Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

by Admin | 14 March 2022 08:46 am03

Marhamu ni nini? Na Manukato ni nini?

1) Marhamu ni nini?

Marhamu kwa lugha ya kiingereza ni “perfume”..kwa lugha ya kiswahili iliyozoeleka ni “pafyumu”. Pafyumu inatengenezwa kutoka katika mimea mbali mbali na inakuwa katika mfumo wa kimiminika, matumizi yake ni kukifanya kitu kiwe  chenye kutoa harufu nzuri, na kufukuza wadudu na baadhi ya viumbe viharibifu, Viwango na ubora wa pafyumu (marhamu) unatofautiana.

Zipo Marhamu za gharama kubwa, ambazo hazipungui nguvu yake ya harufu haraka! (Mfano wa hizo ndio zile Bwana Yesu alizopakwa kichwani na yule mwanamke, kipindi yupo nyumbani mwa Simoni, mkoma).

Mathayo 26:6 “Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,

7 mwanamke mwenye KIBWETA CHA MARHAMU YA thamani kubwa alimkaribia akaimimina kichwani pake alipoketi chakulani.

8 Wanafunzi wake walipoona, wakachukiwa, wakasema, Ni wa nini upotevu huu?

9 Maana marhamu hii ingaliweza kuuzwa kwa fedha nyingi wakapewa maskini”.

Na zile akina Mariamu, Magdalene walizoziandaa kwaajili ya kumpaka Bwana siku ile ya kwanza ya juma

Luka 23:56 “Wakarudi, wakafanya tayari manukato na MARHAMU. Na siku ya sabato walistarehe kama ilivyoamriwa”.

Lakini pia zipo Marhamu za gharama ndogo!, ambazo hazidumu sana katika mwili wa mtu.

Kwa urefu juu ya Marhamu Mwanamke aliyompaka Bwana kichwani na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa>> MARHAMU KICHWANI MWA BWANA

2) Manukato ni nini?

Manukato ni viungo ambavyo havipo katika mfumo wa kimiminika, ambavyo vikichomwa, au kupikwa au kuwekwa mahali basi vinatoa harufu Fulani inayovutia, au inayowakilisha jambo Fulani. Mfano wa manukato ni UDI, UVUMBA, na MANEMANE.. Kwasasa kuna maelfu ya aina za Manukato!

Kwa maelezo marefu kuhusu Manukato aina ya UVUMBA, na jinsi wakuhani walivyofukiza uvumba na ujumbe wake kiroho unaweza kufungua hapa >> KUVUKIZA UVUMBA NDIO KUFANYAJE?

Maran atha!

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema,

Kwa maombezi/Ratiba za ibada/ Ushauri/ Maswali.
Piga namba hizi: +255693036618 au +255789001312

pia kama utapenda uyapate mafundisho haya kwa njia ya Whatsapp au email basi tutumie ujumbe kwenye namba hizo hizo.


Mada Nyinginezo:

LIPI TUNAJIFUNZA KWA WALIOMWONA YESU ALIYEFUFUKA?

MUNGU HATAZAMI MOTO WA KIGENI,KUWA MAKINI!

Ratli/ Ratili ni nini katika biblia?

NAMNA YA KUMTAMBUA BIBI ARUSI WA KWELI WA KRISTO.

TOFAUTI KATI YA HEKALU, SINAGOGI NA KANISA NI IPI?

Rudi nyumbani

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2022/03/14/marhamu-ni-nini-na-manukato-ni-nini/