MISTARI YA BIBLIA YA FARAJA.

by Admin | 4 September 2020 08:46 am09

Jiunge na channel yetu ya Whatsapp, ujifunze biblia na upate Neno la siku kila asubuhi. kwa link hii >>> https://chat.whatsapp.com/GWxBOH2GXncIc0pwVIhnch

Mistari ya biblia ya faraja.


Unaweza ukawa unapitia katika wakati mgumu, wakati wa mateso, wakati wa majaribu, wakati wa jangwa, wakati wa shida wewe kama mkristo kwa ajili ya imani yako,. Lakini nachoweza kukwambia ni kuwa biblia peke yake, ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.. Haijalishi utaambiwa maneno elfu kumi ya faraja na wanadamu, lakini ni biblia pekee ndiyo inayoweza kukupa faraja ya kweli.

Hivyo itafakari mistari ifuatayo, ni lipo jambo ambalo litakutia nguvu katika safari yako ya Imani..

Wafilipi 4:13 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu”.

Isaya 41:10 “usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam, nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu”.

Isaya 40:31 “bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia”.

Kumbukumbu 31: 6 “Iweni hodari na moyo wa ushujaa, msiogope wala msiwahofu; kwa maana Bwana, Mungu wako, yeye ndiye anayekwenda pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha”.

Isaya 40:29 “Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo”.

1Wakorintho 10:13 “Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili”.

Kutoka 15:2 “Bwana ni nguvu zangu, na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu. Yeye ni Mungu wangu, nami nitamsifu; Ni Mungu wa baba yangu, nami nitamtukuza”.

Kumbukumbu 20: 4 “kwa maana Bwana, Mungu wenu, ndiye awaandamaye kwenda kuwapigania juu ya adui zenu, ili kuwaokoa ninyi”.

2Wakorintho 12:9 “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu”.

Isaya 12:2 “Tazama, Mungu ndiye wokovu wangu; Nitatumaini wala sitaogopa; Maana Bwana YEHOVA ni nguvu zangu na wimbo wangu; Naye amekuwa wokovu wangu”.

Mathayo 6:34 “Basi msisumbukie ya kesho; kwa kuwa kesho itajisumbukia yenyewe. Yatosha kwa siku maovu yake”.

Zaburi 27:1 “Bwana ni nuru yangu na wokovu wangu, Nimwogope nani? Bwana ni ngome ya uzima wangu, Nimhofu nani”?

Zaburi 31: 24 “Iweni hodari, mpige moyo konde, Ninyi nyote mnaomngoja Bwana”.

Zaburi 73:26 “Mwili wangu na moyo wangu hupunguka, Bali Mungu ni mwamba wa moyo wangu Na sehemu yangu milele”.

Zaburi 29: 11 “Bwana atawapa watu wake nguvu; Bwana atawabariki watu wake kwa amani”.

Zaburi 23:4 “Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”.

Zaburi 118:14 “Bwana ni nguvu zangu na wimbo wangu, Naye amekuwa wokovu wangu”.

Habakuki 3:19 “YEHOVA, aliye Bwana, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka”.

Yohana 16:33 “Hayo nimewaambieni mpate kuwa na amani ndani yangu. Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; mimi nimeushinda ulimwengu”.

2Wathesalonike 3:3 “Lakini Bwana ni mwaminifu, atakayewafanya imara na kuwalinda na yule mwovu”.

Luka 1:37 “kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu”.

Yeremia 29:11 “Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho”.

Wafilipi 1:6 “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu”;

Zaburi 34:8 “Onjeni mwone ya kuwa Bwana yu mwema; Heri mtu yule anayemtumaini”.

Mathayo 11:28 “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha”.

Inawezekana  pia hujaokoka, lakini leo hii unataka Yesu asikupite bila kuyaokoa maisha yako. Unasema mimi na dunia sasa basi, mimi na dhambi basi..Hivyo Kama umeamua leo kumgeukia Mungu kwa moyo wako wote, yeye mwenyewe anasema, “kila ajaye kwangu sitamtupa Nje kamwe”..Kwahiyo Leo hii Yesu ataingia ndani ya maisha yako kama umeamua kweli kumfuata…hivyo kama upo tayari fungua hapa kwa ajili ya kuongozwa sala ya Toba..>>>> KUONGOZWA SALA YA TOBA

Bwana akubariki.

Ikiwa utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu, kwa njia ya email, au whatsapp yako basi tutumie ujumbe kwenye namba hii tukuweke : +255789001312

Mada Nyinginezo:

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/09/04/mistari-ya-biblia-ya-faraja/