Babeli ni nchi gani kwasasa?

by Admin | 12 March 2022 08:46 pm03

Eneo ambalo mji wa Babeli ulikuwepo, ni maeneo ya nchi ya IRAQ kwa sasa, Mji huu ndio uliokuwa maarufu kwa kuwa na “bustani zinazoelea”, lakini kwasasa mji huu haupo tena, wala maajabu yake hayapo!!,

kwasababu mji huo ulikuwa mji wa kishetani na ulifanya dhambi nyingi, na Mungu akauadhibu.. mahali ulipokuwepo pamebakia tu mbuga!!, sawasawa na unabii Mungu alioutoa juu ya mji huo.

Isaya 13:19 “Na Babeli, huo utukufu wa falme, uzuri wa kiburi cha Wakaldayo, utakuwa kama Sodoma na Gomora hapo Mungu alipoiangamiza.

20 Hautakaliwa na watu tena kabisa, wala watu hawatakaa ndani yake tangu kizazi hata kizazi. Mwarabu hatapiga hema yake huko, wala wachungaji hawatalaza makundi yao huko.

21 Lakini huko watalala hayawani wakali wa nyikani; na nyumba zao zitajaa bundi; mbuni watakaa huko; na majini watacheza huko.

22 Na mbwa-mwitu watalia ndani ya ngome zake; na mbweha ndani ya majumba ya anasa; na wakati wake u karibu kufika, na siku zake hazitaongezeka”..

Kwahiyo leo hii hakuna kilichosalia pale!, pamebakia tu kuwa sehemu ya makumbusho ya kale.

Kumbuka shetani aliinyanyua Babeli ya kwanza, ambayo Mungu aliiharibu kwa kuchafua lugha za wajenzi wao!, na kazi ya ujenzi ikaishia pale! (Mwanzo 11), Lakini hakukata tamaa bali aliitengeneza Babeli nyingine, ambayo ndiyo iliyokuja kuangushwa na falme za Umedi na Uajemi, ikawa jaa!!

Lakini sasa shetani katengeneza Babeli nyingine ambayo ni ya KIROHO, hii iliyopo sasa ndio mbaya kuliko mbili zilizotangulia, na ndio kitovu cha machukizo na machafuko yote yan chi (sawasawa na Ufunuo 17).

Kwa urefu juu ya Babeli hiyo ya rohoni iliyopo sasa, fungua hapa >>> BABELI YA ROHONI.

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

MISTARI YA BIBLIA KUHUSU WATOTO.

JE WEWE NI LAZARO YUPI, WA KWANZA AU WA PILI?

Ninawi ni nchi gani kwasasa?

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 12 (Kitabu cha Isaya)

TABIA ZITAKAZOMTAMBULISHA MPINGA-KRISTO AJAYE.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/03/12/babeli-ni-nchi-gani-kwasasa/