Title 2026

NAMI NITAMPA ILE NYOTA YA ASUBUHI.

Ufunuo  2:26 “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa,

27 naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama mimi nami nilivyopokea kwa Baba yangu.

28 Nami NITAMPA ILE NYOTA YA ASUBUHI”.

Je unaijua nyota ya ASUBUHI nini?

Hii si nyingine  zaidi ya YESU KRISTO mwenyewe.

Ufunuo 22:16 “Mimi Yesu nimemtuma malaika wangu kuwashuhudia ninyi mambo hayo katika makanisa. Mimi ndimi niliye Shina na Mzao wa Daudi, ile NYOTA YENYE KUNG’AA YA ASUBUHI”.

Ahadi ya kuishi na YESU milele ni ahadi kuu sana, ni furaha isiyo na kifani kuishi na YESU milele.

Ni furaha isiyo na kifani kumtazama milele yeye aliyemwaga damu yake pale msalabani kwaajili yetu sisi tusiostahili.

Lakini ni hasara kubwa sana kukosa kuwa na YESU milele. Ndio maana katika kitabu hiko cha Ufunuo Bwana  YESU mwenyewe anasema yeye ashindaye atampa “Ile nyota ya asubuhi”.

Maana yake yeye atakayeshinda atakaa na YESU milele.

Je umempokea YESU?.. Je una uhakika kwamba atakaporudi utakwenda naye mawinguni na kukaa naye milele?.

1 Wathesalonike 4:17 “Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo TUTAKUWA PAMOJA NA BWANA MILELE”.

Kama bado mpe leo YESU maisha yako kwa kutubu na kubatizwa kwa maji na kwa Roho Mtakatifu.

Shalom.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Biblia ina maana gani inaposema katika kuota kwao huutia mwili unajisi?

Yuda 1:7-8

[7]Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele. 

[8]Kadhalika na hawa, katika kuota kwao, huutia mwili uchafu, hukataa kutawaliwa, na kuyatukana matukufu. 

Maandiko hayo, yanazunguzia tabia ya watu waasi ambao wameshaijua kweli lakini wamependa kuendelea katika dhambi zao.

Hivyo katika andiko hilo anasema katika kuota kwao huutia mwili uchafu…sasa huko kuota kunakozungumziwa hapo sio ile hali ya kulala na kuota ndoto…hapana bali ni maono yao, yaani ndoto zao za jinsi watakavyokuwa baadaye, namna wanavyojiona baadaye..sasa hiyo namna ndio sio nzuri bali ni ya kujitia mwili uchafu.

Kuutia mwili uchafu ni nini?

Kuutia mwili uchafu ni ile hali ya kuruhusu matendo yote ya mwilini kukutawala…matendo hayo yanazunguziwa vema katika Wagalatia 5:19-21

[19]Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, 

[20]ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, 

[21]husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. 

Haya ndio watu wanayoyaona mbele yao, wanayoyawaza na kuyatazamia wakati wote, wanayoyaota yaje kutokea..

Fikra za watu wengi leo ni ili baadaye waishi kiasherati, wafanye anasa kwa pombe, ulafi, waibe..

Hii ni kutufunulia pia kunajisika sio mpaka mtu akatende jambo lenyewe bali ile kulitamania, tu au kulitarajia mbeleni…tayari ameshajinajisi.

Jiulize kuota kwako ni kupi? Kama mtoto wa Mungu, lazima tujue sisi yatupasa kuota maendeleo ya kazi ya Mungu, kuota ukuaji wa kiroho, kuota upendo, kuota kuingia mbingu mpya na nchi mpya,..namna hiyo humfanya mtu kuendelea katika utakaso.

Shalom.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Yuda alimaanisha nini kusema “wokovu ambao ni wetu sisi sote”

KITABU CHA YUDA: SEHEMU YA 1

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

Print this post

USIGEUKE KWA KUUME WALA KWA KUSHOTO

Kama wewe ni msafiri utakuwa umegundua kuwa nyasi zilizopo katikati ya barabara zenye vumbi huwa haziathiriwi na tairi za gari.

Utakuta barabara inapitiwa kila siku na magari yenye tairi zenye nguvu na nzito lakini katikati ya barabara utaona mstari wa nyasi, zilizo salama kabisa.

Ikifunua kuwa si kila kilichopo katikati ya hatari kipo hatarini, kuna watu wanaonekana kama wapo katikati ya changamoto na hatari nyingi lakini wapo salama, na kuna wengine wanaonekana kama wapo pembezoni (mahali salama) lakini ndio wapo hatarini.

Watu waliosimama kweli na YESU, wanaonekana ambao hawasogezi mguu wao kulia wala kushoto, ni watu wanaoonekana wamwisho kabisa duniani, na wenye wanaopotea, watu waliojikana nafsi kwaajili ya YESU ni watu wanaonekana wamepotea,

Watu wanaotukanwa, na kudhalilika kwaajili ya misimamo yao ya kiimani wanaonekana kama wamepotea lakini ukweli ni kwamba wao ni mfano wa nyasi zilizopo katikati ya barabara, hazikanyagwi wala kuathiriwa na tairi za magari.

Siku zote wanasimama na Zaburi 23..

Zaburi 23:1 “BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.

2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.

3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.

4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”

Kama ulikuwa unasuasua katika Imani na Wokovu, huu ni wakati wako wa kusimama katika njia kuu.

Simama kwa imani na tembea kwa ujasiri katikati ya njia yako ya wokovu, usisogeze mguu wako kushoto wala kulia nawe utakuwa salama, na utaona wema wa MUNGU.

Mithali 4:25-27 “Macho yako yatazame mbele.

26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike;

27 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni”.

Vile vile kama bado haujaokoka, fahamu ya kuwa hizi ni siku za mwisho, na Bwana amekaribia sana kurudi. Na upendo wake kwako ni ule ule usio na mwisho,

YESU anawapenda watu wote wa kike na kiume, wakubwa kwa wadogo, walio na maradhi na wenye afya, wenye uwezo na wasio na uwezo,

Maandiko yanasema kwa moyo mtu huamini hata kupata Haki na kwa kinywa hata kupata wokovu.(Warumi 8:9-10).

Leo hii mwamini moyoni na mkiri kinywani ubadilike na kuwa mwana wa MUNGU, Mzao wa mbinguni.(1Peteo 2:9).

Bwana akubariki.

 

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

UMEUFIKILIA MLIMA SAYUNI?.

Waebrania 12:22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”

Nyakati za Nabii Musa,Ulikuwepo mlima uliojulikana kama mlima wa Mungu, au Sinai, au mlima Horebu.

Katika mlima huo, Mungu aliposhuka hakuruhusiwa mtu mwingine kuusogelea isipokuwa Musa tu peke yake, hata mnyama aliyekaribia alikufa.

Kwani ulikuwa umejaa utukufu wa MUNGU, ulioambatana na radi na umeme na ngurumo zinazotisha.

Na kutokana na hali hiyo, ni Musa tu peke yake ndiye aliyepata kibali cha kuusogelea mlima huo na kusikia sauti ya MUNGU, wengine wote walibaki chini, kusubiria kusikia kile Musa alichoambiwa na MUNGU.

Lakini katika agano jipya, tunasoma kwamba upo mlima mfano wa huo, lakini si katika mwili bali katika roho, na mlima huo una utukufu mkubwa kuliko ule wa Sinai, Musa alioupanda.

Mlima huu wa rohoni, nao pia unaitwa Sinai, ambao umejaa malaika wa Mungu, na wenye utukufu mwingi.

Tofauti na mlima ule wa kwanza wa mwilini ambao ni Musa tu ndiye aliyeruhusiwa kuupanda, mlima huu wa rohoni unapandwa na mtu yeyote aliye ndani ya imani kamili ya YESU KRISTO.

Waebrania 12:21 “Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.

Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”,

Na faida za kuupanda mlima huu (Sinai ya rohoni) ni kwamba mtu atapata nafasi ya kumkaribia MUNGU zaidi na kumsikia MUNGU zaidi kuliko Musa alivyomsikia kule Sinai,

Pia atashuka na utukufu mkuu zaidi ya ule Musa aliokuwa nao aliposhuka hata uso wake ukang’aa.

Swali linarudi je wewe ni miongoni mwa watu walioufikia huo mlima wa MUNGU?.

Lakini labda utajiuliza pia mtu ataufikiaje huo mlima?..

Biblia imetupa majibu..

Zaburi 24:3 “Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?

4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.

5 Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake”.

Sasa tunapataje mikono safi na mioyo myeupe, itakayotufanya tustahili kufika katika mlima huo mtakatifu?.

Njia ni moja tu, kumwamini Bwana YESU, Kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kupokea Roho Mtakatifu, na kila siku kuishi maisha  ya utakatifu.

Kwa njia hiyo basi tutaweza kufikia kilele cha baraka, kwani ni Neema kuu tulipewa ya sisi kuufikia mlima wenye utukufu zaidi ya ule Musa aliopanda.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

SHIKA JEMBE NA SURURU CHIMBA MAHANDAKI. 

2 Wafalme 3:16-17

[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. 

[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu. 

Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..

Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.

Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..

Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..

Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.

Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.

Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.

Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…

Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…

Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.

Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.

Mwanzo 2:6

[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi. 

 

Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.

Bwana akubariki

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

 

Print this post

UKIMBIE UHURU WA ULIMWENGU

Umewahi kujua tofauti ya makundi haya mawili ya MBWA?.

Kundi la kwanza Mbwa wanaotembea huru barabarani na kundi la pili ni wale Mbwa wanaofugwa majumbani?.

Utaona Mbwa wanaozurula mitaani bila makao rasmi, huwa hawana afya, wanadharaulika, na ijapokuwa wanao uhuru wa kwenda popote watakapo lakini bado huwa hawana afya huwa ni wenye maradhi.

Utaona mbwa anayekatiza mitaani, ataona vyakula vingi vinapikwa, ataona minofu mingi ikitengenezwa na wanadamu, atasikia harufu ya kila aina ya chakula kizuri lakini hatakula?.

Lakini tukirudi kwa wale Mbwa wanaofugwa majumbani ni kinyume chake.

Wao wana afya kwasababu wanalishwa na wanaowafuga, pia ni jasiri kwasababu wanaaminiwa na wanaowafuga.

Hawana haja ya kuhangaika kutafuta chakula kwani wanaletewa, hawana haja ya kujitibu kwani wanatibiwa na wanaowafuga kwa ufupi wanaishi maisha ya raha isipokuwa tu hawana uhuru wa kuzurula ovyo na kukatiza mitaani.

Ni hivyo hivyo kwa watoto waliotoroka kwao na kuishi mitaani, huwa hawana afya njema, wala ustawi ijapokuwa wana uhuru wa kufika popote watakapo na kufanya chochote watakacho..

Lakini watoto wanaolelewa nyumbani hawana uhuru wa kwenda popote watakapo au kufanya chochote watakacho lakini ndio wenye ustawi mzuri na wanaofanikiwa.

Ni hivyo hivyo kwetu pia, Uhuru wa kufanya chochote na kutenda chochote tutakacho ni uhuru potofu ambao, mwisho wake ni kuharibika na kudharaulika.

Lakini tukikubali kulelewa na MUNGU kama watoto wanaopendwa basi tutafika mbali na kustawi sana.

Kama upo nje ya hifadhi rudi nyumbani kwa baba yako leo, kwa kutubu dhambi na kumkaribisha YESU, Na Bwana atakupokea na kukulea kama mtoto anayependwa sana.

Waefeso 5:1 “Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa”.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Print this post

Huduma ya kuendelea kuwa mwaminifu pale wachache wanapokusikiliza.

Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu. 

Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.

Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo,  lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana,  injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..

Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.

Yeremia 7:27

[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia. 

Ezekieli 2:3-7

[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. 

[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. 

[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. 

[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. 

[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana. 

Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.

Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.

Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao  sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.

Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.

Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni. 

Mungu akubariki sana.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.

SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.

KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.

Print this post

MTU WA NNE, ANADHIHIRISHWA KWA MOTO

Shedraki, Meshaki, na Abednego, walipokataa kuisujudia sanamu ya mfalme, kama tusomavyo maandiko, walifungwa na kutupwa kwenye tanuru ya moto,  lakini wakiwa kule motoni, alionekana mtu wa nne, ambaye mfalme Nebukadreza alimwona kama mwana wa Mungu,  ndiye Yesu Kristo mwenyewe.

Danieli 3:24  Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme.
25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.

Nachotaka ufahamu ni kwamba mtu wa nne, alikuwa Pamoja nao, siku zote, lakini kufunuliwa machoni pa watu, ilihitaji moto, ikiwa na maana nje ya moto, hakutambulika Dhahiri machoni pa wengi, bali kwa wale tu waliomwamini, tena mioyoni mwao.

Moto ni nini?

Moto, ni shinikizo lolote juu ya Imani ya mtu kwa Yesu Kristo, ambalo wakati mwingine  linahatarisha hata maisha yake. Huu moto wengi wanaukwepa lakini hawajui kuwa ndio unaompa Kristo nafasi ya kujifunua zaidi kwenye maisha yako.

Ukiona unataka kufukuzwa kazi kisa, siku za jumapili huwendi kazini unahudhuria ibadani, fahamu kuwa Kristo anaumbika Dhahiri kwenye maisha yako.

Ukiona unahatarisha biashara yako, kisa umegoma kula rushwa, ndivyo Kristo anakwenda kuonekana Dhahiri kwenye kazi zako, ni jambo tu la muda..

Ukiona, unafukuzwa, unapigwa, unafungwa, kwasababu ya msimamo wako mkali wa kimafundisho unaokemea dhambi, ujue kuwa, Kristo anakwenda kusimama na wewe kwa viwango vingine vya juu sana.

Moto kimsingi si mzuri, upitapo ni lazima utasikia maumivu, lakini mbele ya Kristo, hauna nguvu, hivyo vitisho, mapigo, vifungo, dhihaka, havina nguvu yoyote, kwasababu yeye yupo Pamoja na wewe muda huo, ndivyo ilivyokuwa kwa Shedraki, Meshaki na Abednego, hawakuungua kwasababu ya ule moto.

Badili fikra zako, badala ya kuhuzunika kwa majaribu, Bwana anasema furahi, kwasababu huko ndipo viwango vyetu vya kumuona Kristo vipo.

Maran atha.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

Kwanini Mungu azungumze na Ayubu kupitia upepo wa kisulisuli (Ayubu 38:1)

VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).

USIYAKUBALI MARADHI YA MISRI

Print this post

Je ni kweli Mungu haangali utu wa nje katika kumpatia mtu haki au hukumu?.

Swali: Katika 1Samweli 16:7 tunasoma, MUNGU anamwambia nabii Samweli kuhusu mtu atakayempaka mafuta kama Mfalme katika nyumba ya Yese, kwamba yeye haangalii uso kama wanadamu wanavyoangalia.


Jibu: Turejee..

1Samweli 16:6 “Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.

7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, USIMTAZAME USO WAKE, WALA UREFU WA KIMO CHAKE; KWA MAANA MIMI NIMEMKATAA. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; MAANA WANADAMU HUITAZAMA SURA YA NJE, BALI BWANA HUUTAZAMA MOYO”.

Andiko hili linalenga MAUMBILE ya ASILI ya Mtu, kwamba hayo ndio MUNGU hayaangalii kama kipimo cha kumpatia mtu “haki” au “hukumu”, na mambo hayo ni kama rangi ya mtu, urefu, ufupi, ulemavu, au uzima..

Mambo hayo hayatutofautishi sisi kwa sisi mbele za MUNGU. Kwamba ukiwa mfupi au mrefu au mweupe au mweusi basi ndio unaweza kupata kibali mbele za MUNGU. La!, hayo ni mambo ambayo MUNGU hayaangalii kabisa..

Lakini jinsi tunavyoiweka miili yetu, na kuivisha na kuilisha na kuinywesha ni vitu ambavyo MUNGU anavitazama sana kwasababu vipo ndani ya uwezo wetu, lakini urefu na ufupi hakuna mtu anajipangia, ni maumbile ya asili ya MUNGU mwenyewe.

Kwahiyo mtu anapovaa mavazi ya jinsia nyingine, au yanayouchora mwili wake, hayo yanajalisha sana mbele za MUNGU (1Timotheo 2:9, Kumbukumbu 22:5), au mtu anapojichubua au kujichora mwili wake Mungu anatazama (Soma Walawi 19:28).

Kwahiyo Bwana MUNGU, aliposema Haangalii uso, maana yake hashawishwi na maumbile ya asili  ya mtu. Je umempokea YESU?. Una hakika YESU akirudi leo utakwenda naye?.

 Kama bado haujampokea YESU unasubiri nini? Mwamini leo na ubatizwe kwa maji na kwa Roho Mtakatifu.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.

Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?

MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.

TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.

NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?

Print this post

AU NATAKA KUWAPENDEZA WANADAMU?

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”

Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchukiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.

Ni kufanya jambo machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.

Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.

Mathayo 6:2,5

[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…

[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.

Ni hali mbaya sana, Mahali  pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..

Yohana 12:42-43

[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.

Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kanisani.

Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana na Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)

Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.

Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukanwa, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.

Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.

Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.

Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.

Wagalatia 1:10

[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.

Bwana akubariki.

Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea

Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.

Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10

Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312

Bwana akubariki.

Mafundisho mengine:

MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.

Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)

USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.

Print this post