Maziwa yasiyoghoshiwa ni nini? Kwanini biblia inatumia mfano huo?

by Admin | 20 February 2021 08:46 am02

1Petro 2:1 “Basi, wekeni mbali uovu wote na hila yote, na unafiki na husuda na masingizio yote. 2 Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu”;

Kughoshi ni kugeuza, au kutia dosari, lengo likuwa ni kukifanya kionekane kama kile cha kwanza, leo hii utasikia maneno kama ‘vyeti vimeghoshiwa’, maana yake ni kuwa wametengeza vyetu bandia ili waonekane kama na wao ni wahitimu kumbe ni uongo. Utasikia tena watu pia ‘wanaghoshi fedha’, maana yake ni kuwa wanatengeneza fedha bandia ili zionekane kama zile halisi, zifae kwa manunuzi.

Sasa mtume Paulo aliposema yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, alitumia mfano wa maziwa yanyonywao na watoto wachanga kufananisha na Neno la Mungu. Kwamba maziwa yale kwa asili huwa hayagoshiwi, hayatiwi kitu kingine chochote, wala hayaingiliwi na uchafu wowote, kwani mtoto hujafyonza moja kwa moja kutoka kwa mama yake.

Lakini kama vile leo hii utaona mambo yamebadilika watoto wachanga hawapewi tena maziwa  yanayotoka moja kwa moja katika matiti ya mama zao, badala yake wanakwenda kuletewa maziwa mengine ya kwenye makopo, ya ng’ombe, ambayo kwa kutazama unaweza kuona yanafanana sana na yale ya mama,  lakini kumbe yapo mbali sana kiubora na kiafya kwa mtoto mchanga.  Utakuta hayo ya kwenye makopo yamechanganywa na vitu vingine wanavyoviita virutubisho, na kemikali baadhi za kuyafanya yasiharibike mapema..Sasa maziwa hayo ni maziwa yaliyoghoshiwa. Mtoto ananyweshwa kama mbadala wa maziwa halisi ya mama yake, na kamwe hayawezi kuwa na ubora ule ule kama wa yale ya mama.

Vivyo hivyo na sisi kama wakristo, tunapaswa tuyafyonze maziwa yanayotoka moja kwa moja kwa Mungu wetu mwenyezi, yanayotoka katika maandiko matakatifu (yaani BIBLIA), hayo ndio matiti yetu. Ili tuukulie wokovu katika afya njema za rohoni Mungu anazozihitaji.  Lakini kama tutataka tuikulie injili nyingine ambayo si ile tunayoisoma katika maandiko tufahamu, tunajidhohofisha wenyewe.

Na ndio hapo, utashangaa kwanini mkristo anashindwa kusimama vema katika Imani, leo yupo sawa kesho kaanguka katika dhambi, utakuta mwingine yupo katika kanisa kwa miaka mingi, lakini ukitafuta matunda yoyote kwa Mungu wake hana, ukitafuta ni wangapi alishawahi waleta kwa Kristo, hupati, hayo yote ni matokeo ya kunywa maziwa ya aina nyingine yasiyomtia mtu nguvu rohoni.

Ukiona unakaa mahali na kuhubiriwa injili ya mafanikio tu wakati wote,  auhubiriwi utakatifu, au mambo ya ufalme wa mbinguni na siku za mwisho, ujue kuwa hayo ni maziwa ya kughoshiwa, yanayofanana na yale halisi, hayatakusaidia chochote katika kuushinda ulimwengu.

Lakini mtume Paulo anasisitiza kwa kusema..‘Kama watoto wachanga waliozaliwa sasa yatamanini maziwa ya akili yasiyoghoshiwa, ili kwa hayo mpate kuukulia wokovu’

Unaona ni wajibu wetu kuitamani injili ya kweli, injili ile iliyoandikwa na mitume kwenye biblia, ili kwamba tuweze kuukulia wokovu wetu vema inavyostahili, tusishindwe na shetani kivyepesi, pia ili tuwe watu wa kumzalia Mungu matunda katika ukristo wetu.

Kumbuka hizi ni siku za mwisho, mafundisho mengi ya uongo yameenea sasa ulimwengu mzima, na ndio maana Bwana Yesu alituonya na kusema .ANGALIE JINSI MSIKIAVYO (Luka 8:18)..Akiwa na maana tuwe makini na yale tunayohubiriwa kwasababu si yote yanajenga roho zetu.Mengi ya hayo ni feki, yanatia ubovu roho zetu.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

MAMBO YA KUJIFUNZA KATIKA WARAKA WA PILI WA YOHANA.

MAMA UNALILIA NINI?

Bwana Yesu alimaanisha nini kusema “Saa yangu haijawadia?”

Je! Daudi hakuwa mtoto wa ndoa wa Yese? (Zab 51:5)

MAPEPO YANATAFUTA HIFADHI NDANI YAKO KWA BIDII SANA.

Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/02/20/maziwa-yasiyoghoshiwa-ni-nini-kwanini-biblia-inatumia-mfano-huo/