MISTARI YA BIBLIA KUHUSU NDOA.

by Admin | 6 August 2020 08:46 am08

Jiunge na group la Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/FgA1HWRFZWH4IqqLunFGcs

Mistari ya biblia kuhusu ndoa  ni ipi?


Ndoa ni tendo ambalo Mungu aliliumba kwa makusudi kabisa, ili kumpa mwanadamu picha ya jinsi ndoa yake halisi itakavyokuwa kati ya yeye na watu wake, baada ya ulimwengu huu kuisha. 

Uhusiano walio nao mke na mume, ni mfano mdogo sana wa uhusiano atakaokuwa nao Mungu na watu wake watakaoshinda, katika mbingu mpya na nchi mpya.

Hivyo tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa za kibinadamu, na vilevile tutaitazama mistari michache ihusuyo ndoa ya ki-mbinguni(yaani Kristo na kanisa lake).

NDOA YA MKE NA MUME

Mwanzo 2:24 “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja”

Waefeso 5:25  “Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake”;

Waefeso 5:33  “Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mumewe”

Mithali 5:18 “…. Chemchemi yako ibarikiwe; Nawe umfurahie mke wa ujana wako”

Waefeso 4:2  “kwa unyenyekevu wote na upole, kwa uvumilivu, mkichukuliana katika upendo; 3  na kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani”.

Marko 10:9  “Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe”

Wimbo 8:6 “Nitie kama muhuri moyoni mwako, Kama muhuri juu ya mkono wako; Kwa maana upendo una nguvu kama mauti, Na wivu ni mkali kama ahera. Mwako wake ni mwako wa moto, Na miali yake ni miali ya Yahu. 

7 Maji mengi hayawezi kuuzimisha upendo, Wala mito haiwezi kuuzamisha; Kama mtu angetoa badala ya upendo Mali yote ya nyumbani mwake, Angedharauliwa kabisa”.

Waebrania 13:4  “Ndoa na iheshimiwe na watu wote, na malazi yawe safi; kwa maana waasherati na wazinzi Mungu atawahukumia adhabu”.

Mithali 30:18 “Kuna mambo matatu yaliyo ya ajabu kwangu, Naam, kuna manne nisiyoyafahamu. 

19 Mwendo wa tai katika hewa; Na mwendo wa nyoka juu ya mwamba; Mwendo wa merikebu katikati ya bahari; Na mwendo wa mtu pamoja na msichana”.

Mithali 31:10 “Mke mwema, ni nani awezaye kumwona? Maana kima chake chapita kima cha marijani”.

Mhubiri 4:9 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja; Maana wapata ijara njema kwa kazi yao. 

10 Kwa maana wakianguka, mmoja wao atamwinua mwenzake; lakini ole wake aliye peke yake aangukapo, wala hana mwingine wa kumwinua! 

11 Tena, wawili wakilala pamoja, hapo watapata moto; lakini mmoja aliye peke yake tu awezaje kuona moto”?

Mathayo 19:6  “Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe”

1Petro 3:7  “Kadhalika ninyi waume, kaeni na wake zenu kwa akili; na kumpa mke heshima, kama chombo kisicho na nguvu; na kama warithi pamoja wa neema ya uzima, kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe”

Malaki 2:16 “Maana mimi nakuchukia kuachana, asema Bwana, Mungu wa Israeli…”

Ruthu 1:16 “Naye Ruthu akasema, Usinisihi nikuache, Nirejee nisifuatane nawe; Maana wewe uendako nitakwenda, Na wewe ukaapo nitakaa. Watu wako watakuwa watu wangu, Na Mungu wako atakuwa Mungu wangu; 

17 Pale utakapokufa nitakufa nami, Na papo hapo nitazikwa; Bwana anitende vivyo na kuzidi, Ila kufa tu kutatutenga wewe nami”.

Yohana 13:34  “Amri mpya nawapa, Mpendane. Kama vile nilivyowapenda ninyi, nanyi mpendane vivyo hivyo”.

1Wakorintho 13:4  “Upendo huvumilia, hufadhili; upendo hauhusudu; upendo hautakabari; haujivuni;

5  haukosi kuwa na adabu; hautafuti mambo yake; hauoni uchungu; hauhesabu mabaya”;

Malaki 2:14 “Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako. 

15 Hakuna mtu mmoja aliyetenda hivi, ambaye alikuwa na ufahamu kidogo. Au je! Kuna mtu mmoja atafutaye mzao mwenye kumcha Mungu? Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana”.

Mistari ya biblia kuhusu ndoa ya;

KRISTO NA KANISA LAKE.

Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Isaya 54:5 “Kwa sababu Muumba wako ni mume wako; Bwana wa majeshi ndilo jina lake; na Mtakatifu wa Israeli ndiye Mkombozi wako; Yeye ataitwa Mungu wa dunia yote”.

2Wakorintho 11:2  “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi”.

Ufunuo 19:9  “Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo. Akaniambia, Maneno haya ni maneno ya kweli ya Mungu”.

Ufunuo 21:1  “Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya; kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza zimekwisha kupita, wala hapana bahari tena.

2  Nami nikauona mji ule mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, umewekwa tayari, kama bibi-arusi aliyekwisha kupambwa kwa mumewe”.

Luka 14:24  “Maana nawaambia ya kwamba katika wale walioalikwa, hapana hata mmoja atakayeionja karamu yangu”.

Luka 5:34 “ Lakini Yesu akawaambia, Je! Mwaweza kuwafanya wafunge walioalikwa arusini, akiwapo bwana arusi pamoja nao”?

Ufunuo 21:9 “…Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi-arusi, mke wa Mwana-Kondoo”.

Mathayo 25:1  “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi.

2  Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara.

3  Wale waliokuwa wapumbavu walizitwaa taa zao, wasitwae na mafuta pamoja nao;

4  bali wale wenye busara walitwaa mafuta katika vyombo vyao pamoja na taa zao.

5  Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.

6  Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.

7  Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.

8  Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.

9  Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.

10  Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.

11  Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.

12  Akajibu akasema, Amin, nawaambia, siwajui ninyi.

13  Basi kesheni, kwa sababu hamwijui siku wala saa.

Ufunuo 22:17  “Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure”.

Hivyo ni wajibu wetu mimi na wewe kuhakikisha kwa gharama zozote hatuikosi hii karamu ya mwana-kondoo mbinguni, Kumbuka kama tunavyojua huwa kinaanza ndoa kisha baadaye karamu,.vivyo hivyo na kwa Mungu pia, inaanza kwanza ndoa, ambayo Kristo anafunga na watakatifu wake hapa hapa duniani, na baadaye atawanyakua kwenda nao kula naye karamu kule mbinguni.

Kwa mapana na marefu juu ya somo hili la karamu ya mwanakondoo, angalia somo lililoorodheshwa chini baada ya hili; Lakini kikubwa zaidi, ni kuwa tuhakikishe na sisi ni bibi-arusi ambao wapo tayari kumkojea Bwana wao aje waende karamuni.

Na tunakuwa bibi-arusi kwa kumwamini Yesu, na kubatizwa, na kuishi maisha yampendezayo.

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda tukuunge kwenye group la mafundisho ya biblia,Whatsapp: basi utatutumia ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KARAMU YA MWANA-KONDOO.

https://wingulamashahidi.org/mafundisho-ya-ndoa/

UTAWALA WA MIAKA 1000.

MJI WENYE MISINGI.

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

HERI YULE ATAKAYEKULA MKATE KATIKA UFALME WA MUNGU.

DHIKI KUU INAKUJA NA UNYAKUO UPO KARIBU.

MIHURI SABA

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/08/06/mistari-ya-biblia-kuhusu-ndoa/