Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.
Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.
Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingi kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kawaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…
Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;
Luka 1:28-29
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. [29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
Luka 2:17-19
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. [18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. [19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
Luka 2:48-51
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. [49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? [50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. [51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi mwake sio kwa akili zake…
Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.
Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…
Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.
Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.
Halidhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..
Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..
Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.
Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.
Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…
Hayo ndio mambo ya kubeba..
Geuka fikiri kama Mariamu..
Shalom
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Bwana akubariki.
Mafundisho mengine:
MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
Print this post
Utakaso wa ndani ni jambo endelevu.. hakuna hatua ambayo mtu amefika na kusema hapa sasa nimekamilika na sihitaji tena kujitakasa.. hakuna, lakini Biblia inatufundisha kuwa ni lazima tujitakase utu wetu wa ndani na kuwa wapya siku baada ya siku.
2Wakorintho 4:16 “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, LAKINI UTU WETU WA NDANI UNAFANYWA UPYA SIKU KWA SIKU”.
Na tena katika Ufunuo, maandiko yanasema “Mtakatifu na azidi kutakaswa (Ufunuo 22:11)”…
Sasa tunahoji kama Mtakatifu ameshakamilika kuna haja gani tena ya kuendelea kutakaswa?..Umeona?.. maana yake mtakatifu ni lazima aendelee na utakaso, ijapokuwa anaitwa “Mtakatifu” hakuna mahali atafika na kusema sasa nimekamilika..
Kila hatua ya usafi tunayoifikia inatufungua macho kuona uchafu mwingine uliopo ndani, na tunashughulika na huo, na mwingine na mwingine..mpaka siku ya ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).
Sasa twende mbele zaidi kuangalia vitu gani vinavyomtakasa mtu.
1. ROHO MTAKATIFU.
Roho Mtakatifu ndio sabuni ya kwanza ya kuondoa uchafu ndani ya Mtu ndio maana kuna umuhimu sana wa Mtu kupokea ujazo wa Roho Mtakatifu baada ya kuamini.
1Petro 1:2 “kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika KUTAKASWA NA ROHO, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu”.
Soma pia 1Wakorintho 6:11 na Warumi 15:16.
Kanuni ya Ujazo wa Roho Mtakatifu ni ile tunayoisoma katika Matendo 2:37-38, yaani kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na ubatizo wa maji mengi kwa jina la Bwana YESU.
2. NENO LA MUNGU
Maneno ya MUNGU yaliyoandikwa ndani ya kitabu ya Biblia ndio sabuni ndio sabuni ya pili kumtakasa mtu maisha yake. Bwana YESU alisema, tunatakaswa na kweli ya Neno la MUNGU.
Yohana 17:17 “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli”.
Soma pia Waefeso 5:26..
Mtu mwenye desturi ya kusoma Neno la Mungu ni lazima kila siku atakuwa anayaona makosa yake, lakini mtu asiyesoma Neno la Mungu kila siku atajiona yupo sawa na hahitaji kujitakasa wala kurekebishwa. Kwanini? Kwasababu Neno la Mungu ni kama kioo, mtu huwezi kujua uso wako upoje kama hujitazami kwenye kioo (Yakobo 1:22-23).
3. MAOMBI.
Maombi yanatakasa utu wa ndani katika kiwango kikubwa sana.. na si tu utu wa ndani bali vitu vyote pia..
1Timotheo 4:5 “kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba”.
Kiwango cha mtu kukua kiroho pia kinapimwa na kiwango cha Maombi, mtu anayeongeza viwango vyake vya maombi kila siku ni mtu pia anayekua kiroho.
WhatsApp
Swali: Je ni kweli malipo ya watu wote ni hapa hapa duniani?
Jibu: Turejee Mithali 11:31, tutapata mwanga wa swali letu..
Mithali 11:31 “Tazama, mwenye haki atalipwa duniani; Basi mwovu na mkosaji si mara nyingi zaidi?”
Ndio madhara ya makosa yote yanaanzia hapa hapa duniani, kabla ya kufa.. Kwamfano, Neno linasema “waheshimu baba yako na mama yako upate siku nyingi na za heri za kuishi duniani (Kutoka 20:12)”.
Sasa mtu ambaye hawaheshimu wazazi wake wala kuwatii, yeye ni kuwadharau na kuwatukana, mtu huyo ataanza kulipwa hapa hapa duniani kwa kupunguziwa miaka yake ya kuishi, na sio tu miaka ya kuishi, bali pia na ya Kheri, na sio hiyo tu bali na dhambi nyingine zote, kama wizi, au uzinzi hukumu yake inaanzia hapa hapa kama mtu haQtapigwa kwa maradhi basi atapigwa kwa roho za mapepo kwani uzinzi unaunganisha nafsi za watu.
Kwahiyo utaona ni kweli, adhabu ya waovu, inaanzia hapa hapa duniani, lakini hiyo bado haimaanishi kuwa baada ya kifo hakutakuwa tena na adhabu..La! Biblia inatufundisha kuwa hata baada ya kulipwa duniani bado kuna hukumu nyingine baada ya kifo ya ziwa liwakalo moto kwa mtu mwovu.
Kwa namna gani? Tusome maandiko yafuatayo..
Ufunuo 22:8 “Nami Yohana ndimi niliyeyasikia na kuyaona mambo hayo. Na hapo nilipoyasikia na kuyaona nalianguka, ili nisujudu mbele ya miguu ya malaika yule mwenye kunionyesha hayo”.
Umeona?.. Kwahiyo kama mzinzi akipigwa na maradhi kutokana na uzinzi alioufanya na akafa bila kutubu, ijapokuwa kateseka duniani na maradhi, bado tena ataenda kuteseka na adhabu ya ziwa la moto, hata watu wa Sodoma na Gomora Biblia inatuonyesha kuwa watahukumiwa tena siku ya mwisho ingawa tayari walishachomwa duniani (Soma Mathayo 10:145).
Ikifunua kuwa dhambi si ya kuchezea kabisa, ina madhara hapa duniani, na kule kwenye maisha ya baada ya kifo.
Upo usemi ya kwamba, Mungu atawapunguzia adhabu wale waliokufa katika dhambi ikiwa walidhurika wakiwa duniani, nataka nikuambia, dhambi ina matokeo makubwa kote kote, huku duniani na baada ya kifo.
Tunafundishwa kuikimbia dhambi, Sasa labda unajiuliza utaikimbiaje?.. Utaikimbia kwa kuanza kujitambua kuwa wewe ni mwenye dhambi na umemkosea MUNGU, baada ya hapo unachukua hatua ya kuungama, yaani kuomba toba kwa makosa yako yote, kwa kumaanisha kabisa.
Baada ya hapo, hatua inayofuata ni kubatizwa katika ubatizo sahihi wa maji tele, na Roho Mtakatifu atashuka juu yako kukutia muhuri wa milele. Kupitia Roho Mtakatifu atakayeingia ndani yako utaona mabadiliko ya kimaisha na kiutendaji ndani ikiwa kama hutamzimisha kwa kurudia dhambi kwa makusudi na kuacha kukusanyika na wengine.
Lakini kama utazingatia kuhudhuria vipindi vya Neno la Mungu na maombi ya pamoja, Roho Mtakatifu atakaa na wewe na hapo utakuwa umekamilisha hatua yako ya kuikimbia dhambi.
Bwana atusaidi.
Shalom.
NIMEAZIMIA KUWAKUSANYA MATAIFA. NIPATE KUWAMWAGIA GHADHABU YANGU
Ipi tofauti ya Hasira na Ghadhabu ya MUNGU?.
MALIPO YA UPOTEVU.
Ni kwa namna gani YESU KRISTO atawahukumu walio hai na waliokufa?
Kura hutupwa katika mikunjo ya nguo; Lakini hukumu zake zote ni za BWANA.
Jina la Bwana na Mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..
Ipo tofauti kati ya “kufahamu jambo” na “kulijua jambo”.. Unaweza kulifahamu jambo lakini usilijue kwa undani, vivyo hivyo kuna tofauti ya “kuyafahamu maandiko” na “kuyajua maandiko”. Hivi ni vitu viwili vyenye tofauti kubwa sana, hebu tujifunze kidogo kwa namna gani.
Tusome habari ifuatayo kisha tufafanue..
Mathayo 22:23 “Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza, 24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao. 25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake. 26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba. 27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye. 28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye. 29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.
Mathayo 22:23 “Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,
24 wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
25 Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
26 Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
27 Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
28 Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU.
30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.
Nataka tuzingatia hilo neno “MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU”.
Kumbuka hawa watu waliokuja kumwuliza Bwana hilo swali ni MASADUKAYO, ni watu wa dini, wanayoyafahamu maandiko karibia yote ya kwenye torati, na hapa wanamjia YESU kwa swali linalotoka katika maandiko ya MUSA (torati), wakisema “Mtu akifa basi mke wake anaruhusa ya kuolewa na ndugu wa karibu”.. jambo ambalo ni kweli kabisa lipo kwenye Biblia.
Lakini pamoja na kwamba walikuwa wanayafahamu hayo maandiko, bado Bwana YESU anawaambia “Hawayajui maandiko” na tena wanapotea sana.
“29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU. 30 Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni”.
“29 Yesu akajibu, akawaambia, MWAPOTEA, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO WALA UWEZA WA MUNGU.
Tuirudie tena habari hii katika Marko..
Marko 12:24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO wala uweza wa Mungu? 25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni. 26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? 27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana”.
Marko 12:24 Yesu akajibu, akawaambia, JE! HAMPOTEI KWA SABABU HII, KWA KUWA HAMYAJUI MAANDIKO wala uweza wa Mungu?
25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni.
26 Na kwa habari ya wafu ya kwamba wafufuliwa, hamjasoma katika kitabu cha Musa, Sura ya Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akisema, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo?
27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa walio hai. Hivyo mwapotea sana”.
Kumbe wakati ambao wanajidhania kuwa wanayajua maandiko kwa wingi wa mistari wanayoifahamu vichwani mwao, Kristo alikuwa anawaona hawajui chochote, na hiyo ndio sababu kuu ya kupotea kwao, hawayajui maandiko bali wanayafahamu tu.
Ndugu hatupaswi kuwa kama compyuta au simu ambao inaweza kuwa na vitu vingi pamoja na biblia nzima, lakini haiyajui maandiko, na wala yale maandiko hayaisaidii kwa chochote.
Hatupaswi kuwa na idadi kubwa ya mistari vichani ambayo haina ufunuo wowote. Mistari yenye nguvu na ibilisi anayoigopa ni ile iliyopo moyoni iliyobeba ufunuo, maana yake yenye uhai katika maisha ya mtu, na inayomwongoza, na yenye nguvu, na inayothibitisha imani.
Masadukayo walikuwa wanafahamu tu Musa kasema, na kujitamba katika hayo, pasipo kujua kuwa andiko bila ufunuo ni bure..
Sasa swali ni je!, tutayajuaje maandiko badala ya kuyafahamu tu?
Kinachotangulia ni kuyafahamu, ni lazima tuyafahamu na kufahamu kunakuja kwa kuyasoma au kuyasikia yanaposomwa.. baada ya kuyafahamu hatua inayofuata ni kuyajua. Na njia pekee ya kuyajua maandiko ni kwa kupitia Roho Mtakatifu..
Huyu peke yake ndiye anayeweza kutuhamisha kutoka katika kuyafahamu maandiko mpaka kuyajua, kwani anapoingia ndani ya Mtu, anakuwa ni Mwalimu mwingine wa ziada, kukufundisha maana za ndani ya maandiko uyasomayo, anakuchambulia na kukufundisha mambo ambayo hata ukirudia kusoma tena hilo andiko ulilolisoma utaona kama vile ni jingine kabisa, na huo ndio uhudumu wa agano jipya unaotajwa katika 2Wakorintho 3:6, ambao unatutosheleza.
2Wakorintho 3:6 “Naye ndiye aliyetutosheleza kuwa wahudumu wa agano jipya; si wa andiko, bali wa roho; kwa maana andiko huua, bali roho huhuisha”.
Je tayari umempokea Roho Mtakatifu?.. kama bado mwamini YESU na tubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha, kisha tafuta ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Bwana YESU KRISTO, baada ya hapo Roho Mtakatifu ataingia ndani yako na kukaa na wewe siku zote, kwani ahadi ya Roho Mtakatifu ni kwa kila mtu.
Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu. 39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
Matendo 2:38 “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.
39 Kwa kuwa ahadi hii ni kwa ajili yenu, na kwa watoto wenu, na kwa watu wote walio mbali, na kwa wote watakaoitwa na Bwana Mungu wetu wamjie”.
JE UNAZAA MATUNDA NA KUWAPONYA MATAIFA?
Ipi tofauti ya “Majibu” ya Maombi na “Majaribu”.
Ipi Tofauti ya Agano jipya na Agano la Kale?.
TOFAUTI KATI MAASKOFU, MASHEMASI, WAZEE WA KANISA NI IPI?
Nini tofauti kati ya kileo na divai ?
Swali: Turejee…
Jibu: Zaburi 1:5 “Kwa hiyo wasio haki HAWATASIMAMA hukumuni, Wala wakosaji katika kusanyiko la wenye haki”.
Andiko hili halimaanishi kwamba wasio haki (yaani watu waovu) hawatasimamishwa siku ya hukumu, La! haimaanishi hivyo, bali kinyume chake inamaanisha “watasimamishwa” lakini hawataweza kujitetea wala kushinda hukumu.
Neno “kusimama” linamaanisha “kushinda au kufanikiwa”… kwahiyo Wasio haki wote watahukumiwa, na sehemu nyingine nyingi katika maandiko zinathibitisha hilo..
2Petro 2:9 “basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, NA KUWAWEKA WASIO HAKI KATIKA HALI YA ADHABU HATA SIKU YA HUKUMU; 10 na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka”.
2Petro 2:9 “basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, NA KUWAWEKA WASIO HAKI KATIKA HALI YA ADHABU HATA SIKU YA HUKUMU;
10 na hasa wale waufuatao mwili katika tamaa ya mambo machafu. na kudharau mamlaka”.
Ni njia moja tu mtu anaweza kuitumia kuepuka hukumu ya MUNGU, nayo ni Kumwamini Bwana YESU KRISTO na kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi, na kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu (Marko 16:16).
Yohana 5:24 “Amin, amin, nawaambia, Yeye alisikiaye neno langu na kumwamini yeye aliyenipeleka yuna uzima wa milele; WALA HAINGII HUKUMUNI, bali amepita kutoka mautini kuingia uzimani”.
Je biblia inajichanganya kwa habari ya hukumu ya Mungu (Yohana 12:47 na Yohana 5:22, 27).
Nini maana ya Hukumu haina huruma kwake yeye asiyeona huruma?
Yohana 3:12
[12]Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?
SWALI: Je! Hayo Mambo ya duniani ni yapi? Na hayo mambo ya mbinguni pia ni yapi Yesu aliyoyamaanisha?
JIBU: Ukianza kusoma tokea vifungu vya juu utaona sababu ya Bwana Yesu kusema maneno hayo, ni baada ya yule Nikedemo mkuu wa mafarisayo kumfuata usiku ili kumuuliza maswali, lakini Yesu akamjibu kwa kumwambia kuhusu habari za kuzaliwa mara ya pili, lakini jambo hilo likawa gumu sana kwa nikodemu kulipokea…akamweleza Bwana yawezekanikaje mambo hayo? …Ndipo Yesu mwishowe akayasema maneno hayo;
12]Ikiwa nimewaambia mambo ya duniani, wala hamsadiki, mtasadiki wapi niwaambiapo mambo ya mbinguni?
Sasa hapo hamaanishi alikuwa anafundisha mambo ya duniani, hapana…bali alikuwa anatumia mifano ya duniani kueleza yale ya rohoni ili iwe rahisi watu kuelewa..kwamfano hapo alitumia mifano ya mtu kuzaliwa, vilevile akatumia mifano ya tabia ya upepo kumfafanulia Nikodemu aelewe mtu wa rohoni naye anavyopaswa awe…mahali pengine alitumia mifano ya wakulima, wafanyabiashara, maharusi, wavuvi, wafalme. wanyama n.k.
Ilikufundisha ufalme wa Mungu ulivyo na unavyofanya kazi..
Lakini mambo ya mbinguni ni yale ambayo hayana uhalisia na maisha yetu ya duniani kabisa…mambo hayo huwezi yaeleza kwa mifano ya kidunia..Hivyo ni kuyapokea tu kwa imani.
Kwamfano jinsi gani hekima ya Mungu isipopatikana popote isipokuwa ndani ya Yesu Kristo. Na jinsi gani Mungu aliumba ulimwengu kwa kupitia Kristo, ambaye alikuja kama mwana aliye Mungu yuleyule (Yohana 1:1-4).
Mambo hayo hayakuweza kusadikika kwa hekima za kibinadamu, ndio maana yalifichwa yakaja kufunuliwa baadaye kwa Roho Mtakatifu kwa mitume kuwa ndiye Mungu mwenyewe katika mwili( 1Timotheo 3:16)
Ndio maana wayahudi na hata watu wengine leo hii wa dini wanashindwa kuelewa iweje Mungu awe na mtoto, wakati hana mshirika…halafu huyo huyo mtoto awe ndio yeye tena.
Jambo kama hili halina mifano ya kibinadamu ya kujitosheleza kuelezea, ni kuamini tu!…lakini kwa imani waziona kazi zake na kujua hakika Kristo ndiye Mungu mwenyewe bila tashwishwi…Hivyo amini tu, uelewa kamili utaufahamu ufikapo mbinguni, ni sawa na Yesu alivyomwambia Nikodemu upepo huvuna upendako, hujui utokako vilevile hujui uendako, lakini sauti yake waisikia…ndivyo ilivyo katika asili ya uungu wa Mungu.. Tunamjua Kristo kuwa ni Mungu kwa kazi zake kuu na timilifu juu ya maisha yetu..
Ni nini Bwana anataka wewe ujue.
Sehemu kubwa ya mambo yanayotuzunguza yanahubiri habari za ufalme wa mbinguni. Kama hatutaelewa kwa kuitafakari mifano hii, kamwe tusidhani tutaelewa yale yasiyoingia maanani kabisa tuyasikiapo.
Je! Umempa Yesu maisha yako? Kumbuka hizi ni siku za mwisho na Yesu amekaribia kurudi, unasubiri nini usiokoke?
Tubu sasa upokee uzima wa milele. Ikiwa unahitaji msaada huo wa kuokoka basi wasiliana nasi kwa namba zetu hizi;
Kwa ajili ya mwongozo wa sala ya Toba na ushauri.
+255789001312 / +255693036618
UNAWAZA NINI SASA, JUU YA UFALME WA MBINGUNI?
BALI WANA WA UFALME WATATUPWA NJE!.
JIFUNZE KUTOA KATIKA HAZINA YAKO VITU VIPYA NA VYA KALE.
2 Yohana 1:10-11
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu. [11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
[10]Mtu akija kwenu, naye haleti mafundisho hayo, msimkaribishe nyumbani mwenu, wala msimpe salamu.
[11]Maana yeye ampaye salamu azishiriki kazi zake mbovu.
Ni salamu ya namna gani ambayo ililengwa hapo?
JIBU: Ukisoma habari yote tokea juu utaona mtume Yohana anazungumzia kundi la wadanganyifu ambao walitokea wengi duniani wakati ule, ni kundi la watu waliopinga kuja kwa Yesu katika mwili kwa namna ya kibinadamu, akasema hao ndio wapinga Kristo.
Na mbeleni akatoa katazo la kutowakaribisha hata majumbani kwao, wala kuwapa salamu, maana kuwapa salamu ni kushiriki kazi zao mbovu.
Swali je ni salamu ya namna gani ililengwa hapo.?
Salamu zinazozungumziwa hapo si salamu hizi za kijamii za “umeamkaje, au shikamoo, au za mchana” hapana bali ni salamu za kiroho ambazo hata wakati ule wayahudi walipozisema zilimaanisha ushirika mmoja katika kiimani. Kwamfano, walipokutana walibusiana na kusema “Amani ya Bwana iwe pamoja nawe”..
Sasa salamu kama hiyo utajiuliza ni bwana yupi ikiwa huyo mwingine haamini katika fundisho kama lenu.. ukimsalimia basi unakubaliana na bwana wake ambaye hajaja katika mwili. Tayari umeshazishiriki kazi zake.
Ni sawa na leo labda tuseme unakutana na watu wanaomwamini kweli Yesu, lakini Yesu ambaye hajafufuka, yupo kaburini mpaka sasa, halafu anakuja anakusalimia “Bwana Yesu asifiwe” na wewe unasema Amina..Mtu mgeni akipita akakusikia atajua kuwa mna imani moja kuhusu Yesu Kristo ambaye hajafufuka.
Hivyo hata kwa wakati huu, salamu zetu za kiroho zisimame mahali ambapo tunajua imani tulio nayo kuhusu Kristo ni moja.
Kwasababu salamu tu, hutangaza, zina nguvu kama lilivyo fundisho.
ANDALIZI LA MWISHO LA UJIO WA MPINGA KRISTO.
JAWA SANA MOTO ULAO.
Jina la Bwana wetu YESU KRISTO libarikiwe, karibu katika kujifunza Biblia.
Upo usemi usemao “wanadamu tumeumbiwa maradhi”..Usemi huu ni wa hekima za ulimwengu, ambao Biblia inasema ni upuuzi mbele za Mungu (1Wakorintho 3:19).
Ni kweli maradhi yapo lakini hatupaswi kuyakiri na kuyakumbutia kama sehemu yetu, (ikiwa tumeshampokea YESU) ….hata kama yapo ndani yako si sahihi kusema “hayo ni ya kwako” au “umeumbiwa”, ni kauli ambayo ni hatari sana.
Kwanini Maradhi si sehemu yetu tuliomwamini YESU? Na kwanini hatupaswi kutawaliwa nayo?.
Hebu tujifunze kidogo historia ya Maradhi mabaya na hatari kibiblia.
Kipindi wana wa Israeli wanatoka MISRI, kuelekea nchi ya Ahadi, Kanaani, Mungu aliwaambia yale maradhi yaliyokuwa yanawapata MISRI hayatawafuata Kaanani..
Kumbukumbu 7:15 “Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote; wala hatatia juu yako MARADHI YO YOTE MABAYA UYAJUAYO YA MISRI, lakini atayaweka juu ya wote wakuchukiao”.
Maana yake ni kwamba wakiwa Misri pamoja na kwamba walikuwa katika utumwa wa mwilini lakini pia Misri ILITAWALIWA NA MAGONJWA YA KUTISHA (Soma Kutoka 15:26 na Kumbukumbu 28:60).
Misri haikuwa sehemu salama kiroho na hata kimwili, kulikuwa kuna mlipuko wa magonjwa ya ajabu na ya kutisha, ambayo hayo yalitokana na miungu wa Misri waliyokuwa wakiiabudu..Na Bwana aliwaonya wana wa Israeli kwamba wakirudi kuitumikia hiyo miungu basi yale maradhi ya MISRI yatavuka kuwafuata waendako.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe. 61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kumbukumbu 28:60 “Naye atakurejezea maradhi yote ya Misri juu yako uliyokuwa ukiyaogopa, nayo yataambatana nawe.
61 Tena kila ugonjwa, na kila pigo yasiyoandikwa katika kitabu cha torati hii, atakutia nayo Bwana juu yako, hata utakapokwisha kuangamizwa”.
Kwahiyo tunachoweza kuona ni kuwa “Magonjwa yote asili yake ni Misri”, na Mungu aliyaweka kwa waMisri kutokana na maisha yao ya kuabudu miungu (shetani)..
Sasa swali kwanini yatutawale sisi ambao hatuabudu miungu ya Misri, na wala hatupo Misri, vile vile kama yanavyowatawala waMisri (watu ambao hawamjui Mungu)?
Ni swali la kutafakari sana..
Ukiona kuna ugonjwa unakusumbua miaka mingi, na umejaribu kutumia matibabu ya hospitalini yaliyo halali lakini tatizo linabaki kuwa sugu, au linakwenda baada ya muda linarudi..hebu wakati wa leo simama na kusema “imetosha”.
Huenda hujajua tu haki yako ndio maana ibilisi anakutesa na kukusumbua…anakujengea saikolojia kwamba huo ugonjwa ni wa kwako na huwezi kupona.. Leo hii simama na kusema “Magonjwa ya Misri si sehemu yangu”.
Kama umeokoka kweli kweli, usikae ukiri kwa kinywa chako, au uamini moyoni mwako kuwa “magonjwa ni sehemu yako”.. anza kuanzia leo kufuta kalenda za kwenda hospitali hospitali kila mara.
Tatizo linalowakabili watu wengi waliookoka ni kuamini na kujiwekea matumaini katika madawa na mahospitali, sio vibaya kuamini hivyo, lakini kunadumaza imani yako kwa MUNGU na kuyapa nafasi magonjwa ya Misri juu yako.
Si kila dalili tu ya mafua unayoyasikia unakimbilia dawa!..si kila homa tu inayokupata unakimbilia hospitalini utaacha lini hiyo tabia?.. Hufanyi dhambi lakini unadumaza imani yako.
Jenga tabia ya kuamini kuwa ninaweza kuwa na afya na uzima bila ya madawa wala hospitali, kwasababu wewe sio Mmisri, kwahiyo Maradhi ya Misri hayakuhusu, wala taarifa za maradhi ya Misri si sehemu yako.
Afya yako ni ya muhimu sana, ukiwa na maradhi hata uwezo wako wa kiutendaji kiroho unakuwa hafifu, hivyo usikubali hata kidogo, maandiko yanatufundisha hivyo kwamba ni mapenzi ya Mungu tuwe na afya zetu..
3Yohana 1:2 “Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako, kama vile roho yako ifanikiwavyo”
Ikiwa una maradhi yanayokuonea leo kwa imani fuatisha maneno yafuatayo na yatakuacha haraka sana..
Sema “Bwana YESU ninasogea mbele zako, ninaomba unisamehe nilipofungua mlango wa maradhi katika maisha yangu, lakini pia naomba unisamehe nilipopungukiwa imani, siku leo ninakiri uzima na afya, ninayakataa maradhi yote ya Misri juu ya mwili wangu, kwakuwa mimi sio Mmisri, kuanzia leo mimi ni mzima na wala sitasumbuka tena, ninaomba na kuamini katika jina kuu lako Bwana YESU KRISTO. Amen”
Nini maana ya kuinuliwa juu ya nchi? (Yohana 12:32).
JINSI MATENDO YA IMANI YANAVYOWEZA KULETA UTAMBULISHO MPYA KWA MTU.
UTAIKUZAJE IMANI NDANI YAKO?
Je ni kweli imani ya mtu ndiyo itakayomuokoa, na si kitu kingine?
Je! Imani ya mitume ipo katika maandiko?
Jina la Bwana YESU KRISTO libarikiwe, karibu tujifunze maandiko..
shetani hana jipya zaidi ya kunakili (kucopy) vile vilivyopo na kuvutumia kinyume.
Kwamfano kafara za wanyama kama mbuzi na kondoo kwaajili ya utakaso hazikuanzia kwa shetani, bali zilianza kwa MUNGU, ambapo katika Agano la kwanza (yaani Agano la kale) damu za wanyama hao zilitumika kwaajili ya utakaso, lakini sasa Agano jipya hazitumiki tena kwani Damu ya YESU ni bora zaidi ya damu za wanyama.
Kwahiyo shetani anachokifanya ni kunakili kilichokuwa kinatumika zamani (kisicho na matumizi tena) na kukileta siku za mwisho kwaajili ya matumizi yake, ndio maana utaona waganga wa kienyeji na wachawi ndio sadaka zao hizo.
Sasa sio tu hilo, lakini pia katika utumishi, shetani anayo desturi ya kutengeneza nakala..
Kwa namna gani?
Hebu turejee ile habari ya yule mchawi aliyeitwa.. “Bar-YESU” katika Matendo 13?..tuzisome habari zake kidogo kisha tuendelee mbele..
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU; 7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Matendo 13:6 “Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake BAR-YESU;
7 mtu huyu alikuwa pamoja na liwali SERGIO PAULO, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu”
Huyu “Bar-Yesu” ni nabii wa uongo na ni mchawi, lakini ajabu ni kwamba jina lake limebeba jina la YESU ndani yake.. Je unaelewa maana ya Bar-Yesu?.. maana yake ni “Mwana wa YESU” hiyo ndio tafsiri yake..
Kwahiyo huyu mchawi na nabii wa uongo, alikuwa ni mtu anayemjua YESU na anayedai kufundisha habari za YESU, lakini nyuma yake alikuwa ni mwongo.
Na jambo jingine la ajabu ni kwamba huyu Bar-Yesu alikuwa ni mwalimu wa kiroho wa mtu mmoja aliyeitwa “Sergio-Paulo”… Je unaelewa maana ya Sergio-Paulo?…maana yake ni “Mhudumu-Paulo”..
Kwahiyo wakati YESU wa Mnazareti, anammiliki Paulo mtumishi wa Mungu, yupo mtu anaitwa Bar-YESU anayemmiliki Sergio Paulo.
Kwahiyo hapa kuna “Sergio-Paulo” na “Bar-Yesu” na kuna “Paulo” na “YESU”. Kuonyesha kuwa shetani hana jipya zaidi ya kunakili vile vilivyopo vilivyo halali na kuvigeuza kwa matumizi yake.
Maandiko yanasema hivyo…
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. 15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
2Wakorintho 11:14 “Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru.
15 Basi si neno kubwa watumishi wake NAO WAKIJIGEUZA WAWE MFANO WA WATUMISHI WA HAKI, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao”.
Kwahiyo si kila anaitwa mtumishi wa YESU ni mtumishi kweli wa YESU, vile vile si kila anayejiita ni Mkristo, ni Mkristo kweli kweli, ni muhimu kuwa macho sana, na kujua vipimo halisi vya kuwatambua manabii wa uongo, waalimu wa uongo, wachungaji wa uongo, waimbaji wa uongo pamoja na wakristo wa uongo.
Na kipimo hiko si kingine zaidi ya NENO LA MUNGU, baada ya kujaa Roho Mtakatifu, Neno la MUNGU pekee ndio kipimo cha kumjua huyu ni wa MUNGU au wa ibilsi, hii ni sauti ya Mungu au ya ibilisi.
Je umeokoka?.. unao uhakika wa kwenda mbinguni ikitokea parapanda imelia leo?
Kama bado haujampa YESU maisha yako, bado parapanda haijalia leo, lakini muda wowote mambo yanabadilika, hivyo fanya mabadiliko kabla ya mabadiliko makuu kutokea.
JIHADHARI NA ROHO YA YEZEBELI.
Roho ya Malipizi/ roho za malipizi ni nini?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
MKUU WA UZIMA AKUWEKE HURU.
UNAMALIZAJE MWAKA WAKO, JE NA MUNGU AU SHETANI?
Mfundishe mtoto namna ya kutumia jina la Yesu katika kutenda mambo yake yote.