Biblia inamaanisha nini inaposema “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake”?

by Admin | 19 August 2021 08:46 pm08

 Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.


JIBU: Hapa ni Mungu alikuwa anaonyesha tabia za mtu mwenye haki jinsi zilivyo kwamba huruma zake haziishi tu kwa wanadamu wenzake, bali pia zitadhihirika mpaka na kwa wanyama.

Kama vile Mungu sasa anavyowajali wanyama wake, kiasi kwamba hakuna hata mmoja anayekufa bila ya yeye kujua, na vivyo hivyo na sisi tunapaswa tuwe na tabia hizo, alisema ..

Mathayo 10:29 “Je! Mashomoro wawili hawauzwi kwa senti moja? Wala hata mmoja haanguki chini asipojua Baba yenu;”

Sehemu nyingine Bwana Yesu alisema maneno haya;

Luka 14:5 Akawaambia, Ni nani miongoni mwenu, ikiwa ng’ombe wake au punda wake ametumbukia kisimani, asiyemwopoa mara hiyo siku ya sabato?

 Akimaanisha kuwa, kumbe watu wengi walikuwa wanainajisi sabato pasipo wao kujua na Mungu asiwahesabie makosa, kwa tendo tu hilo la kuwaokoa wanyama wao.

Utaona pia sehemu nyingine, Balaamu Yule nabii wa uongo alipompigia Yule punda wake, mara tatu, Mungu alichukizwa sana na kitendo kile.. Na ndio maana swali la kwanza aliloulizwa na Yule malaika ni kwanini amempiga Yule punda kiasi kile? (Hesabu 22:32)

 Kuonyesha kuwa Mungu hapendezwi na kitendo cha utesaji wanyama.

Hivyo na sisi pia kama tulikuwa na tabia za kuwatesa wanyama, au kutoijali mifugo yetu, kiasi kwamba ukimkuta mbwa unamsindikiza na mawe,tuache hizo tabia, kama wanaishi na sisi pasipo madhara yoyote, hakuna sababu ya kuwapiga piga ovyo, au kuwafuga na kutowahudumia.

Kwasababu kitendo cha kuwatendea mema, biblia inasema kinaongeza pia siku za kuishi duniani soma,

Kumbukumbu 22:6 “Kiota cha ndege kikitukia kuwa mbele yako njiani, katika mti wo wote, au chini, chenye makinda au mayai, naye koo ameatamia juu ya makinda, au juu ya mayai, usimtwae yule koo pamoja na makinda;

7 sharti umwache yule koo aende zake, lakini makinda waweza kuyatwaa uwe nayo; ili upate kufanikiwa, ufanye siku zako kuwa nyingi”.

Hiyo ndio maana ya huo mstari ..Mithali 12:10 “Mwenye haki huufikiri uhai wa mnyama wake; Bali huruma za mtu mwovu ni ukatili”.

Bwana akubariki.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Na hekima imejulikana kuwa ina haki kwa watoto wake wote.

HAKUNA MTU ANIONDOLEAYE, BALI MIMI NAUTOA MWENYEWE

USIRUDI NYUMA KWA KUITUMAINIA HAKI YAKO.

SINA PESA SASA, YESU ATANISAIDIA NINI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/08/19/biblia-inamaanisha-nini-inaposema-mwenye-haki-huufikiri-uhai-wa-mnyama-wake/