Ni maombi yangu kuwa utachagua njia ya uzima, kama hujampa Bwana Yesu Kristo maisha yako, ndio wakati wakufanya hivyo sasa, usisubiri leo ipite, kwasababu hujui lisaa limoja mbele nini kitatokea, hapo ulipo mwambie Bwana akusamehe makosa yako yote, na mwambie hutaki tena kuishi maisha ya dhambi, na baada ya kuomba sala hiyo, dhamiria ndani ya moyo wako kuacha dhambi kweli kweli, dhamiria kuacha pombe, sigara, rushwa, uasherati, uvaaji mbaya wa vimini na suruali na mapambo ya kidunia hii, dhamiria kuacha kampani mbovu, na mambo mengine yote yasiyofaa..Ukimaanisha kutoka moyoni mwako kuacha hayo mambo, nguvu ya ajabu itashuka juu yako kukusaidia kuyashinda hayo mambo yasikurudie tena…na ukishamaliza hiyo hatua nenda mahali popote wanapoamini ubatizo sahihi wa maji mengi na kwa jina la Yesu Kristo, ubatizwe hapo, na Bwana mwenyewe atakusaidia kufanya yaliyosalia..