauli, nikajisachi sina pesa, ila ninayo kwenye simu, nikamwambia kondakta sina pesa hapa, naomba tukifika kituoni, nikatoe nikupe, lakini kondakta akaonekana kama sio mwelewa akadhani kama natumia ujanja tu ili nisimpe nauli yake..

Wakati naendelea kufikiria, na huku nikiangalia safari yangu haiishii mwisho wa kituo, nitashukia njiani hata nikienda kutoa atakuwa radhi kunisubiri?,.kulikuwa ni kijana mmoja anaonekana kama maskini, akatoa shilingi elfu moja akanipa, akaniambia chukua hii kondakta atakusumbua, nikamwambia ninayo nauli wacha tu tufike kituoni nitampa, lakini alinishurutisha kuichukua ile hela.

Nikakaa nayo kwa muda, nikitafakari, nikawa sina jinsi baadaye kidogo nikampa yule konda na yule kijana akashuka kwenye gari. Nikapata somo, wakati nadhani wenye shida ndio wanahitaji msaada, kumbe hata wewe usiye na shida utahitaji msaada ule ule kama wa yule mwenye shida.

Mama yule alikuwa na haja ya sh. Elfu moja, muda mchache baadaye uhitaji huo huo ulinigeukia mimi, japokuwa nilikuwa nayo. Ndugu yangu, utatembea, na gari lako, utatembea na mabilioni yako benki, utatembea na afya yako nzuri, lakini kamwe usiache kuwasaidia wenye uhitaji, kwasababu uhitahitaji ule ule wakati Fulani utaupitia hata wewe isipokuwa tu katika maumbile mengine.

Katika utajiri wako huo huo, unaweza ukafa njaa, kama tu vile yule mtu asiye na chakula kabisa, katika afya yako hiyo hiyo unaweza ukasumbuliwa na magonjwa kama tu mtu yule aliyelazwa pale muhimbili, katika nyumba yako nzuri, unaweza kulala nje kama tu yule mtu alalaye mabarazani, Vilevile katika elimu yako kubwa, hiyo hiyo unaweza kuwa mjinga sawa tu na yule ambaye hajasoma kabisa. Kamwe usifikirie kwasababu umeshapata kitu Fulani, ndio tayari umeepukana na tatizo hilo, ambalo watu wengine wanalipitia kwa kukikosa hicho. Lipindue hilo wazo kuanzia sasa.

Bwana atusaidie tujifunze unyenyekevu kwa watu wote, na kusaidiana sisi kwa sisi, kwasababu biblia inasema.

Mhubiri 1:6 “Upepo huvuma kusi, hugeuka kuwa kaskazi; hugeuka daima katika mwendo wake, na upepo huyarudia mazunguko yake.

7 Mito yote huingia baharini, walakini bahari haijai; huko iendako mito, ndiko irudiko tena”.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

HALI ZETU JINSI ZINAVYOWEZA KUATHIRI UTOAJI WETU.

NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

NIFANYALO WEWE HUJUI SASA; LAKINI UTALIFAHAMU BAADAYE.

WALA MSIUANGALIE MWILI, HATA KUWASHA TAMAA ZAKE.

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 3

ILI NIWE KIELELEZO KWA WALE WATAKAOMWAMINI BAADAYE.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/07/04/bado-tutahitaji-tu-kushirikiana/