Nini maana ya Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu?

by Admin | 18 March 2021 08:46 am03

SWALI: Samahani mtumishi kuna andiko linatoka kitabu cha Mhubiri 7:29 sijalielewa vizuri linamaanisha nini

Mhubiri 7:29  “Tazama, hili tu nimeliona; Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu, lakini wamebuni mavumbuzi mengi”.


JIBU: Mungu alipomuumba mwanadamu alimuumba katika ukamilifu wote, Adamu na Hawa walikuwa ni watu ambao hawakuwa na kasoro yoyote, si ya kimwili, si ya kiroho. Waliumbwa katika ukamilifu wa furaha,amani, upendo, maarifa  na kumcha Mungu.

Lakini ilifika wakati, hawakuridhika, na vile ambavyo Mungu alivyowaumba na kuwaweka, wakataka kuwa sawa na Mungu, wakabuni namna yao wenyewe ya kuishi, ya kutaka uhuru wao wenyewe. Na ndio hapo utaona wakashawishika kwenda kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, ambayo Mungu aliwaambia wasile, Ili wakipate wanachokitafuta. Lakini matokeo yake ni kuwa mpaka sasa mwanadamu hajakipata alichokitafuta tangu wakati ule, kinyume chake ndio matatizo yalizidi kuongezeka japokuwa anajibunia kila siku njia zake mwenyewe za kuishi.

Mpaka sasa mambo hayo yanaendelea, tunavyoona watu wakijibadilisha maumbile yao, kisa tu hayawavutii machoni pao. Na ndio hapo utaona, wanawake wanachubua ngozi zao, ili waonekane weupe, wengine wanapaka make-up ili waonekane wa kitofauti na wenye mvuto zaidi, wanaweka kucha za bandia, wanavaa wigi za wazungu.. Yote hayo ni mavumbuzi mengi watu wanaojibunia..na kibaya zaidi leo hii wameshafikia mpaka hatua ya kubadilisha maumbile yao kwa kufanyiwa upasuaji na kunyeshwa madawa makali.

Hawataki tena kuwa wao wa asili kama Mungu alivyowaumba ,wanataka wawe kama wanavyotaka wao. Sasa badala mavumbuzi yao yawasaidie, kinyume chake ndio yanawaletea madhara kama sio kuwapoteza kabisa.

Hivyo, tunapaswa tujue kuwa si mpango wa Mungu tujigeuze mionekano yetu, kwasababu Mungu alituumba kwa mfano wake na sura yake, alishatuumbia ukamilifu ndani yetu,.Jukumu letu sisi ni kumcha yeye, na kuisiliza sauti yake basi.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.

Mada Nyinginezo:

Nini maana ya tumeumbwa kwa mfano na sura ya Mungu?

Nini maana ya “yasiyokuwapo hayahesabiki”(Mh 1:15)

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 1

Ufunuo 12 inaelezea vita vya wakati upi?

LAKINI NINYI, NDUGU, MSIKATE TAMAA KATIKA KUTENDA MEMA.

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2021/03/18/nini-maana-ya-mungu-amemfanya-mwanadamu-mnyofu/