Areopago ni nini? Kwanini mtume Paulo walimpeleka huko?

by Admin | 13 September 2020 08:46 am09

Areopago ni nini?


Areopago ni baraza kuu la Waathene au mahali walipokutanika wakuu wa Athene. Kwa ajili ya kuzungumza mambo mbalimbali ya muhimu,kama vile kusikiliza   kesi zinazohusiana na mauaji au dini,  au kutoa hukumu, au kuchambua mambo mengine yenye uzito katika jamii.

Eneo hili lilikuwa upande wa kaskazini magharibi mwa mji wa Athene,Ukigiriki, na lilijengwa ya juu ya mwamba mkubwa.

Baraza hili, lilifanana na lile baraza la wayahudi ambalo, wazee pamoja na kuhani mkuu walikuwa wanakutanika kutoa mashahuri juu ya kesi za kidini, kama vile ilivyokuwa wakati wa Bwana Yesu (Mathayo 26:57-68)

Sasa Mtume Paulo alipofika katika mji huu na kuanza kuhubiri, tunaona baada ya habari zake kusikika sana katikati ya jamii ya waethene, walimkamata na kumpeka mbele ya baraza hili kuu (Areopago) ili kumsikiliza vizuri juu ya imani yake.

Tusome:

Matendo 17:16 “Paulo alipokuwa akiwangojea huko Athene na kuona jinsi mji ule ulivyojaa sanamu, roho yake ilichukizwa sana ndani yake.

17 Basi katika sinagogi akahojiana na Wayahudi na waliomcha Mungu, na wale waliokutana naye sokoni kila siku.

18 Na baadhi ya Waepikureo na Wastoiko, wenye ujuzi, wakakutana naye. Wengine wakasema, Mpuzi huyu anataka kusema nini? Wengine walisema, Anaonekana kuwa mtangaza habari za miungu migeni, kwa maana alikuwa akihubiri habari za Yesu na ufufuo.

19 Wakamshika, wakamchukua AREOPAGO, wakisema, Je! Twaweza kujua maana ya elimu hii mpya unayoinena?

20 Kwa maana unaleta mambo mageni masikioni mwetu, tutapenda kujua, basi, maana ya mambo haya.

21 Kwa maana Waathene na wageni waliokaa huko walikuwa hawana nafasi kwa neno lo lote ila kutoa habari na kusikiliza habari za jambo jipya.

22 Paulo akasimama katikati ya AREOPAGO, akasema, Enyi watu wa Athene, katika mambo yote naona ya kuwa ninyi ni watu wa kutafakari sana mambo ya dini.

23 Kwa sababu nilipokuwa nikipita huko na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, naliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua……

32 Basi waliposikia habari za ufufuo wa wafu wengine walifanya dhihaka; wengine wakasema, Tutakusikiliza tena katika habari hiyo.

33 Basi hivi Paulo akaondoka akawaacha.

34 Baadhi ya watu wakashikamana naye, wakaamini; katika hao alikuwamo Dionisio, MWAREOPAGO, na mwanamke mmoja jina lake Damari, na watu wengine pamoja na hao”.

Kama tunavyoona wapo miongoni mwa hao wakuu wa baraza wapo waliodhihaki, na wapo walioamini kama vile huyo Dionisio mwareopago.

Je Ma-areopago yanaendelea mpaka sasa?

Ndio, Hata sasa katika agano jipya ma-areopago yapo mengi, Bwana Yesu alishayazungumzia na kuonya kuwa watakatifu watakutana nayo katika safari zao za Imani, na katika kuhubiri injili.. Lakini Bwana Yesu alitupa kanuni ya kusimamia, akasema hivi;

Mathayo 10:17 “Jihadharini na wanadamu; kwa maana watawapeleka mabarazani, na katika masinagogi yao watawapiga;

18 nanyi mtachukuliwa mbele ya maliwali na wafalme kwa ajili yangu, kuwa ushuhuda kwao na kwa mataifa.

19 Lakini hapo watakapowapeleka, msifikiri-fikiri jinsi mtakavyosema; maana mtapewa saa ile mtakayosema.

20 Kwa kuwa si ninyi msemao, bali ni Roho wa Baba yenu asemaye ndani yenu”.

Hivyo, kama umeokoka,au unahubiri injili na ukajikuta umewekwa katikati ya viongozi wa dini, hupaswi kuogopa Areopago lolote..Kwasababu Bwana ameahidi kuwa na wewe.

Shalom.

Tafadhali washirikishe na wengine habari hizi njema, na pia kama utapenda tuwe tunakutumia mafundisho ya Neno la Mungu ya mara kwa mara kwa njia ya email yako au Whatsapp basi tutumie ujumbe kwenye namba hii +255 789001312

Mada Nyinginezo:

KWA MUNGU ASIYEJULIKANA.

SIRI YA KUFANIKIWA KWA MTUME PAULO.

JIFUNZE KULIGAWANYA VYEMA NENO LA MUNGU.

Israeli ipo bara gani?

Mto Frati upo nchi gani, Umuhimu wake katika biblia ni upi?

SIKU YA UNYAKUO ITAKUKUTAJE?

Rudi Nyumbani:

DOWNLOAD PDF
WhatsApp

Source URL: https://wingulamashahidi.org/2020/09/13/areopago-ni-nini-kwanini-mtume-paulo-walimpeleka-huko/