Kama wewe ni msafiri utakuwa umegundua kuwa nyasi zilizopo katikati ya barabara zenye vumbi huwa haziathiriwi na tairi za gari.
Utakuta barabara inapitiwa kila siku na magari yenye tairi zenye nguvu na nzito lakini katikati ya barabara utaona mstari wa nyasi, zilizo salama kabisa.
Ikifunua kuwa si kila kilichopo katikati ya hatari kipo hatarini, kuna watu wanaonekana kama wapo katikati ya changamoto na hatari nyingi lakini wapo salama, na kuna wengine wanaonekana kama wapo pembezoni (mahali salama) lakini ndio wapo hatarini.
Watu waliosimama kweli na YESU, wanaonekana ambao hawasogezi mguu wao kulia wala kushoto, ni watu wanaoonekana wamwisho kabisa duniani, na wenye wanaopotea, watu waliojikana nafsi kwaajili ya YESU ni watu wanaonekana wamepotea,
Watu wanaotukanwa, na kudhalilika kwaajili ya misimamo yao ya kiimani wanaonekana kama wamepotea lakini ukweli ni kwamba wao ni mfano wa nyasi zilizopo katikati ya barabara, hazikanyagwi wala kuathiriwa na tairi za magari.
Siku zote wanasimama na Zaburi 23..
Zaburi 23:1 “BWANA ndiye mchungaji wangu, Sitapungukiwa na kitu.
2 Katika malisho ya majani mabichi hunilaza, Kando ya maji ya utulivu huniongoza.
3 Hunihuisha nafsi yangu; na kuniongoza Katika njia za haki kwa ajili ya jina lake.
4 Naam, nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti, Sitaogopa mabaya; Kwa maana Wewe upo pamoja nami, Gongo lako na fimbo yako vyanifariji”
Kama ulikuwa unasuasua katika Imani na Wokovu, huu ni wakati wako wa kusimama katika njia kuu.
Simama kwa imani na tembea kwa ujasiri katikati ya njia yako ya wokovu, usisogeze mguu wako kushoto wala kulia nawe utakuwa salama, na utaona wema wa MUNGU.
Mithali 4:25-27 “Macho yako yatazame mbele.
26 Ulisawazishe pito la mguu wako, Na njia zako zote zithibitike;
27 Usigeuke kwa kuume wala kwa kushoto; Ondoa mguu wako maovuni”.
Vile vile kama bado haujaokoka, fahamu ya kuwa hizi ni siku za mwisho, na Bwana amekaribia sana kurudi. Na upendo wake kwako ni ule ule usio na mwisho,
YESU anawapenda watu wote wa kike na kiume, wakubwa kwa wadogo, walio na maradhi na wenye afya, wenye uwezo na wasio na uwezo,
Maandiko yanasema kwa moyo mtu huamini hata kupata Haki na kwa kinywa hata kupata wokovu.(Warumi 8:9-10).
Leo hii mwamini moyoni na mkiri kinywani ubadilike na kuwa mwana wa MUNGU, Mzao wa mbinguni.(1Peteo 2:9).
Bwana akubariki.
Washirikishe na wengine habari hizi njema kwa kushea
Ikiwa utapenda kupata msaada wa kumpokea Yesu maishani mwako bure, Basi wasiliana nasi kwa namba uzionazo chini ya makala hii.
Pia kwa kupokea mafundisho ya kila siku kwa njia ya WHATSAPP, jiunge na channel yetu kwa kubofya link hii >> https://whatsapp.com/channel/0029VaBVhuA3WHTbKoz8jx10
Kwa mawasiliano: +255693036618 au +255789001312
Mafundisho mengine:
Print this post
Waebrania 12:22 “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”
Nyakati za Nabii Musa,Ulikuwepo mlima uliojulikana kama mlima wa Mungu, au Sinai, au mlima Horebu.
Katika mlima huo, Mungu aliposhuka hakuruhusiwa mtu mwingine kuusogelea isipokuwa Musa tu peke yake, hata mnyama aliyekaribia alikufa.
Kwani ulikuwa umejaa utukufu wa MUNGU, ulioambatana na radi na umeme na ngurumo zinazotisha.
Na kutokana na hali hiyo, ni Musa tu peke yake ndiye aliyepata kibali cha kuusogelea mlima huo na kusikia sauti ya MUNGU, wengine wote walibaki chini, kusubiria kusikia kile Musa alichoambiwa na MUNGU.
Lakini katika agano jipya, tunasoma kwamba upo mlima mfano wa huo, lakini si katika mwili bali katika roho, na mlima huo una utukufu mkubwa kuliko ule wa Sinai, Musa alioupanda.
Mlima huu wa rohoni, nao pia unaitwa Sinai, ambao umejaa malaika wa Mungu, na wenye utukufu mwingi.
Tofauti na mlima ule wa kwanza wa mwilini ambao ni Musa tu ndiye aliyeruhusiwa kuupanda, mlima huu wa rohoni unapandwa na mtu yeyote aliye ndani ya imani kamili ya YESU KRISTO.
Waebrania 12:21 “Na hayo yaliyoonekana jinsi yalivyokuwa ya kutisha, hata Musa akasema, Nimeshikwa na hofu na kutetemeka.
Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi”,
Na faida za kuupanda mlima huu (Sinai ya rohoni) ni kwamba mtu atapata nafasi ya kumkaribia MUNGU zaidi na kumsikia MUNGU zaidi kuliko Musa alivyomsikia kule Sinai,
Pia atashuka na utukufu mkuu zaidi ya ule Musa aliokuwa nao aliposhuka hata uso wake ukang’aa.
Swali linarudi je wewe ni miongoni mwa watu walioufikia huo mlima wa MUNGU?.
Lakini labda utajiuliza pia mtu ataufikiaje huo mlima?..
Biblia imetupa majibu..
Zaburi 24:3 “Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake? 4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila. 5 Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake”.
Zaburi 24:3 “Ni nani atakayepanda katika mlima wa BWANA? Ni nani atakayesimama katika patakatifu pake?
4 Mtu aliye na mikono safi na moyo mweupe, Asiyeiinua nafsi yake kwa ubatili, Wala hakuapa kwa hila.
5 Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake”.
Sasa tunapataje mikono safi na mioyo myeupe, itakayotufanya tustahili kufika katika mlima huo mtakatifu?.
Njia ni moja tu, kumwamini Bwana YESU, Kutubu dhambi kwa kumaanisha kuziacha na kupokea Roho Mtakatifu, na kila siku kuishi maisha ya utakatifu.
Kwa njia hiyo basi tutaweza kufikia kilele cha baraka, kwani ni Neema kuu tulipewa ya sisi kuufikia mlima wenye utukufu zaidi ya ule Musa aliopanda.
2 Wafalme 3:16-17
[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki. [17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
[16]Akasema, BWANA asema hivi, Fanyeni bonde hili lijae mahandaki.
[17]Kwa kuwa BWANA asema hivi, Hamutauona upepo, wala hamtaiona mvua, ila bonde hilo litajaa maji; nanyi mtakunywa, ninyi, na ng’ombe zenu, na wanyama wenu.
Ilifika wakati wana wa Israeli, walikwama, baada ya kuona wapo katika eneo ambalo ni kame kupita kiasi, na hawana msaada, nguvu zimewaishia maadui zao wapo karibu kuwaangamiza..
Wakalia sana, Lakini baadaye wakapata akili ya kumlingana Mungu kwa kuulizia kupitia nabii wake Elisha. Lakini maagizo waliyopewa hayakuwa bado marahisi sana, kama walivyotegemea.
Hawakufanyiwa muujiza wa maji kutokea mwambani kama kipindi cha Musa, au mvua kushuka mbinguni…bali waliambiwa wachimbe mahandaki…yaani mashimo makubwa sana…pale jangwani..
Fikiri umechoka umeishiwa nguvu, halafu unaambiwa uchimbe mashimo..upige sururu chini, upige jembe chini, utoe jasho la kutosha si jambo jepesi..
Lakini baadaye tunaona Mungu anawaambia hamtaona mvua bali hayo mabonde yote yatajaa maji. Na ndivyo ilivyokuwa. Kwa waliochimba sana walipata maji sana, kwa waliochimba kidogo walipokea maji sawasawa na mashimo yao.
Je nini Bwana alikuwa analifundisha kanisa lake.
Katikati ya jangwa, Si muda wa kulia na kusumbuka, kinyume chake shika jembe lako, chepe lako anza kuchimba mashimo.
Kwanini watu wengi hawaioni mvua ya Mungu ya neema au baraka za rohoni zikidumu kwao lakini kwa wengine hudumu…sio kwamba Mungu anaupendeleo…hapana…bali wale wengine tayari wameshachimba mashimo marefu ya kuhifadhi maji mengi…Kwasababu mvua au umande wa Mungu sikuzote hushuka au hupanda juu ya nchi yote lakini wale wenye visima ndio hudumu na maji yake mda mrefu kwa wengine hudumu tu kwa muda mfupi pale juu, baadaye kidogo hupotelea ardhini…
Kuchimba handaki ni kudumu sana katika maombi, pamoja na kutendea kazi kile ulichokitaka kwa Mungu…
Kwa mfano unamwomba Mungu akupe mke/mume mwema, labda leo huoni kutokea kwa yoyote upo jangwani tu, unakaribia kukata tamaa…hakikisha unazidisha sana maombi, lakini pia unajitunza na kuanza kujifunza mafunzo ya kuwa mke/mume mwema, unaonyesha kivitendo zile sifa za mke mwema/mume mwema anazopaswa awe nazo kibiblia, kwamfano wewe ni mwanamume unafahamu kuwa yapo majukumu ya kibaba mbele yako, kwamba unapaswa uwajibike kwa kipato cha familia yako, lakini hilo kama hulisumbukii na bado unatarajia Bwana akuletee mke..ni kweli atakuletea, atapandisha umande wa maji juu ya nchi lakini hatimaye atashindwa kudumu na wewe katika hatua za awali akiona huwezi kusimama kwenye wajibu wako…baadaye utalalamika mbona wanawake wananikimbia..vilevile mwanamke akikosa tabia njema..wanaume watakuja na kumkimbia baadaye…kwasababu hakuwa na muda wa kujichimbia mahandaki yake, kitabia.
Kila eneo liwe la kihuduma, kikazi, kiafya..wekeza sana kwenye mahandaki kwasababu mvua/ umande utakuja tu…kwasababu kwa Mungu kushusha baraka si jambo la kulisumbukia sana, yeye anawanyeshea mvua waovu na wema alisema hivyo (Mathayo 5:45) bali kuzihifadhi hizo baraka ndio ugumu ulipo.
Mwanzo 2:6
[6]ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
Wekeza kwenye maombi na kutendea kazi imani yako kwa vitendo. Zaidi ya kutarajia tu Mungu atende mwenyewe.
Bwana akubariki
Umewahi kujua tofauti ya makundi haya mawili ya MBWA?.
Kundi la kwanza Mbwa wanaotembea huru barabarani na kundi la pili ni wale Mbwa wanaofugwa majumbani?.
Utaona Mbwa wanaozurula mitaani bila makao rasmi, huwa hawana afya, wanadharaulika, na ijapokuwa wanao uhuru wa kwenda popote watakapo lakini bado huwa hawana afya huwa ni wenye maradhi.
Utaona mbwa anayekatiza mitaani, ataona vyakula vingi vinapikwa, ataona minofu mingi ikitengenezwa na wanadamu, atasikia harufu ya kila aina ya chakula kizuri lakini hatakula?.
Lakini tukirudi kwa wale Mbwa wanaofugwa majumbani ni kinyume chake.
Wao wana afya kwasababu wanalishwa na wanaowafuga, pia ni jasiri kwasababu wanaaminiwa na wanaowafuga.
Hawana haja ya kuhangaika kutafuta chakula kwani wanaletewa, hawana haja ya kujitibu kwani wanatibiwa na wanaowafuga kwa ufupi wanaishi maisha ya raha isipokuwa tu hawana uhuru wa kuzurula ovyo na kukatiza mitaani.
Ni hivyo hivyo kwa watoto waliotoroka kwao na kuishi mitaani, huwa hawana afya njema, wala ustawi ijapokuwa wana uhuru wa kufika popote watakapo na kufanya chochote watakacho..
Lakini watoto wanaolelewa nyumbani hawana uhuru wa kwenda popote watakapo au kufanya chochote watakacho lakini ndio wenye ustawi mzuri na wanaofanikiwa.
Ni hivyo hivyo kwetu pia, Uhuru wa kufanya chochote na kutenda chochote tutakacho ni uhuru potofu ambao, mwisho wake ni kuharibika na kudharaulika.
Lakini tukikubali kulelewa na MUNGU kama watoto wanaopendwa basi tutafika mbali na kustawi sana.
Kama upo nje ya hifadhi rudi nyumbani kwa baba yako leo, kwa kutubu dhambi na kumkaribisha YESU, Na Bwana atakupokea na kukulea kama mtoto anayependwa sana.
Waefeso 5:1 “Hivyo mfuateni Mungu, kama watoto wanaopendwa”.
Huu ni mfululizo wa masomo yawahusuyo watumishi wa Mungu.
Kuna makosa mengi yapo miongoni mwa mitazamo yetu sisi (watumishi wa Mungu), tunadhani mafanikio ni pale hasaa huduma yetu inaposhawishi mioyo ya wengi …pale tunapoona umati unaipokea, na kuishangilia.
Lakini tukifuatilia huduma za manabii wengi wa Mungu, kwenye biblia kama vile Isaya na Ezekieli, Yeremia hawakuwa na mafanikio makubwa ya mahubiri yao, kama tunavyodhani hivi leo, kinyume chake waliishia kukataliwa, kuteswa na kuuliwa, kwa ufupi huduma zao ziliwavunja sana moyo, lakini kwasababu aliyewatuma ni Bwana, injili yao imesimama vizazi na vizazi mpaka leo..
Walijua wanakwenda kuhubiri kwa watu ambao wana mioyo migumu sana…na Mungu aliwaeleza kabisa, lakini walifanya hivyo kwa uaminifu wote, kana kwamba wanauokoa umati wa watu.
Yeremia 7:27
[27]Nawe utawaambia maneno hayo yote; lakini hawatakusikiliza, nawe utawaita; lakini hawatakuitikia.
Ezekieli 2:3-7
[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo. [4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi. [5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao. [6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi. [7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
[3]Akaniambia, Mwanadamu, nakutuma kwa wana wa Israeli, kwa mataifa wanaoasi, walioniasi mimi; wao na baba zao wamekosa juu yangu, naam, hata hivi leo.
[4]Na wana hao wana nyuso zisizo na haya, na mioyo yao ni migumu. Mimi nakutuma kwa hao; nawe utawaambia, Bwana MUNGU asema hivi.
[5]Nao, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia, (maana ndio nyumba ya kuasi hao), hata hivyo watajua ya kuwa nabii amekuwako miongoni mwao.
[6]Na wewe, mwanadamu, usiwaogope hao, wala usiyaogope maneno yao, ijapokuwa miiba na michongoma i pamoja nawe, nawe unakaa katikati ya nge; usiyaogope maneno yao, wala usifadhaike kwa sababu ya nyuso zao, wajapokuwa ni nyumba yenye kuasi.
[7]Nawe utawaambia maneno yangu, kwamba watasikia, au kwamba hawataki kusikia; maana hao wanaasi sana.
Hakuna jambo linaloumiza kwa mtumishi wa Mungu pale unapoona unahubiria jamii kubwa ya watu lakini matokeo yoyote huoni kwao,…Ni vema ufahamu kuwa Mungu hakutumi ukawe mshawishi, anakutuma ukawe mwaminifu kwa kazi yake.
Kushindwa kwako katika huduma sio, kukosa watu wa kukusikiliza au watu kupungua kwenye huduma yako, kushindwa kwako ni kukosa uaminifu..hilo tu.
Leo hii ungewekwa kwenye nafasi ya Nuhu ambaye aliuhubiria ulimwengu kwa miaka mia moja na ishirini, na kuambulia tu familia yake, ungeshamkimbia Mungu siku nyingi na kusema sijatumwa, ungewekwa kwenye nafasi ya Yeremia, Mika, sefania ungesema huyu si Mungu, ni akili zangu zimenituma, ungesema ninachofanya ni uwendawazimu…hii sio huduma lazima kuna shida mahali, haiwezekani watu hawataki kugeuka, na kutubu, ungewekwa nafasi ya Musa ungesema hawa nilionao sio watu wa Mungu ni kizazi cha nyoka, pamoja na ishara zote na miujiza…lakini bado wanatengeneza ndama wa shaba, wanaasi, wananung’unika…najitaabisha bure tu.
Kama mtumishi wa Mungu jitahidi sana kuwa mwaminifu, hata kama huoni ukuaji wowote, au mafanikio yoyote ya machoni, ya kuokoka kwa watu wengi…wewe ifanye kazi yake, mtumikie yeye, timiza ratiba zako. mtumikie Mungu kwa mtazamo huo wa uaminifu na sio wa matokeo, utadumu na hutapindishwa na chochote.
Kwani thawabu yako ni kubwa mbinguni.
Mungu akubariki sana.
MHESHIMU MCHUNGAJI WAKO.
SIKU ZA WATUMISHI WA MUNGU.
KARAMA TUZIPATAZO KWA MSAADA WA WATU WENGI.
Shedraki, Meshaki, na Abednego, walipokataa kuisujudia sanamu ya mfalme, kama tusomavyo maandiko, walifungwa na kutupwa kwenye tanuru ya moto, lakini wakiwa kule motoni, alionekana mtu wa nne, ambaye mfalme Nebukadreza alimwona kama mwana wa Mungu, ndiye Yesu Kristo mwenyewe.
Danieli 3:24 Ndipo Nebukadreza akastaajabu, akainuka kwa haraka; akanena, akawaambia mawaziri wake, Je! Hatukutupa watu watatu, hali wamefungwa, katikati ya moto? Wakajibu, wakamwambia mfalme, Kweli, Ee mfalme. 25 Akajibu, akasema, Tazama, mimi naona watu wanne, nao wamefunguliwa, wanatembea katikati ya moto hali hawana dhara; na sura yake yule wa nne ni mfano wa mwana wa miungu.
Nachotaka ufahamu ni kwamba mtu wa nne, alikuwa Pamoja nao, siku zote, lakini kufunuliwa machoni pa watu, ilihitaji moto, ikiwa na maana nje ya moto, hakutambulika Dhahiri machoni pa wengi, bali kwa wale tu waliomwamini, tena mioyoni mwao.
Moto ni nini?
Moto, ni shinikizo lolote juu ya Imani ya mtu kwa Yesu Kristo, ambalo wakati mwingine linahatarisha hata maisha yake. Huu moto wengi wanaukwepa lakini hawajui kuwa ndio unaompa Kristo nafasi ya kujifunua zaidi kwenye maisha yako.
Ukiona unataka kufukuzwa kazi kisa, siku za jumapili huwendi kazini unahudhuria ibadani, fahamu kuwa Kristo anaumbika Dhahiri kwenye maisha yako.
Ukiona unahatarisha biashara yako, kisa umegoma kula rushwa, ndivyo Kristo anakwenda kuonekana Dhahiri kwenye kazi zako, ni jambo tu la muda..
Ukiona, unafukuzwa, unapigwa, unafungwa, kwasababu ya msimamo wako mkali wa kimafundisho unaokemea dhambi, ujue kuwa, Kristo anakwenda kusimama na wewe kwa viwango vingine vya juu sana.
Moto kimsingi si mzuri, upitapo ni lazima utasikia maumivu, lakini mbele ya Kristo, hauna nguvu, hivyo vitisho, mapigo, vifungo, dhihaka, havina nguvu yoyote, kwasababu yeye yupo Pamoja na wewe muda huo, ndivyo ilivyokuwa kwa Shedraki, Meshaki na Abednego, hawakuungua kwasababu ya ule moto.
Badili fikra zako, badala ya kuhuzunika kwa majaribu, Bwana anasema furahi, kwasababu huko ndipo viwango vyetu vya kumuona Kristo vipo.
Maran atha.
Kwanini Mungu azungumze na Ayubu kupitia upepo wa kisulisuli (Ayubu 38:1)
VITABU VYA BIBLIA: Sehemu ya 13 (Kitabu cha Hosea).
USIYAKUBALI MARADHI YA MISRI
WhatsApp
Swali: Katika 1Samweli 16:7 tunasoma, MUNGU anamwambia nabii Samweli kuhusu mtu atakayempaka mafuta kama Mfalme katika nyumba ya Yese, kwamba yeye haangalii uso kama wanadamu wanavyoangalia.
Jibu: Turejee..
1Samweli 16:6 “Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake. 7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, USIMTAZAME USO WAKE, WALA UREFU WA KIMO CHAKE; KWA MAANA MIMI NIMEMKATAA. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; MAANA WANADAMU HUITAZAMA SURA YA NJE, BALI BWANA HUUTAZAMA MOYO”.
1Samweli 16:6 “Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake.
7 Lakini Bwana akamwambia Samweli, USIMTAZAME USO WAKE, WALA UREFU WA KIMO CHAKE; KWA MAANA MIMI NIMEMKATAA. BWANA HAANGALII KAMA BINADAMU AANGALIAVYO; MAANA WANADAMU HUITAZAMA SURA YA NJE, BALI BWANA HUUTAZAMA MOYO”.
Andiko hili linalenga MAUMBILE ya ASILI ya Mtu, kwamba hayo ndio MUNGU hayaangalii kama kipimo cha kumpatia mtu “haki” au “hukumu”, na mambo hayo ni kama rangi ya mtu, urefu, ufupi, ulemavu, au uzima..
Mambo hayo hayatutofautishi sisi kwa sisi mbele za MUNGU. Kwamba ukiwa mfupi au mrefu au mweupe au mweusi basi ndio unaweza kupata kibali mbele za MUNGU. La!, hayo ni mambo ambayo MUNGU hayaangalii kabisa..
Lakini jinsi tunavyoiweka miili yetu, na kuivisha na kuilisha na kuinywesha ni vitu ambavyo MUNGU anavitazama sana kwasababu vipo ndani ya uwezo wetu, lakini urefu na ufupi hakuna mtu anajipangia, ni maumbile ya asili ya MUNGU mwenyewe.
Kwahiyo mtu anapovaa mavazi ya jinsia nyingine, au yanayouchora mwili wake, hayo yanajalisha sana mbele za MUNGU (1Timotheo 2:9, Kumbukumbu 22:5), au mtu anapojichubua au kujichora mwili wake Mungu anatazama (Soma Walawi 19:28).
Kwahiyo Bwana MUNGU, aliposema Haangalii uso, maana yake hashawishwi na maumbile ya asili ya mtu. Je umempokea YESU?. Una hakika YESU akirudi leo utakwenda naye?.
Kama bado haujampokea YESU unasubiri nini? Mwamini leo na ubatizwe kwa maji na kwa Roho Mtakatifu.
TAFUTA UTAKASO WA SEHEMU KUU NNE ZA MWILI WAKO.
Je! Yesu aliwezaje kuchukuliwa na shetani juu ya kinara cha hekalu kujaribiwa?
MWIMBIE BWANA ZABURI KATIKA NYAKATI ZA FURAHA.
TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO.
NI NANI TUNAPASWA TUMWONE ZAIDI KILA TUSOMAPO BIBLIA?
Wagalatia 1:10
[10]Maana, sasa je! Ni wanadamu ninaowashawishi, au Mungu? Au nataka kuwapendeza wanadamu? Kama ningekuwa hata sasa nawapendeza wanadamu, singekuwa mtumwa wa Kristo.
Kuna dhambi moja ya kale, ambayo imekuwa sugu sana, na kibaya zaidi imekuwa tishio kubwa kwa mwanadamu, hata kumfanya ashindwe kabisa kuyatenda mapenzi ya Mungu, haijalishi atamaanisha kiasi gani, dhambi yenyewe si zile tunazozifahamu, kama vile uzinzi, uongo, n.k., Hapana bali ni dhambi ya “kuwapendezesha wanadamu”
Ni dhambi ya kufanya jambo kwa hofu ya kuchukiwa na watu, kufikiriwa vibaya na watu. Hofu ya Kutengwa na watu, kudharauliwa na watu.
Ni kufanya jambo machoni pa watu ili utukuzwe, uonekane mkuu, uonekane ni wa rohoni, uonekane unajua kuliko wengine… ni kuwa radhi kuvumiliana na vilivyo kinyume na Mungu ilimradi tu mbele za watu, usipoteze heshima yako.
Bwana Yesu alijua moyo wa mwanadamu unafurahia hali hii, upo radhi kufanya vitu kinafki, bila kujali haja ya Mungu ni nini.
Mathayo 6:2,5
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu… [5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
[2]Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu…
[5]Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin, nawaambia, Wamekwisha kupata thawabu yao.
Ni hali mbaya sana, Mahali pengine waliogopa kumkiri hadharani kwasababu watapoteza heshima zao za kikuhani machoni pa watu..
Yohana 12:42-43
[42]Walakini hata katika wakuu walikuwamo wengi waliomwamini; lakini kwa sababu ya Mafarisayo hawakumkiri, wasije wakatengwa na sinagogi.
Madhara ya dhambii hii ni kwamba, Tunaweza tukayapindisha maandiko tusiongee ukweli wote, tuhubiri injili ya juu juu, injili ya vichekesho, tusikemee aina Fulani ya dhambi kwasababu zitawafanya watu wainamishe vichwa vyao, matokeo yake wasije kanisani.
Hali hii inatufanya tuwe na kigeugeu, ilimvaa hata Petro, wakati ule alipoketi na wayahudi, anasema hivi, alipokutana na Watu wa mataifa anasema vingine kwa hofu ya wayahudi, mpaka Paulo alipomwona akamkemea mbele ya wote. (Wagalatia 2:11)
Tunaogopa kuvaa mavazi ya kujisitiri yasiyokuwa na mvuto machoni pa watu, lakini mbele za Mungu yanapendeza, kisa tutaonekana washamba, wazee. Nuru yetu inashindwa kuangaza ulimwenguni.
Ijapokuwa Bwana Yesu aliwapenda sana wanadamu, lakini hakuishi kwa kuziangalia hisia zao zinasemaje, kwasababu sifa za wanadamu, hazitabiriki, leo watakusifia, kesho watakuchukia.. Alipoingia Yerusalemu walimwita mbarikiwa Hosana, wiki moja baadaye wakasema Asulubiwe.. Lakini katika nyakati zote hizi hatuoni Bwana Yesu akigeuka, akipindisha pindisha msimamo wake, alipotukanwa, hakutazama umati unasemaje, aliutazama utukufu wa Mungu unamwelekezaje.
Hii huitwa hofu ya mwanadamu, Tunasahau kuishi kwa hofu ya Mungu, yaani Mungu anasemaje, Anajisikiaje, tunawaza sana wanadamu wanasemaje, wanafikirije..Hatupaswi kuwafanya watu sanamu zetu.
Ili tushinde hii hali kwanza ni lazima tujue kuwa kumpendezesha kila mtu ni jambo ambalo haliwezekani, hivyo usiogope kufikiriwa kivingine pale unapokusudia kuishi maisha yampendezayo Mungu.
Lakini pia ni lazima ufahamu, wanadamu hawana sifa za kweli, za kudumu, hivyo acha kufanya vitu, kuwaridhisha, ilihali unajua wewe mwenyewe unaumia ndani kwa ndani, na mwisho jitahidi kufanya mambo yako kwa msukumo wako mwenyewe sirini, bila watu kukutazama, hapo utaua sifa za wanadamu, utaanza kuishi kwa kumwangalia Mungu.
MWONGOZO WA MAOMBI YA WAHUDUMU/ WASIMAMAO MADHABAHUNI.
Kuwaogopa wanadamu huleta mtego,(Mithali 29:25)
USIONDOE ALAMA YA MPAKA ILIYOWEKWA NA MABABA.
Huu ni mfululizo wa masomo maalumu ya wanawake, ikiwa utapenda kupata madarasa mengine mengi ya nyuma wasiliana nasi kwa namba zilizo chini ya somo hili.
Mariam ni mwanamke ambaye Mungu alimchagua kipekee kuwa mfano bora wa kuigwa wa namna wanawake wa kikristo wanavyopaswa kuwa.
Mariamu alijitunza usichana wake, lakini pia sifa nyingine kubwa aliyokuwa nayo, hakuwa mtu wa kuwaza ki-akili bali aliwaza kwa moyo. Kila jambo lililomfikia halikuishia akilini tu, kwamba ni hoja nzuri tu, au kwamba inaingia akilini, hapana bali alijifunza kulishusha mpaka moyoni, kulitafakari …Na hilo lilimsaidia sana kuwa mwanamke bora…
Embu tafakari haya matukio machache, mwitikio wake ulivyokuwa;
Luka 1:28-29
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe. [29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
[28]Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema, Bwana yu pamoja nawe.
[29]Naye akafadhaika sana kwa ajili ya maneno yake, akawaza moyoni, Salamu hii ni ya namna gani?
Luka 2:17-19
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto. [18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji. [19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
[17]Walipomwona wakatoa habari waliyoambiwa juu ya huyo mtoto.
[18]Wote waliosikia wakastaajabu kwa hayo waliyoambiwa na wachungaji.
[19]Lakini Mariamu akayaweka maneno hayo yote, akiyafikiri moyoni mwake.
Luka 2:48-51
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni. [49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu? [50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia. [51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
[48]Na walipomwona walishangaa, na mama yake akamwambia, Mwanangu, mbona umetutenda hivi? Tazama, baba yako na mimi tulikuwa tukikutafuta kwa huzuni.
[49]Akawaambia, Kwani kunitafuta? Hamkujua ya kuwa imenipasa kuwamo katika nyumba ya Baba yangu?
[50]Nao hawakuelewa na neno hilo alilowaambia.
[51]Akashuka pamoja nao mpaka Nazareti, naye alikuwa akiwatii; na mamaye aliyaweka hayo yote moyoni mwake.
Hiyo ni kuonyesha ilikuwa ni desturi ya maisha yake, kufikiri kutoka kilindi cha moyoni mwake sio kwa akili zake…
Wazia zaidi, Mariamu aliposalimiwa alijiuliza salama hii, lengo lake ni nini? nyuma ya salamu kuna lengo gani, Mwisho wake ni upi.. hakupokea salamu, ilimradi salamu kisa inamtakia mema…aliivunja vunja kwanza..Na huko ndio kuwaza kwa moyo.
Mabinti wengi leo hii wanaingia kwenye mitego ya kulaghaiwa kwa kutowaza kutoka moyoni..hujiulizi iweje mtu usiyemjua aje kukupa tu salamu ya zawadi, akusifie, na wewe hufikiri salamu hii ni ya namna gani…
Hujiulizi huyu mtu nia yake ni nini? Anatarajia nini kwangu, kumbuka salamu sio lazima tu ije kwa maneno, yaweza kuja kwa kupewa lifti, kupewa nafasi ya upendeleo, kulipiwa manunuzi fulani, dada kuwa makini na salamu hizo, hata kama umeolewa kuwa makini sana. Ni kweli si zote ni mbaya lakini jiulize maudhui yake ni nini? Waza moyoni mwako, Nia ni nini?.
Kama mama yetu Hawa pale bustanini angejiuliza salamu za nyoka ni za namna gani, sote tusingekuwa kwenye matatizo tuliyonayo sasa.
Halikadhalika Mariamu, hakuyaacha maneno yenye jumbe za Mungu yampite hivi hivi, mahali ambapo hajaelewa alihifadhi ndani yake akitumai upo wakati ataelewa vema kwa jinsi anavyozidi kutafakari…alihifadhi matukio yake yote moyoni..
Lakini wanawake wengi wa leo, wanahifadhi maneno yasiyo na maana, utaona moyoni mwao yamejaa maneno waliyosengenywa, waliyoaabishwa, waliodhalilishwa..hayo ndio yanawaganda lakini si maneno ya Mungu..
Wanatumia vibaya nafasi hizo, Na matokeo yake kinachotoka nje ya mioyo yao ni wivu, uchungu, hasira, chuki, masengenyo, badala ya mafunuo, upendo, hekima, na adabu.
Tumia moyo wako kwa lengo la kupambanua na kuhifadhi mambo mema…sio maovu.
Ifike wakati, unasema…lile hubiri lililohubiriwa mwaka juzi mpaka leo linanitafakarisha, lile ono Mungu alilonionyesha utotoni linanirudia rudia akilini, yale maonyo ya mhubiri tuliyokemewa kipindi kile yanazunguka ndani yangu hata sasa siwezi yasahau…
Hayo ndio mambo ya kubeba..
Geuka fikiri kama Mariamu..
Shalom
MAOMBI MAALUMU YA WA-WAMAMA / WANAWAKE WA KANISANI.
MAPAMBO YA WANAWAKE WALIOUKIRI UCHAJI WA MUNGU.
MASOMO MAALUMU KWA WANAWAKE.
Utakaso wa ndani ni jambo endelevu.. hakuna hatua ambayo mtu amefika na kusema hapa sasa nimekamilika na sihitaji tena kujitakasa.. hakuna, lakini Biblia inatufundisha kuwa ni lazima tujitakase utu wetu wa ndani na kuwa wapya siku baada ya siku.
2Wakorintho 4:16 “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, LAKINI UTU WETU WA NDANI UNAFANYWA UPYA SIKU KWA SIKU”.
Na tena katika Ufunuo, maandiko yanasema “Mtakatifu na azidi kutakaswa (Ufunuo 22:11)”…
Sasa tunahoji kama Mtakatifu ameshakamilika kuna haja gani tena ya kuendelea kutakaswa?..Umeona?.. maana yake mtakatifu ni lazima aendelee na utakaso, ijapokuwa anaitwa “Mtakatifu” hakuna mahali atafika na kusema sasa nimekamilika..
Kila hatua ya usafi tunayoifikia inatufungua macho kuona uchafu mwingine uliopo ndani, na tunashughulika na huo, na mwingine na mwingine..mpaka siku ya ukombozi wa miili yetu (Waefeso 4:30).
Sasa twende mbele zaidi kuangalia vitu gani vinavyomtakasa mtu.
1. ROHO MTAKATIFU.
Roho Mtakatifu ndio sabuni ya kwanza ya kuondoa uchafu ndani ya Mtu ndio maana kuna umuhimu sana wa Mtu kupokea ujazo wa Roho Mtakatifu baada ya kuamini.
1Petro 1:2 “kama vile Mungu Baba alivyotangulia kuwajua katika KUTAKASWA NA ROHO, hata mkapata kutii na kununyiziwa damu ya Yesu Kristo. Neema na amani na ziongezwe kwenu”.
Soma pia 1Wakorintho 6:11 na Warumi 15:16.
Kanuni ya Ujazo wa Roho Mtakatifu ni ile tunayoisoma katika Matendo 2:37-38, yaani kutubu kwa kumaanisha kuacha dhambi na ubatizo wa maji mengi kwa jina la Bwana YESU.
2. NENO LA MUNGU
Maneno ya MUNGU yaliyoandikwa ndani ya kitabu ya Biblia ndio sabuni ndio sabuni ya pili kumtakasa mtu maisha yake. Bwana YESU alisema, tunatakaswa na kweli ya Neno la MUNGU.
Yohana 17:17 “Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli”.
Soma pia Waefeso 5:26..
Mtu mwenye desturi ya kusoma Neno la Mungu ni lazima kila siku atakuwa anayaona makosa yake, lakini mtu asiyesoma Neno la Mungu kila siku atajiona yupo sawa na hahitaji kujitakasa wala kurekebishwa. Kwanini? Kwasababu Neno la Mungu ni kama kioo, mtu huwezi kujua uso wako upoje kama hujitazami kwenye kioo (Yakobo 1:22-23).
3. MAOMBI.
Maombi yanatakasa utu wa ndani katika kiwango kikubwa sana.. na si tu utu wa ndani bali vitu vyote pia..
1Timotheo 4:5 “kwa kuwa kimetakaswa kwa neno la Mungu na kwa kuomba”.
Kiwango cha mtu kukua kiroho pia kinapimwa na kiwango cha Maombi, mtu anayeongeza viwango vyake vya maombi kila siku ni mtu pia anayekua kiroho.