by Admin | 6 January 2022 08:46 pm01
Neno Bushuti limeonekana mara moja tu katika biblia, na maana ya Neno hilo ni “Blanketi”.
Waamuzi 4:18 “Yaeli akatoka kwenda kumlaki Sisera, akamwambia, Karibu Bwana wangu, karibu kwangu; usiogope. Akakaribia kwake hemani, naye akamfunika kwa bushuti”.
Kipindi Sisera, Adui wa wayahudi anamkimbia Baraka, alifika kwenye nyumba ya mwanamke mmoja aliyeitwa Yaeli, na mwanamke huyu alimlaghai kwa hila na kumwua.
Kabla ya kumwua maandiko yanasema alimlaza na kumfunika kwa hilo Bushuti (yaani blanketi), na alipopata usingizi alimwua.
Habari hiyo kamili inapatikana katika mlango wa 4 wa kitabu hicho cha Waamuzi.
Maran atha!
Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,
Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Mada Nyinginezo:
Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/01/06/bushuti-ni-nini/
Copyright ©2025 unless otherwise noted.