Kwanini Kristo hakuitwa Imanueli badala yake akaitwa Yesu?

by Admin | 29 May 2020 08:46 pm05

SWALI: Unabii uliotolewa na Isaya kumuhusu Kristo unasema angekuja kuitwa Imanueli (Isaya 7:14), lakini badala yake tunaona alikuja kuitwa Yesu? Ni kwanini?


JIBU: Tukisoma pale katika Mathayo 1:19-23 Inasema..

Mathayo 1:19 “Naye Yusufu, mumewe, kwa vile alivyokuwa mtu wa haki, asitake kumwaibisha, aliazimu kumwacha kwa siri.

20 Basi alipokuwa akifikiri hayo, tazama, malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto, akisema, Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uweza wa Roho Mtakatifu.

21 Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao.

22 Hayo yote yamekuwa, ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa nabii akisema,

23 Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; NAO WATAMWITA JINA LAKE IMANUELI; YAANI, MUNGU PAMOJA NASI”.

Jiulize ni kwanini biblia haijaishia tu pale kwenye jina Imanueli, badala yake ikamalizia kuandika mpaka tafsiri yake, yaani “Mungu Pamoja nasi”?..Ni Kwasababu msisitizo upo hapo kwenye hiyo tafsiri na sio jina tu..

Ukiangalia tena utaona Malaika anasema “Nao watamwita” Ikimaanisha “sisi” ndio tutakaomwita yeye kuwa ni Mungu ambaye yupo Pamoja nasi..Lakini yeye jina lake hasaa sio hilo bali ni YESU ..ambayo tafsiri yake ni (YEHOVA-MWOKOZI).

Jambo hilo limekuja kutumia kama lilivyo kwasababu sisi ndio tunaojua Yesu kwetu sisi si mwokozi tu, bali ni Zaidi ya mwokozi,..Ni Mungu kwetu, aliyeutwaa mwili akaishi Pamoja nasi..Kama maandiko yanavyosema..

Yohana 1:1 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu”…..

14 Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli”.

1Timotheo 3:16 “Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili, Akajulika kuwa na haki katika roho, Akaonekana na malaika, Akahubiriwa katika mataifa, Akaaminiwa katika ulimwengu, Akachukuliwa juu katika utukufu.”

“Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili”(Wakolosai 2:9) .

“tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Kristo Yesu, Mungu mkuu na Mwokozi wetu;(Tito 2:13)

Hivyo tunao ujasiri wote wa kusema kuwa YESU ni MUNGU WETU..

Yaani IMANUELI.

Haleluya.

Mada Nyinginezo:

KWANINI YESU KRISTO ALIKUJA DUNIANI?

nini maana ya haya maneno aliyosema Bwana ; Tuliwapiga filimbi wala hamkucheza; Tuliomboleza wala hamkulia?

 

WINGU KUBWA LA MASHAHIDI.

BWANA HUWAJUA HAO WAMKIMBILIAO.

NA YEYE ALIYEKETI JUU YA WINGU AKAUTUPA MUNDU WAKE JUU YA NCHI, NCHI IKAVUNWA.

Je! kuna ubaya wowote kuwaombea ndugu zetu waliokufa katika dhambi, Mungu awakumbuke katika ufalme wa mbinguni?.

NG’OMBE MWEKUNDU ALIYEZALIWA ISRAELI, ANAFUNUA NINI?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/05/29/kwanini-kristo-hakuitwa-imanueli-badala-yake-akaitwa-yesu/