Title July 2026

UPANGA USHIKAMANAO NA MKONO

2 Samweli 23:9-10

[9]Na baada yake kulikuwa na Eleazari, mwana wa Dodai, Mwahohi, mmojawapo wa wale mashujaa watatu waliokuwa pamoja na Daudi; walipowatukana Wafilisti waliokuwa wamekusanyika huko ili kupigana, na watu wa Israeli walikuwa wamekwenda zao; 

[10]huyo aliinuka, akawapiga Wafilisti hata mkono wake ukachoka, na mkono wake ukaambatana na upanga; naye BWANA akafanya wokovu mkuu siku ile; nao watu wakarudi nyuma yake ili kuteka nyara tu. 

Kibaolojia mwili wa mwanadamu unapokamata kitu, kwa muda mrefu sana, kwa nguvu, huwa unatabia ya kukakamaa katika hali hiyo hiyo hata kama mtu huyo hatakuwa na nia ya kuendelea kukishikilia kitu hicho.

Ndicho kilichomkuta huyu shujaa wa Daudi, alipokutana na jeshi la wafilisti angali yupo peke yake. Aligundua kitu pekee ambacho kingeweza kumtetea ni upanga wake. Hivyo aliukamata kwa nguvu sana bila kuuachia, akaanza kupambana na wafilisti wale kwa muda mrefu,  hakujua kuwa mkono wake utabakia katika hali ile ile…yeye aliendelea tu kupigana vita, mpaka  baadaye aliposhangaa  kuona hana jitihada yoyote tena ya kuushika upanga, ni kama vile ulikuwa ni sehemu ya kiungo chake…kazi yake ilikuwa ni kurusha tu mkono kuupeleka anapotaka, huku upanga ukiwa tu pale pale kiganjani hautoki…

Kikawaida hali ikishafikia hatua hiyo huwa inamgharimu mtu masaa mengi hata siku,  ili kung’atuka kutoka kwenye kitu kilichoshikamana naye..wakati mwingine ili kuharakisha uponyaji, wengine hutumia maji ya uvuguvugu na kuchua kiganja kwa muda baadaye kunyosha kidole kimoja baada ya kingine…

Sasa askari wa mwilini ni kivuli cha mtu wa rohoni. Yeye naye ana mikono na analazimika wakati wote kuwa na upanga…Lakini si upanga tu, wa kushika, bali ule Ugandao na mkono. 

Waefeso 6:11-14,17

[11]Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. 

[12]Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. 

[13]Kwa sababu hiyo twaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kushindana siku ya uovu, na mkiisha kuyatimiza yote, kusimama. 

[14]Basi simameni, hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa dirii ya haki kifuani,..

[17]Tena ipokeeni chapeo ya wokovu, na upanga wa Roho ambao ni neno la Mungu; 

Kama maandiko yanavyotuonyesha hapo Mtu wa rohoni, hulazimika kubeba upanga wake, ambao ni Neno la Mungu.

Tunapoonyesha nia ya kuling’ang’ania Neno la Mungu, mwanzoni ni kama tutatumia jitihada zetu, lakini haitakuwa hivyo mbeleni …baadaye litashikamana na sisi..maana yake haitakuwa jitihada tena kuliishi.

Jambo lolote la kiroho, mfano maombi ya masafa marefu, mwanzoni ukianza utaona kama ni jitihada zinatumika lakini ukiendelea mara mbili, mara tatu utaona ni kawaida..

Mambo yote ya rohoni iwe ni upendo, unyenyekevu, utaanza kwa jitihada fulani lakini Kwasababu umekusudia tu kung’ang’nia kwa nguvu, utagandamana navyo.

Kumbuka hakuna wepesi wowote utakuja bila mtu kutia nia kwanza. Anza sasa kutendea kazi Neno la Mungu.

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:


 

ZIDI KUTAFUTA UJAZO WA ROHO MTAKATIFU.

Luka 11:13 “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni HATAZIDI SANA KUWAPA ROHO MTAKATIFU HAO WAMWOMBAO?”.

Kufuatana na maandiko haya, ni wazi kuwa Biblia inatufundisha  ujazo wa Roho Mtakatifu ni jambo endelevu siku zote za maisha ya mtu.

Ikiwa na maana kuwa ni lazima kila siku tujazwe Roho Mtakatifu kila siku kwa kipimo kipya, kwani maandiko yasema yeye hamtoi Roho kwa kipimo (Yohana 3:34) na tena yanasema Tujazwe Roho..

Waefeso 5:18 “Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; BALI MJAZWE ROHO”.

Sasa tunajazwaje Roho Mtakatifu?.

 Si kwa njia nyingine bali kwa kuomba.

Vifuatavyo ni vipengele muhimu katika maombi ya ujazo wa Roho Mtakatifu.

1.      OMBA KUFUNDISHWA NA ROHO MTAKATIFU.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, ATAWAFUNDISHA YOTE…”

Unaposoma BIBLIA, Roho Mtakatifu akawe mwalimu wako katika kulielewa vizuri Neno, tenga muda wa kutosha kumwomba MUNGU akakujaze Roho wake wa ualimu.

Watu waliojaa Roho Mtakatifu kweli kweli, wanajifunza Biblia na kuielewa vizuri kwasababu ndani yao Roho Mtakatifu anawafundisha.

Pia wanakuwa ni watu wenye maisha yaliyostaarabika kwasababu ndani yao wanaye mwalimu anayewafundisha kanuni za maisha.

2.      OMBA KUKUMBUSHWA NA ROHO.

Yohana 14:26 “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na KUWAKUMBUSHA YOTE niliyowaambia”.

Kuna mambo uliyowahi pengine kufunuliwa na MUNGU zamani, kwa njia ya Neno au ndoto, na umesahau, unapojaa Roho Mtakatifu, basi atakukumbusha yote aliyekuambia au kukuonesha.

Na sio tu kukumbusha  maneno ya Mungu au maagizo yake bali hata mambo yako mengine ya kimaisha yaliyo ya muhimu, Roho Mtakatifu atakukumbusha na kukutahadharisha.

Hata katika elimu za Dunia, Wanafunzi waliojaa Roho Mtakatifu, ni ngumu kusahau kabisa waliyojifunza, kwani yupo msaidizi ndani yao anayewakumbusha waliyojifunza.

Hali kadhali watu wenye Roho Mtakatifu kweli kweli huwa hawasahau maelekezo au maneno ya Mungu kwani yupo Msaidizi, Roho Mtakatifu anayewakumbusha kila siku.

Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba ujazo wa Roho Mtakatifu ndani yako.

3.      KUONGOZWA NA ROHO.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, ATAWAONGOZA awatie kwenye kweli yote….”.

Pia Roho Mtakatifu kazi yake nyingine ni kumwongoza Mtu, nini cha kusema, nini cha kufanya, au ni wakati gani wa kusema na wakati gani wa kunyamaza, ni wakati gani wa kutenda na wakati gani wa kutulia.

Zaidi sana Roho Mtakatifu pia anamwongoza mtu nini cha kusikiliza na nini ambacho hakifai kusikiliza au kufanya..

Na katika maombi pia, Roho Mtakatifu anamwongoza mtu nini cha kuomba na jinsi ya kuomba.

Warumi 8:26 “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo…..”.

Kwahiyo tenga muda wa kutosha kuomba Ujazo wa Roho Mtakatifu, ili uweze kunufaika na tunda hili la kuongozwa na Roho.

4.      OMBA KUFUNULIWA NA ROHO MAMBO YAJAYO.

Yohana 16:13 “Lakini yeye atakapokuja, huyo Roho wa kweli, atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, NA MAMBO YAJAYO ATAWAPASHA HABARI YAKE”.

  Ni muhimu sana kuyajua mambo yajayo yahusuyo maisha yako, kanisa, familia…kwani uishivyo sasa ni kutokana na kile unachokiona mbele yako, na Roho Mtakatifu pekee ndiye awezaye kufunua mambo yajayo ya mtu au watu kwa usahihi.

Kwa mambo haya manne, tutaimarisha  ile safari yetu ya kuenenda kwa Roho.

Wagalatia 5:16 “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili”.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kauli ya Bwana ya “Heri kutoa kuliko kupokea” tunaisoma wapi?

Swali: Katika Matendo 20:15, tunasoma Mtume Paulo akirejea kauli ya Bwana kwamba akisema “Heri kutoa kuliko kupokea”.. Je ni wapi katika Injili nne, Bwana YESU alisema maneno hayo?

Jibu: Tuanzie kusoma ule mstari wa 33..

Matendo 20:33 “Sikutamani fedha wala dhahabu, wala mavazi ya mtu.

34 Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono yangu hii imetumika kwa mahitaji yangu na ya wale waliokuwa pamoja nami.

35 Katika mambo yote nimewaonyesha ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapasa kuwasaidia wanyonge, NA KUYAKUMBUKA MANENO YA BWANA YESU, JINSI ALIVYOSEMA MWENYEWE, NI HERI KUTOA KULIKO KUPOKEA”.

Katika vitabu vyote vinne vya injili (yaani kitabu cha Mathayo, Marko, Luka na Yohana) hakuna mahali popote pameandikwa  maneno hayo ya Bwana kama yalivyo kwamba “heri kutoa kuliko kupokea”. Lakini ni wazi kuwa aliyasema mahali fulani ila hayakuandikwa katika vitabu vinne vya injili.

Tunalithibitisha vipi hilo?.. Turejee kitabu cha Yohana 21:24..

Yohana 21:24 “Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa”.

Hapa Mtume Yohana anasema, yapo mambo mengi aliyoyafanya Bwana YESU ambayo hayakuandikwa katika vitabu hivyo..maana yake yapo maneno mengi aliyoyafundisha na mifano mingi na ishara nyingi alizozifanya ambazo laiti kama zingeandikwa moja baada ya nyingine, dunia isingetoshea kwa vitabu..

Kwa mantiki hiyo basi tunaanza kuelewa kuwa maneno hayo ya “heri kutoa kuliko kupokea” ni kweli Bwana YESU aliwahi kuyasema mahali fulani, isipokuwa tu hayakunukuliwa na waandishi wa vitabu vinne vya injili.

Lakini pamoja na hayo, yapo maneno aliyoyasema yenye mlengo huo huo wa “uheri wa kutoa kuliko kupokea”

Luka 6:38 “Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa; kipimo cha kujaa na kushindiliwa, na kusukwa-sukwa hata kumwagika, ndicho watu watakachowapa vifuani mwenu. Kwa kuwa kipimo kile kile mpimacho ndicho mtakachopimiwa”.

Hii ni kauli ya Bwana YESU akitufundisha faida za kuwapa watu vitu, kwani tunapotoa ndivyo tutakavyopokea, na si tupokee kwanza na ndipo tutoe.. hiyo ikithibitisha kuwa ni kweli Bwana alifundisha uheri wa kutoa kuliko kupokea, na pia alituonya tujilinde na “uchoyo”.

Luka 12:15  “Akawaambia, Angalieni, jilindeni na choyo, maana uzima wa mtu haumo katika wingi wa vitu vyake alivyo navyo”.

Je umempokea YESU?.. Je una uhakika akirudi leo utakwenda naye?

Kama bado tengeneza maisha yako kwani majira tunayoishi ni ya hatari na parapanda ya mwisho imekaribia sana kulia.

Bwana atusaidie.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MAISHA YA IMANI NI KAMA SIFA YA MTI.

Mti una sifa moja, hautembei kutoka sehemu moja Kwenda nyingine, Utaupanda eneo fulani, utaridhika kubakia hapo hapo, haijalishi ni pabaya kiasi gani, utaenda utarudi miaka na miaka utaukuta pale pale, tofauti na viumbe hai vingine, ambavyo vyenyewe, vikiona hali si nzuri ya mahali, huama na Kwenda kutafuta makazi pengine. Lakini Mti hauna sifa hiyo, na bado utaendelea kustawi na kuwepo kwa miaka mingi zaidi ya viumbe hai vingine,  haijalishi ni kipindi gani kitapita.

Siri ya mti ipo wapi?

Jibu ni kwenye mizizi yake. Ijapokuwa hautembei kwa juu, lakini chini unatembea. Kwa juu utauna upo pale pale, lakini kwa chini mizizi yake ina mwendo, kila siku inaendelea katika safari ya huku na huko kutafutia virutubisho na maji.

Ni nini Bwana anatufundisha katika maisha ya mti.

Yeye hutupanda apendako.

Leo hii ni rahisi kulalamika, kwanini nimezaliwa hili taifa, kwanini hili kabila, kwanini hii familia, kwanini hii jinsia, kama ningezaliwa kwenye nchi ile, kabila lile, familia ile yenye Uchumi mkubwa ningekuwa mbali sana, ningestawi vizuri sana, ningeimarika kiroho kwa kasi kubwa mno… Kama umekuwa na Mawazo hayo, basi kuna tatizo la kiufahamu.

Mafanikio ya mwanadamu hayapo katika mazingira yake sasa. Mafanikio yake yapo katika mizizi yake rohoni. Mti ukikosa mizizi, hata uwe kwenye udongo mzuri kiasi gani hauwezi kukua popote.

Kama mwamini fahamu mzizi uliyopewa inauwezo wa kukustawisha popote, isipokuwa sifa yake ni ile ile yaani huwa haionekani kwa juu, hukaa matopeni, na huzidi Kwenda chini kila siku sio kurudi juu. Vivyo hivyo na sisi tujue nguvu yetu ipo rohoni, (pasipoonekana), Na katika unyenyekevu kwa Mungu wetu kila siku, ndivyo tutakavyoleta ustawi mema wa maisha yetu.

Kunyenyekea kiroho ni mjumuiko wa mambo : kumkubali Kristo, kutii maagizo yake (ikiwemo maombi, ushirika), kuliishi Neno, na kumtumikia yeye.

Huko ndiko kurefusha mizizi.

2 Wafalme 19:30

[30]Na mabaki yaliyookoka ya nyumba ya Yuda yatatia mizizi chini, na kuzaa matunda juu. 

Kristo alipaswa aishi Yerusalemu, mji  wenye sifa za kiroho na kisomi, lakini alipelekwa Nazareti , mji mnyonge, lakini huko huko alimzalia Mungu matunda, kwasababu mizizi yake ilienea sana.

Yusufu aliuuzwa utumwani, akawa msikwao, asiye na makazi kule Misri, lakini aliendea kuiimarisha mizizi yake, ijapokuwa kwa nje, hakukuonekana dalili ya badiliko lolote, lakini hatimaye, Mungu akamwinua akawa, mkuu kule kule Misri, Ndivyo ilivyokuwa kwa Danieli, Ayubu na watumishi wa Mungu.

Kabla ya kulalamikia mazingira, jiuliza kwanza je! Mizizi yangu, ipo sawa? Kwasababu haiwezekani mizizi ikawa sawa, mti ukafa. Haiwezekani ukawa mtakatifu halafu ukamezwa na mazingira.

Imarisha kiroho chako.

Shalom.

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.